Mpita Njia
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 6,997
- 1,163
Ni kweli katika miaka 50 tangu kupata Uhuru wetu kuna mafanikio yamepatikana. Ni lazima kumshukuru Mungu na wale waliofanikisha kupatikana kwa mafanikio hayo. Lakini ninapotakari na kujiuliza, sioni uwiano wa mafanikio hayo na kipindi hicho cha miaka 50. Sijaweza kupima kwa uhakika, lakini naamini kuwa kiwango cha mafanikio haya ya miaka 50, kama ingekuwa tumefanya mambo vile inavyotakiwa, yasingetuchukua hata miaka kumi kuyapata.
Najiuliza; kama kwa miaka 50 tumepata mafanikio machache kiasi hicho, kuna maana gani kusherehekea miaka 50 ya Uhuru? Kwa nini tusitumia maadhimisho ya mwaka huu kutafakari na kujipanga vizuri zaidi ili baada ya miaka kumi ijayo tuwe tumepata mafanikio zaidi ya haya tuliyoyapata katika miaka 50 iliyopita?
Najiuliza; kama kwa miaka 50 tumepata mafanikio machache kiasi hicho, kuna maana gani kusherehekea miaka 50 ya Uhuru? Kwa nini tusitumia maadhimisho ya mwaka huu kutafakari na kujipanga vizuri zaidi ili baada ya miaka kumi ijayo tuwe tumepata mafanikio zaidi ya haya tuliyoyapata katika miaka 50 iliyopita?