Patriote
JF-Expert Member
- Jul 13, 2011
- 1,718
- 1,047
Taarifa ya CAG inaonyesha deni la taifa limekua hadi kufikia Sh14.4 trilioni sasa tunajiuliza hivi inaingia akilini kweli? Tunashindwa kujitegemea katika bajeti hapo hapo tunatoa misamaha ya ajabu, hivi hii nchi kweli itakwenda? Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma wiki hii, CAG alisema deni la taifa limeongezeka kutoka sh10.5 trilioni mwaka wa fedha wa 2009/2010 hadi kufikia sh14.4 trilioni mwaka 2010/2011 sawa na ongezeko la asilimia 38.
Kuna ongezeko kubwa la deni la taifa lakini hoja hapa si kuongezeka kwa deni la taifa bali ni kwamba deni hili limeletwa kwa mikopo yenye manufaa kwa taifa na yenye kukuza uchumi wa nchi? Hii ndio hoja ya msingi ya kuangalia, alisema. Mara baada ya kutolewa kwa ripoti hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali Kuu(PAC), John Cheyo alionyesha kushangazwa na kuendelea kukua kwa deni la Taifa wakati miradi mingi nchini haina fedha. Deni la taifa linatupa matatizo sisi wote hapa kwa sababu mimi sielewi maana tunakopa lakini miradi yetu haina pesa hapa kuna kitendawili,alisema Cheyo na kusema Bunge itabidi lijadili na kutegua kitendawili hicho.
Maoni yangu
Suala la kukua kwa deni la Taifa si geni masikioni mwa watanzania. Deni hili limekuwa likikua hata bila ya mabadiliko yoyote yanayoonekana hadi imefikia hatua masikio yetu yamekuwa sugu kusikiliza wimbo wa kukua kwa deni la Taifa. Kuna uwezekano mkubwa sana usugu huu wa masikio yetu kusikia kichefuchefu hiki, unawapa fursa mafisadi kuingiza madeni hewa kwenye deni la serikali na hivyo kufanya deni kuongezeka, inawezekana tunaingiza figures hewa kwenye hilo deni au fedha tunazokopo zinafika nchini na zinaliwa na wezi wachache na hivyo hazifikii walengwa. Tunaambiwa kwa mwaka wa fedha 2009/10-2011/12 asilimia 38% ya deni hilo imeongezeka.
Ukiangalia miaka ambayo huduma zimezorota sana hapa nchini kwa viwango vyote ni mwaka 2009-2012 sasa kama kuna pesa mingi hivyo tulikopa zipo wapi Mungu wangu????zimetumika kwenye miradi gani ya kumkomboa mwananchi???Zilikopwa kwa kazi gani???zimetumika kwa shughuli gani???Mbona kila siku ni afadhali ya jana???Hapa tunahitaji microscopic eyes kubaini mauoza mana kama mpaka CAG na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuu wanashangaa, itakuwaje sisi tusiofika huko jikoni????Mimi nadhani CAG/Cheyo wasiishie tu kwenye kushangaa. Wadig down kujua kuna nini, Bora iundwe tume maalum kuchimbua undani wa madeni yetu na ikiwezekana reputable Auditing firms wapewe kazi ya kulichokonoa hilo deni mana nadhani hili deni ni commulative toka enzi ile ambayo BOT ilikuwa chini ya Majizi kama Balali na washirika wake wa Serikalini. Kama waliweza EPA, si ajabu kuwa walianzia kwenye madeni mengine na kuishia EPA. MwanaJF changia nini kifanyike katika hili??
Kuna ongezeko kubwa la deni la taifa lakini hoja hapa si kuongezeka kwa deni la taifa bali ni kwamba deni hili limeletwa kwa mikopo yenye manufaa kwa taifa na yenye kukuza uchumi wa nchi? Hii ndio hoja ya msingi ya kuangalia, alisema. Mara baada ya kutolewa kwa ripoti hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali Kuu(PAC), John Cheyo alionyesha kushangazwa na kuendelea kukua kwa deni la Taifa wakati miradi mingi nchini haina fedha. Deni la taifa linatupa matatizo sisi wote hapa kwa sababu mimi sielewi maana tunakopa lakini miradi yetu haina pesa hapa kuna kitendawili,alisema Cheyo na kusema Bunge itabidi lijadili na kutegua kitendawili hicho.
Maoni yangu
Suala la kukua kwa deni la Taifa si geni masikioni mwa watanzania. Deni hili limekuwa likikua hata bila ya mabadiliko yoyote yanayoonekana hadi imefikia hatua masikio yetu yamekuwa sugu kusikiliza wimbo wa kukua kwa deni la Taifa. Kuna uwezekano mkubwa sana usugu huu wa masikio yetu kusikia kichefuchefu hiki, unawapa fursa mafisadi kuingiza madeni hewa kwenye deni la serikali na hivyo kufanya deni kuongezeka, inawezekana tunaingiza figures hewa kwenye hilo deni au fedha tunazokopo zinafika nchini na zinaliwa na wezi wachache na hivyo hazifikii walengwa. Tunaambiwa kwa mwaka wa fedha 2009/10-2011/12 asilimia 38% ya deni hilo imeongezeka.
Ukiangalia miaka ambayo huduma zimezorota sana hapa nchini kwa viwango vyote ni mwaka 2009-2012 sasa kama kuna pesa mingi hivyo tulikopa zipo wapi Mungu wangu????zimetumika kwenye miradi gani ya kumkomboa mwananchi???Zilikopwa kwa kazi gani???zimetumika kwa shughuli gani???Mbona kila siku ni afadhali ya jana???Hapa tunahitaji microscopic eyes kubaini mauoza mana kama mpaka CAG na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuu wanashangaa, itakuwaje sisi tusiofika huko jikoni????Mimi nadhani CAG/Cheyo wasiishie tu kwenye kushangaa. Wadig down kujua kuna nini, Bora iundwe tume maalum kuchimbua undani wa madeni yetu na ikiwezekana reputable Auditing firms wapewe kazi ya kulichokonoa hilo deni mana nadhani hili deni ni commulative toka enzi ile ambayo BOT ilikuwa chini ya Majizi kama Balali na washirika wake wa Serikalini. Kama waliweza EPA, si ajabu kuwa walianzia kwenye madeni mengine na kuishia EPA. MwanaJF changia nini kifanyike katika hili??