BRUCE LEE
JF-Expert Member
- Dec 11, 2010
- 2,096
- 1,332
Ndugu zangu wana jamvi mi kuna jambo linanitatiza kuhusu huyu mnajibu wa kimataifa, kipindi cha mkapa aliwahi kusema kua wananchi wanampenda sana mkapa na watamuomba aendelee kuongoza ingawa katiba haimruhusu, pia juzi juzi tu wakati wa uchaguzi mkuu alisema nyota ya mkwere ina ng'aa sana na yeyote atakae simama kumpinga atakufa, pia ikulu wakasema kauli ya sheikh yahaya iheshimiwe, nashindwa kuelewa haya mahusiano kati ya gwiji huyu wa utabiri wa nyota na viongozi mafisadi wa chama tawala. Kwa upande wangu mi namuona huyu mzee ni mnafiki sana na pia sidhani kama anania nzuri na nchi yetu.nayeye ni fisadi, kwa wanao mjua vizuri mtaalam huyu naombeni mnijuze zaidi kwani namuona ni mtata sana na haelewiki.