Gosbertgoodluck
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 2,855
- 401
Ndugu zangu,
Jana tukiwa katika mapumziko ya Jtatu ya Pasaka tulikuwa na mjadala kuhusu mabaya na mazuri ya Edward Lowassa. Kulikuwa na makundi mawili. Kundi la kwanza lilikuwa na msimamo kwamba hakuna lolote na maana alilofanya EL katika nchi hii zaidi ya kuifilisi. Kundi la pili lilimwelezea EL kama miongoni mwa viongozi ambao wapo tayari kusimamia maamuzi yao kwa manufaa ya wananchi. Kundi hilo lilitaja kwa uchache Mradi Mkubwa wa Maji wa Ziwa Victoria, ujenzi wa shule za sekondari za Kata na Sakata la City Water kama miongoni mwa mambo aliyoyasiamamia kwa ukamilifu kwa manufaa ya wananchi.
Kundi linalomfagilia EL lilifikia hatua ya kusema eti kuwepo kwake kwenye serikali ya kikwete angalau kulileta heshima fulani mbele ya wananchi na kwamba tangu alipoondoka kufuatia sakata la Richmond serikali ya kikwete iliyumba na ikapwaya kiasi cha kuonekana haifai mbele ya wananchi. Je, kuna ukweli kiasi gani kuhusu hoja hii?
Jana tukiwa katika mapumziko ya Jtatu ya Pasaka tulikuwa na mjadala kuhusu mabaya na mazuri ya Edward Lowassa. Kulikuwa na makundi mawili. Kundi la kwanza lilikuwa na msimamo kwamba hakuna lolote na maana alilofanya EL katika nchi hii zaidi ya kuifilisi. Kundi la pili lilimwelezea EL kama miongoni mwa viongozi ambao wapo tayari kusimamia maamuzi yao kwa manufaa ya wananchi. Kundi hilo lilitaja kwa uchache Mradi Mkubwa wa Maji wa Ziwa Victoria, ujenzi wa shule za sekondari za Kata na Sakata la City Water kama miongoni mwa mambo aliyoyasiamamia kwa ukamilifu kwa manufaa ya wananchi.
Kundi linalomfagilia EL lilifikia hatua ya kusema eti kuwepo kwake kwenye serikali ya kikwete angalau kulileta heshima fulani mbele ya wananchi na kwamba tangu alipoondoka kufuatia sakata la Richmond serikali ya kikwete iliyumba na ikapwaya kiasi cha kuonekana haifai mbele ya wananchi. Je, kuna ukweli kiasi gani kuhusu hoja hii?