Kuna Mchezo Unachezwa!

MMM nj wazi mchezo unaozungumzia ni muswada wa katiba mpya na mchakato mzima unaoendelea sasa. Bila chenga ni dhahiri kuna mchezo mchafu unachezwa ili kwa wao ni kama kuikomoa CDM lakini kumbe ni kinyume chake. Lakini ni matumaini yangu kuwa mchezo huo mwamuzi ni mwananchi.

Wacha waringe kama wao walijipeleka wenyewe bungeni, lakini kwa kadri mambo yanavyosonga ipo siku kitaeleweka tu.
 
Kuna mchezo unachezwa na wapo wanaopenda kucheza mchezo huo. Mchezo unaochezwa na wenye kucheza hucheza. Mchezo huo huchezwa na wale wenye kuupenda mchezo huo. Ukikaa pembeni wanakushangaa kwanini hutaki kucheza na ukiingia kucheza utakavyo watakuuliza 'mbona huchezi kama sisi'? Ukiwaambia mchezo wenu haufuati kanuni wala mlio wa muziki watakuambia haijalishi wewe cheza tu alimradi uonekane unacheza. kuna mchezo unachezwa na wapo wanaopenda kucheza mchezo huo. Ukialikwa kucheza utacheza au utabakia kutazama? Au utajaribu kutaka mchezo ubadilishwe ili wengi waufurahie kwa kufuata kanuni, na mirindimo yenye kuendana na uzuri wa mchezo wenyewe?

Ndugu zangu, kuna mchezo unachezwa, na wapo wenye kupenda kucheza mchezo huo!
[/B

MMM


siasa au?
 
MMM naomba nikutafutie chance kwa Mrisho Mpoto uwe kwenye bendi yake..maana naona una kipaji cha mashahiri sana....
 
Well inaonekana wengine hata mlikuwa hamjui kuna mchezo unachezwa.. well lets see tutaona muziki utakapoisha na kukuta watu wanaendelea kucheza... kumbe walikuwa viziwi!
Unajuwa baada ya watu makini wenye akili zao kukataa kuucheza mchezo huu spika wa Bunge leo alisitisha mjadala ili wabunge wakasome vizuri muswada maana inaonekana wabunge wa magamba wote hakuna mwenye jipya wanaongea kama tape recorder, yaani wote wanaongea kitu cha aina moja.

Sasa swali linakuja hivi kama wabunge wenyewe wa CCM spika amewaona kwamba hawajausoma ule muswada badala yake wamekariri kama kasuku neno CHADEMA na Tundu Lisu hivi hawa kuna hata akili ndogo iliyosalia vichwani mwao?
 
Nyinyi nanyi mbna mnakuwa na upeo kama wa KOMBA, kama sio wa LUSINDE.... Mchezo wenyewe ni ule wa magamba wanaoucheza mjengoni juu ya muswada wa katiba mpya
 
MMM natumai fumbo hili utalifumbua kabla usiku haujawa mwingi,sitapata usingizi mpaka umwage maelezo yakinifu mkuu!naamini kuna somo hapa kama ilivyo kawaida yako,am waiting
 
Nasikia muziki toka mbali kanda ya kati, pia naona watu wanacheza bila kufuata mirindimo na midundo ya muziki, yani ni vurugu ukiingia na ukijifanya unajua lazima utahanyagwa tu, kuna watu pia kila ukianza muziki wanatoka nje, bora wasikie sauti kuliko kushriki kuharibu ladha ya muziki kwa kukanyagana.

Well inaonekana wengine hata mlikuwa hamjui kuna mchezo unachezwa.. well lets see tutaona muziki utakapoisha na kukuta watu wanaendelea kucheza... kumbe walikuwa viziwi!
 
Well inaonekana wengine hata mlikuwa hamjui kuna mchezo unachezwa.. well lets see tutaona muziki utakapoisha na kukuta watu wanaendelea kucheza... kumbe walikuwa viziwi!

...kama ni huo mchezo basi na-wachezeane wenyewe huko huko ndani kwao,sisi huku michezo ya kijinga huwa hatuitaki na tunawatahadhalisha na kuwaonya ya-kwamba "1.muda wa huo mchezo wao mchafu umekwisha,2. huku kwetu hakuna kiwanja cha huo mchezo wao dhalimu", na wawe makini kwani tunaona wanataka kutuchezea na kwakua sisi si watu wakuchezewa tena,"sasa watachezea kichapo muda si mrefu,kwani sisi ujinga tanautaka?!" ...Eboo...
 
Kuna mchezo unatakwa kuchezwa lakini bado haujachezwa na mchakato uliopo ni kuandaa namna ya kutengeneza kanuni za kuucheza mchezo huo. Walio wengi hawafurahishwi na jinsi kanuni zinavyoandaliwa kwani zinampa sana nguvu timu mojawapo shindani katika kutengeneza kanuni za kucheza huo mchezo.

Mfano, kwa hali ilivyo sasa, timu shindani inayovaa sare za kijani ndiyo inayotoa referee, kamisaa, vibendera, walinzi wa uwanjani, kukatisha tiketi, kugawa mapato ya mchezo, kutangaza matokeo ya mchezo, n.k

Lakini walio wengi wanaona kanuni ya namna hiyo haitaleta usawa, kila mechi ikichezwa matokeo ni rahisi kutabirika. Kimsingi, timu ya kijani itakuwa ikishinda wakati wote mara ikutanapo timu zingine katika mechi. Watazamaji hawapendi maana kanuni ya namna hiyo inaharibu raha ya mchezo....
 
Nakubaliana nawe MM,
Kuna mchezo unachezwa!

Wameendelea kuucheza, tena katika uwanja mpya wa gharama kubwa.

Afrika mashariki hakuna nchi yenye uwanja kama ule. Uwanja una kila aina ya ufahari, wachezaji wanaweza kuamua kulala uwanjani bila kuulizwa. Wakiamka wanashangilia bila kujali kuwa timu yao ndo imefungwa goli. Kwa hakika inasikitisha, lakini bado wako uwanjani wanaendelea kucheza.

Nimeangalia na kuwaona walio wengi wanacheza bila kujua kanuni, wanaamini mwalimu wao anajua na kwao hilo latosha. Ni wabishi, hudiriki hata kubishana na picha. Wamesahau kuwa watizamaji walio wengi wanajua kanuni na wanaweza kuucheza mchezo vizuri kuliko wao. Hawaamini, waendelea kucheza.

Nasikia watakutana na mkuu wao siku chache zijazo. Huenda akawakumbusha kanuni na mbinu za mchezo, japo nina uhakika hawatashika. Wana vichwa vigumu au ni wajuaji. Wamekaa na mwalimu wao mara nyingi, huwa hawamuelewi. Hata wakijitokeza walimu wa kimataifa hawaelewi zaidi ya kuwabeza. Wanaendelea kucheza mchezo wasioujua, ni hatari kwao. Watazamaji wamewachoka, wameanza kususia mchezo wao. Hawaamini, wanaomba 'wananchi tusikilizeni sisi'. Sina hakika kama watawasikia, kanuni hawazijui na wanacheza mchezo vibaya, hauvutii.

Kuna mchezo unachezwa, wanaendelea kucheza, kwamba watamaliza salama ni jambo la kufuatilia kwa makini.
 
Fine mimi nimekupata, kuwa unaongelea issu ya Jairo na yale yanayoendele kwenye kikao cha jk na wabinge wa magamba ili wawe kitu kimoja kuiokoa serikali ya magamba. Nikweli kuna mchezo unataka kuchezwa ambao utaduaza wengi.

Well inaonekana wengine hata mlikuwa hamjui kuna mchezo unachezwa.. well lets see tutaona muziki utakapoisha na kukuta watu wanaendelea kucheza... kumbe walikuwa viziwi!
 
Au mjadala wa mswada wa katiba?

mbona umeuliza jibu? Mchezo unachezwa kwa staili ya makengeza, kila anayeuliza wao washangazwa. wanahisi wakwazwa, kwa mambo yaso kukwaza, katu asilani sioni kipi cha kukwaza. pasi akili waja na hoja za kukwaza, mawazo washangaza kwa akili zisowaza. ngoja muda ufike tutavyo wagalagaza, haya majitu yakwaza, mawazo kama ya chaza.
 
Ukitaka mji mimi nitakuchagulia Dodoma bila shaka huo mchezo source yake itakuwa ni pale mjengoni
 
MBAYA ZAIDI MCHEZO HUO MWISHO UNACHEZWA BILA REFA, RULES, WALA POINT NI KUKABA TUU...Ila tutaenda na beats ivo ivo


Kuna mchezo unachezwa na wapo wanaopenda kucheza mchezo huo. Mchezo unaochezwa na wenye kucheza hucheza. Mchezo huo huchezwa na wale wenye kuupenda mchezo huo. Ukikaa pembeni wanakushangaa kwanini hutaki kucheza na ukiingia kucheza utakavyo watakuuliza 'mbona huchezi kama sisi'? Ukiwaambia mchezo wenu haufuati kanuni wala mlio wa muziki watakuambia haijalishi wewe cheza tu alimradi uonekane unacheza. kuna mchezo unachezwa na wapo wanaopenda kucheza mchezo huo. Ukialikwa kucheza utacheza au utabakia kutazama? Au utajaribu kutaka mchezo ubadilishwe ili wengi waufurahie kwa kufuata kanuni, na mirindimo yenye kuendana na uzuri wa mchezo wenyewe?

Ndugu zangu, kuna mchezo unachezwa, na wapo wenye kupenda kucheza mchezo huo!



MMM
 
Mchezo unachezwa watu wataubuka taa ikiwashwa kuna mchezo tena mchafu. Kaz kwako MMM Kuwasha taa watu waubuke!
 
Back
Top Bottom