Kuna watu tunaimani na mwanahalisi kuliko hata serikali yetu

Mkuu kumbe na wewe umemgundua. Najaribu kutafuta kigezo alichotumia kufananisha Chombo cha habari na Serikali nashindwa hata kumueka kundi gani, ni mshabiki? ni mjinga? ni chizi? au basi tu kama ulisema mkuu ,kuwa ni wale wale wakiulizwa leo ni nchi ipi ina mgogoro na Tanzania kuhusu ziwa Nyasa atajibu Zanzibar. What is Mwanahali? au kwa vile linamilikiwa na kiongozi wa CHADEMA? Kumbe unaweza kuwa mpenzi wa kitu fulani hadi ukawa kama roboti. Hawa ndiyo wanaotumiwa kutafuta mabadiliko ili baadaye nchi itumbukie shimoni, hivi mtu kama huyu leo hii kukawa na mabadiliko yanayosemwa atakuwa anajua nini maana yake ? Kazi ipo.
kiongozi wa chadema anamiliki mwanahalisi.......hebu funguka mkuu,,,
 
Tatizo hpa JF mtu akiongea mambo ya msingi anapondwa, Father kasema kweli. Kwanza wewe Kakubilo siamini kama wewe ni Mtanzania, siyo Wanyasa wa Malawi mnaotusumbua kule Ziwa Nyasa?. Unamtetea Kubenea kwa madudu yake, eti anahojiwa BBC kwa nini amefungiwa anasema "kwa sababu naandika habari za kiuchungi ambazo vyombo vingine vinaopopa kuandika" Alifikiri BBC wametandaza nafasi za kazi akaanza kuponda wanahabari wenzake ili yeye apate kazi nini?
hapo kwenye red....panaonesha tatizo lenu mnaotumiwa km t.paper na mafisadi kutoka DHAIFU
 
mtu anae simama kwenye ukweli,jasiri na mzalendo kwanini asiaminike.Kubenea na timu nzima ya Halisi publishers wanastahili tunzo ya ushujaa
 
binafsi naungana na wewe katika hili kwa takribani 98%. ila usiwashangae wenye maoni ya kuponda huwa hawakosi. hivi, kama anayesoma hii thread ni Jack Zoka au Ramadhani Ighondu au ndugu zao wa karibu, unategemea watakubaliana na wewe????? hata mtoto wa jambazi huwa anathamini kazi ya baba yake japo ni haramu. binadamu kiumbe wa ajabu sana. mwanahalisi wameweka kila kitu hadharani, bado anakuja mtu anasema uzushi, ukimwambia athibitishe uzushi kwa hoja au aende mahakamani kama ni uzushi, anaanza kuumauma vidole kama binti anatongozwa na pengine hata kukutukana matusi!!!!!! duh!! Binadamu!!!!???
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom