S.N.Jilala
JF-Expert Member
- Jan 26, 2012
- 540
- 507
Niko wilaya ya Meatu jimbo la KISESA ambalo liko chini ya mbunge wa CCM bwana Luhaga Mpina.Nimezunguka vijiji kazaa,wananchi wanasema jimbo letu ndilo la kwanza kuchagua upinzani ndani ya wilaya ya Meatu iliyo na majimbo mawili moja la KISESA NA LINGINE LA MEATU ambalo liko chini ya CHADEMA.Wanasema walimkataa Erasto Tumbo (2010) ambaye alikuwa mbunge wa UDP kwa sababu alikuwa hasikilizi shida zao,pia ilikuwa ni nadra kumuona jimboni kwake. Wanasema iliwalazimu warudie kuichagua CCM kwa sababu mpinzani alikuja Erasto Tumbo ambaye walishaapa hawatamchagua kwa sababu aliwasaliti alipokuwa mbunge kupitia UDP. Lakini wanasema HAKIKA MBUNGE WETU NI KUPITIA CCM SI KWAMBA TUNAMPENDA NA CCM YAKE bali hawakuwa na chaguo mbadala. Na wengi wao kila kikundi wakiwa wanapiga stori utakuta wanasema CHADEMA NDIYO CHAGUO LETU KWA SASA KAMA UCHAGUZI UTAITISHWA NA TUNASUBIRI 2015 na mbunge wetu itabidi asome upepo huu. Mwisho wanasema wanaipenda CHADEMA si kwa sababu ni wema sana bali wao WANAONGEA MAMBO MUHIMU KWAO NA WANAONEKANA KUUMIZWA NA UMASIKINI WETU.Pia wanahitaji mtu makini kupitia CHADEMA ambaye atakuwa anasikiliza na kutenda kama mbunge.My take: Inawezekana mbunge wao wanampenda lakini CHAMA NDO TATIZO KUBWA.Hakika mambo si shwari tena huku vijijini kwa CCM,watu wameanza kutoa hofu kabisa na wanasema wao hawaogopi chochote kwani hofu ndo adui aliyekuwa anawasumbua na kwa sasa HAWANA HOFU TENA NA WAKO TAYARI KUDAI HAKI ZAO KWA NJIA SAHIHI.