nderingosha
JF-Expert Member
- Mar 20, 2011
- 4,281
- 3,243
..Wakati vyama vya upinzani(haswa CDM)wakipambana kuleta mabadiliko ya kifikra kwa watanzania kujua haki zao za msingi dhidi ya watawala wao...wao chama tawala CCM wanaonekana kwa kasi hiyo hiyo kuzuia vuguvugu hili la mabadiliko kwa watanzania....Badala ya kujikita kwenye kutatua matatizo ya msingi kwa watanzania..tunaona CCM wakitumia nguvu nyingi kwa gharama yoyote kwenye hila...fitna ..hujuma...kejeli...matusi.. etc etc kwenye chaguzi ndogo...mikutano ya kulazimisha kimagumashi...na hata tetesi za kushiriki kuwaua/kuwapiga wapinzani (CDM)....
Way forward (nini kifanyike):
Way forward (nini kifanyike):
- Wapinzani(CDM) kutumia gharama yoyote kuzunguka nchi nzima kutoa elimu ya uraia kwa watanzania haswa wa vijijini ili waweze kujua haki yao ya msingi ya kujiletea mabadiliko kwa njia ya sanduku la kura ifikapo 2015....na haswa kuwafanya wajue kuwa haki haipatikani kwa kupewa chakula,nguo na fedha..Pia kuwafanya watanzania hawa wajue umuhimu wa kulinda kura zao hapo 2015 kwa gharama yoyote kwa manufaa ya mabadiliko ya maisha yao(kama walivyofanya arumeru) ..Pia kuwafanya watanzania hawa wajiandikishe kwa wiingi kwenye daftari la wapiga kura ili wapate fursa ya kupiga kura kwa ajili ya mabadiliko ya maisha yao....
- Ni kwa kufanya hivi tu wapinzani wataweza kupambana na hata kuwashinda watawala kwenye sanduku la kura....Kinyume na hapo nadiriki kutabiri kuwa come 2015...kuna hatari kubwa sana kwa CCM kufanya hujuma/kupora uchaguzi/matokeo kwa gharama yoyote....Hii ni kutokana na trend ya matendo ya CCM tokea vuguvugu la mabadilko lianzishwe na CDM...Kitakachofuata baada ya CCM kupora matokeo sijui...lakini sote twajua yaliyotokea kenya.......Nasisitiza...CDM piteni vijijini kuanzia sasa...haswa mikoa ya uswahilini....Pwani..Morogoro..Tabora...Dodoma etc etc...kama mnavyofanya Mtwara na Lindi...