IshaLubuva
JF-Expert Member
- Dec 4, 2008
- 250
- 11
Katika kuitikia wito wa serikali wa kupambana na uharibifu wa mazingira niliamua kuachana na matumizi ya jiko la mkaa na kununua jiko la gesi. Aidha niliamini kuwa gesi itkuwa na gharama nafuu zaidi (wenyewe wauzaji waliniambia kuwa gharama inakuwa kubwa wakati wa kuanza kwa sababu utalazimika kulipia gharama za mtungi) kuliko mkaa. Lakini hali haikuwa kama nilivyotarajia. Gesi ya Mtungi wa kilo 30 ambao hapa Dodoma unagharimu sh. 28,000.00 haikuweza kuhimili matumizi kwa mwezi mzima kwa familia ya watu watatu pekee. Nilinunua gesi tarehe 11/08/2009 na ilipofika tarehe 08/09/2009 mtungi ulikuwa chwee kabisa. Hali hii imenifanya nirudi kwenye matumizi ya mkaa kwani gunia la mkaa ni sh. 10,000.00 ambapo kwa gharama ya mtungi wa kilo 30 naweza kulumbana na muuzaji wa mkaa na kupata gunia tatu ambazo zinaniwezesha kukata zaidi ya miezi miwili.
1) Ninachojiuliza ni iwapo hii mitungi ya gesi kweli huwa inajazwa kama inavyostahili. Jana niliona tangazo la EWURA wakitoa unyo la udanganyifu kwenye biashara ya gesi ya kupikia
2) Je mimi kama mteja ninayenunua mtungi nitajuwaje kama mtungi ninaonunua umejaa inavyostahili?
3) Kwa hali hii itawezekana kweli wananchi kuachana na matumizi ya mkaa ili kuepusha ukataji wa miti kwa ajili ya kuchoma mkaa na hivyo kupunguza uharibifu wa mazingira?
4) Serikali iko wapi katika hili, wenzetu Ulaya gesi ni bidhaa ya umma na inapewa ruzuku (kumbukeni mzozo kati ya Urusi na Nchi za Ulaya baada ya gesi ya UUrusi kusimama wakati fulani kupelekwa kwao walivyokuwa wanahaha)
1) Ninachojiuliza ni iwapo hii mitungi ya gesi kweli huwa inajazwa kama inavyostahili. Jana niliona tangazo la EWURA wakitoa unyo la udanganyifu kwenye biashara ya gesi ya kupikia
2) Je mimi kama mteja ninayenunua mtungi nitajuwaje kama mtungi ninaonunua umejaa inavyostahili?
3) Kwa hali hii itawezekana kweli wananchi kuachana na matumizi ya mkaa ili kuepusha ukataji wa miti kwa ajili ya kuchoma mkaa na hivyo kupunguza uharibifu wa mazingira?
4) Serikali iko wapi katika hili, wenzetu Ulaya gesi ni bidhaa ya umma na inapewa ruzuku (kumbukeni mzozo kati ya Urusi na Nchi za Ulaya baada ya gesi ya UUrusi kusimama wakati fulani kupelekwa kwao walivyokuwa wanahaha)