Ngambo Ngali
JF-Expert Member
- Apr 17, 2009
- 3,517
- 1,359
Kupiga kura ni muhimu, USIACHE. Kuacha kupiga kura ni kuhalalisha wapiga kura wenzako wakuchagulie kiongozi wako mia kwa mia. Sasa jiulize, je yule mlevi anayesumbua kila usiku mtaani akipigana na mkewe ndio mwenye hekima ya kukuchagulia wewe kiongozi wako? Hapana. Je yule kibaka mvuta bangi aliyeshindikana, baada ya kuhongwa tshirt, ndiye mwenye busara kuliko wewe ya kujua mgombea yupi anafaa kuwa kiongozi? Hapana.
Kupiga kura ni hatua ya kwanza katika kuhakikisha tunapata viongozi wazuri. Lakini tusiishie hapo. Tunatakiwa tudai kuwe na uchaguzi ulio huru na wa haki. Yaani mgombea ambaye anakubalika na wengi ndio mwisho wa siku anatangazwa kuwa mshindi. Tunatakiwa kudai sheria za uchaguzi ziboreshwe ili wagombea wote watendewe haki. Mfano pawepo na ukomo wa matumizi ya pesa kwenye kampeni za uchaguzi na kila mgombea atueleze hizo pesa amezitoa wapi. Hii itazuia watu wenye pesa ambao hawakubaliki kutumia udhaifu wa watu maskini kuwarubuni wakati wa uchaguzi.
Aidha, Kwa ujumla wetu tunatakiwa kuishinikiza Tume ya Uchaguzi (NEC) ili kila mwananchi apate fursa ya kupambanua kwa uhuru kabisa ni mgombea yupi anayefaa na haki itendeke kura yake ihesabike. Kuna mapungufu mengi katika chaguzi zetu lakini NEC inayafumbia macho kwa makusudi kabisa. Mapungufu haya yakiondolewa CCM haitakuwa inashinda kwa kiulani kama ilivyo sasa. Kwa kuwa viongozi wa NEC wanateuliwa na rais basi wameamua kula ngumu. Tunatakiwa tudai kuwe na Tume ya Uchaguzi iliyo huru na itakayoshirikisha wadau wote.
Mapungufu yako mengi nitataja kadha. Mfano NEC bado inang'ang'ania kwamba kura lazima zihesabiwe ndani ya majengo/majumba ya serikali kama vile mashuleni na kwenye zahanati. Kwa mijini hi ni sawa lakini huko vijijini huu ni usumbufu mkubwa. Utakuta kwenye kituo kimoja kumeandikishwa wapiga kura elfu mbili au zaidi ambao wametapakaa katika kila kona ya kijiji. Sasa mwananchi wa kijijini akitaka kupiga kura ni lazima atembee umbali mrefu wengine hata kilomita kumi na zaidi. Hii inakatisha tamaa. CCM kwa vile wana pesa wanakodi malori kusafirisha wapiga kura wao siku ya uchaguzi (Biharamulo). Nchi zingine za Afrika ambazo ni maskini kama sisi wameshaachana na huu mtindo. Kwa mfano Ghana wanapiga kura msimu ambao sio wa mvua na kura zinahesabiwa chini ya mti kwa uwazi kabisa mbele ya kadamnasi. Hivyo kila Kitongoji kinakuwa na kituo chake cha kupiga kura na wanaojitokeza kupiga kura ni asilimia kubwa.
NEC vilevile imekataa kujihusisha na kutoa elimu ya uraia kwa wapiga kura. Utawezaje kuwa na mpango unaotumia mabilioni ya fedha wakati wanaohusishwa na huo mpango ni mambumbumbu kuhusu mpango wenyewe? Mgombea anapanda jukwaani anatishia na kusema wapinzani hawajashika dola hivyo mkiwachagua serikali haitaleta maendeleo na wao wanaamini. NEC iko kimya. Mabalozi na Madiwani wanapita mtaani kukusanya shahada za wapiga kura in exchange na vocha za mbolea (Mbeya Vijijini). Mabalozi wa nyumba kumikumi wanajua wapinzani ni akina nani na wanajua ni shahada zipi za kukusanya. Wanakamatwa red-handed (Busanda) wanapelekwa polisi, NEC wanasema hilo haliwahusu ni kosa la jinai, wanakataa kutoa ushirikiano, kesi zinafutwa kutokana na kutokuwa na ushahidi wa kutosha. Madhehebu ya kidini (TUCTA wako mbioni) wameliona hilo ombwe lililotengenezwa na NEC na sasa wametoa waraka unaotoa elimu ya kiraia, huu ni mwanzo mzuri sana. Kingunge ingefaa aelekeza nguvu zake katika kuikarapia NEC kutotimiza wajibu wake mpaka imefikia pahali inaanza kuingiliwa kazi yake.
Sasa NEC wanatuambia hawajui kwanini asilimia 40% (mpaka 60% kwenye chaguzi ndogo) ya waliojiandikisha hawapigi kura. Wamepanga kuleta kampuni ya kigeni ije ifanye utafiti. Hawa wazungu wasiojua siasa za Tanzania waende huko vijijini wakapokelewe na haohao mabalozi wa nyumba kumikumi waonyeshwe ni akina nani wakuwahoji. Majibu ya huo utafiti tayari wengine tunayajua. Tunaendelea kupoteza kodi zetu kwa mambo ya kifisadi yasioyokuwa na tija kwetu. Hamtoi elimu ya uraia halafu mnashangaa kwanini watu hawapigi kura? Hivi ni vichekesho.
Ndugu Chrispin sina lengo la kukukatisha tamaa ila naona ni muhimu kueleza hali halisi ikoje maana wengi hawaifahamu. Lakini cha msingi ni kwamba tunatakiwa tuongeze nguvu na sio kukata tamaa. Haya mazuri tunayoyataka hututaletewa kwenye kisahani, inabidi tuwe ngangari. Kwani huwezi kudai haki haitendeki wakati umejitoa kwenye mchakato wenyewe ambao unaiminya hiyo haki. Tupige kura, tuhamasishe wengine nao waende kupiga kura, ambao hawajajiandikisha tuwahimize wakajiandikishe, tuelemishe wasiofahamu ni nini elimu ya uraia na mwisho tudai tume huru na sheria za uchaguzi zinazotoa haki ili yule wengi wetu tunayemtaka ndiye mwisho wa siku awe kiongozi wetu.
Umenena kuongeza ni kuharibu tutafakari hizi bold zikifanyiwa kazi anachotaka chrispin kitakuwa