Kuna tofauti gani kati ya binaadamu na mtu (watu)?

hargeisa

JF-Expert Member
Jun 19, 2011
549
41
Greetthinkers!!!!!!!!!!
katika pitapita zangu nilikuta mjadala huu wa binadamu na watu ni tofauti;
kuwa binadamu ni wote wenye ngozi nyeupe na watu ni wote wenye ngozi nyeusi
kuwa watu walikuwepo kabla ya binaadamu rejea mtu wakwanza alipatikana Tanzania Oldvai george
hapa naimani mjadala ulee !!!!! utapata ufumbuzi kwa kiwango fulaani!!!!!!!!!!!!!!!
 
Hii ndo naipata leo lakini nipo tayari kujifunza
watoto waadamu mmoja baada kumuua mwenzake aliienda nchi ya miitu na kuuoa alioa nanai hi inaaana kuwa kulikuwa na viumbe wengini kama yye
 
Binaadamu ni viumbe vyote vilioko ulimwenguni ambavyo vinasifa za kiutu.(sifa alizonano mtu)

Mtu Au watu ni binaadamu amae au ambao wako katika eneo maalum katika dunia.

1)Mfano: binaadamu akitaka lake hazuiliki au haambiliki. (hapa hakuna mpaka binaadamu yupi ni wote)

2)mfano: watu wa Tanzania ni wakarimu mno.(hapa imewabagua binaadamu sio wote ni wakarimu bali ni wa eneo maalum,Tanzania tu).

Ahsante
By Albimany.
 
bin adam - an arabic word means "son of adam" Mtu - is a typical swahili word to mean the same. hii ni nomino.
binaadamu/ ubinaadamu, mtu/ utu pia hutumika kama sifa nzuri. hana utu/ubinaadamu. kumaanisha sifa halisi ya kiumbe mtu/ mwanaadamu ambayo ni ukarimu, upole, huruma na nyingi nyenginezo zinazomtofautisha kiumbe huyo na viumbe wengine kama majini, wanyama nk.
best wishez
 
Nikijazia swali, Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu na Watu-Afrucan Charter on Human and People's Rights
 
Bin Adam ni kiarabu kumaanisha yeyote atokanaye na Adam.
Mtu ni kibantu kumaanisha yeyote atokanaye na kundi hili la wabantu. Hivyo, kama tutazama kwa umakini zaidi, siyo kila binadamu ni mtu au mtu ni binadamu. Watu wanaweza kuwa waafrika wa kundi la wabantu na binadamu wanaweza kuwa waarabu. Kawaida maneno haya hutumika interchangeably. Hivyo, kwa msingi huu, huleta maana sawa. Hii ni sawa na neno ustaarabu. Ustaarabu ni kuchukua mila na desturi za kiarabu. Lawafaa waarabu lakini si waswahili. Nadhani siku zijazo tutakuwa na utaafrika.
 
bin adam - an arabic word means "son of adam" Mtu - is a typical swahili word to mean the same. hii ni nomino.
binaadamu/ ubinaadamu, mtu/ utu pia hutumika kama sifa nzuri. hana utu/ubinaadamu. kumaanisha sifa halisi ya kiumbe mtu/ mwanaadamu ambayo ni ukarimu, upole, huruma na nyingi nyenginezo zinazomtofautisha kiumbe huyo na viumbe wengine kama majini, wanyama nk.
best wishez

Bin Adam ni kiarabu kumaanisha yeyote atokanaye na Adam.
Mtu ni kibantu kumaanisha yeyote atokanaye na kundi hili la wabantu. Hivyo, kama tutazama kwa umakini zaidi, siyo kila binadamu ni mtu au mtu ni binadamu. Watu wanaweza kuwa waafrika wa kundi la wabantu na binadamu wanaweza kuwa waarabu. Kawaida maneno haya hutumika interchangeably. Hivyo, kwa msingi huu, huleta maana sawa. Hii ni sawa na neno ustaarabu. Ustaarabu ni kuchukua mila na desturi za kiarabu. Lawafaa waarabu lakini si waswahili. Nadhani siku zijazo tutakuwa na utaafrika.
Wote wawili mmeanza vizuri ila mmekuja kuharibu baadae...
Ni kweli neno Bin Adam, linatokana na neno la Kiarab Ibnu Adam (kiume) kwa Kihibrania ni Ben Adam, kama mwanamke basi ni bint Adam, ikimaanisha mtoto wa Adam.

Hii ikimaanisha kuwa sisi sote ni watoto wa Adam...!

Neno Mtu, linatoka kwenye lugha za Kibantu "Ntu", likimaanisha kiumbe mwenye kujitambua na mwenye uwezo wa kuongea (human being). Ninaposema lugha za Kibantu nina maanisha ni zile lugha zote zinazo zungumzwa kuanzia ukanda wa Afrika toka kusini mpaka kule Kameruni. (Bantu languages) Lugha hizi zimejengwa na zaidi ya makabila 600.

Waarabu walipokuja Afrika Mashariki na ya kati, walikuwa wakitumia ili neno Bin Adam kuonyesha ustaarabu kuwa wote tumetokana kwa asili ya baba mmoja (Adam). Wangeweza kutumia neno An-Nāsi likimaanisha pia watu (Mankind). Lakini hata hivyo kwa muingiliano wa Lugha za wenyewe (Kibantu) na Lugha za wageni, wakiwemo hao Waarabu, neno Ntu, alikuwachwa nyuma, liliendelea kutumia, na kila lilipotumia lilijikuta linabadirika kimatamshi na kuja kuandikwa Mtu, badala ya Ntu.

Kama lilivyokuja baadae kubadilika neno Bin Adam, ambalo linabeba maneno mawili, "Bin" na "Adam", na kuunganishwa na kuwa Binadam.

Hitimisho ni kwamba, neno Watu na neno Binadam, yote yana maana moja tu... Tofauti itakuja tu pale mtu atapotaka kuleta maana zake binafsi.
 
Adam alikuwa mtu, yeye hakuwa binadamu. Hapo mwanzo mungu aliumba watu, ambao ni Adam na Hawa. Hawa sio binadamu. Ni watu, watu hawa wakazaa watoto sasa ambao ni binadamu mpaka sasa. Tunajiita watu kwa sababu tu. Tunatokana na mtu ambaye na Adam.
 
Greetthinkers!!!!!!!!!!
katika pitapita zangu nilikuta mjadala huu wa binadamu na watu ni tofauti;
kuwa binadamu ni wote wenye ngozi nyeupe na watu ni wote wenye ngozi nyeusi
kuwa watu walikuwepo kabla ya binaadamu rejea mtu wakwanza alipatikana Tanzania Oldvai george
hapa naimani mjadala ulee !!!!! utapata ufumbuzi kwa kiwango fulaani!!!!!!!!!!!!!!!

Maneno yote mawili yana maana moja. Binadamu ni neno Rasmi, Na Mtu ni neno ambalo sio rasmi. Kama Stomach na Belly kwenye kingereza.
 
..kwa muingiliano wa Lugha za wenyewe (Kibantu) na Lugha za wageni, wakiwemo hao Waarabu, neno Ntu, alikuwachwa nyuma, liliendelea kutumia, na kila lilipotumia lilijikuta linabadirika kimatamshi na kuja kuandikwa Mtu, badala ya Ntu.
Mzee, kwa jumla umeeleza vema ila tu nadharia yako ya mabadiliko ya n-tu kuwa m-tu ni yako binafsi kidogo...

lakini haidhuru kwa swali lililoulizwa.
 
Greetthinkers!!!!!!!!!!
katika pitapita zangu nilikuta mjadala huu wa binadamu na watu ni tofauti;
kuwa binadamu ni wote wenye ngozi nyeupe na watu ni wote wenye ngozi nyeusi
kuwa watu walikuwepo kabla ya binaadamu rejea mtu wakwanza alipatikana Tanzania Oldvai george
hapa naimani mjadala ulee !!!!! utapata ufumbuzi kwa kiwango fulaani!!!!!!!!!!!!!!!
wa2 ni weeeengi kwel ila binaadamu wachache haswa.
 
Mtu ni b'dam mkamilifu yaani mwenye akili timam na uwezo wa kutambua mazuri na mabaya mbele ya jamii.
B'adam ni yule ambae hana hayo alokua nayo mtu. So mtt ni b'adam lkn bado hajawa mtu kamili na mwendawazimu atoshindwa kujitambua nae pia hawezi kuwekwa kwenye kundi la watu.
 
Wote wawili mmeanza vizuri ila mmekuja kuharibu baadae...
Ni kweli neno Bin Adam, linatokana na neno la Kiarab Ibnu Adam (kiume) kwa Kihibrania ni Ben Adam, kama mwanamke basi ni bint Adam, ikimaanisha mtoto wa Adam.

Hii ikimaanisha kuwa sisi sote ni watoto wa Adam...!

Neno Mtu, linatoka kwenye lugha za Kibantu "Ntu", likimaanisha kiumbe mwenye kujitambua na mwenye uwezo wa kuongea (human being). Ninaposema lugha za Kibantu nina maanisha ni zile lugha zote zinazo zungumzwa kuanzia ukanda wa Afrika toka kusini mpaka kule Kameruni. (Bantu languages) Lugha hizi zimejengwa na zaidi ya makabila 600.

Waarabu walipokuja Afrika Mashariki na ya kati, walikuwa wakitumia ili neno Bin Adam kuonyesha ustaarabu kuwa wote tumetokana kwa asili ya baba mmoja (Adam). Wangeweza kutumia neno An-N&[HASHTAG]#257[/HASHTAG];si likimaanisha pia watu (Mankind). Lakini hata hivyo kwa muingiliano wa Lugha za wenyewe (Kibantu) na Lugha za wageni, wakiwemo hao Waarabu, neno Ntu, alikuwachwa nyuma, liliendelea kutumia, na kila lilipotumia lilijikuta linabadirika kimatamshi na kuja kuandikwa Mtu, badala ya Ntu.

Kama lilivyokuja baadae kubadilika neno Bin Adam, ambalo linabeba maneno mawili, "Bin" na "Adam", na kuunganishwa na kuwa Binadam.

Hitimisho ni kwamba, neno Watu na neno Binadam, yote yana maana moja tu... Tofauti itakuja tu pale mtu atapotaka kuleta maana zake binafsi.

umeanza vizuri lakini umehitimisha vibaya. Yaani wewe umeonesha utofauti, halafu unasema "Tofauti itakuja tu pale mtu atapotaka kuleta maana zake binafsi", huku ukisema "Ntu", likimaanisha kiumbe mwenye kujitambua na mwenye uwezo wa kuongea, halafu eti neno Bin Adam huonyesha ustaarabu kuwa wote tumetokana kwa asili ya baba mmoja (Adam).

Afadhali ungesema kuwa neno "watu" asili yake ni wabantu na neno "binadamu" asili yake ni waarabu ungeeleweka zaidi kuwa hiyo ndo tofauti katika asili lakini maana ni moja. Hata hivyo umejitahidi kwa ufafanuzi mzuri
 
Back
Top Bottom