<br />Derimto i,aonyesha ni jinsi gani ulivyo kipofu au mlevi wa kufikiri hakuna taarifa isiyokuwa na source,ikiwa hivyo basi ni ya kutunga.Hatuwezi kuwa vampire kwa kudaka kila kinachorushwa.Wote tukiwa na akili kama zako hatutarajii kutoa njia ya kutatua kwani hakuna haki isiyo na sheria.Tambua no evidence no right to speak katika ''court''.<br />
<br />
Hatuna njia nyingine ya kuwahukumu hawa zaidi ya sheria,hivyo tukiwa wanajanvi kila mtu anafani yake.Tambua hatuko kusoma tu hapa na kupata cha kuchagiza kwenye vijiwe vya kahawa ''hapana'',wengine tunayafanyia kazi yanayojitokeza kulingana na uzito wake.<br />
<br />
Nakushauri jaribu kubadilika na kuwamtekelezaji zaidi ya msomaji tu kwani uzalendo wako haujengwi hivyo ila ni ishara ya grapevines.Huwezi kuongelea habari ambayo inahitaji maamuzi huku huna taarifa za kutosha,lazima tu itaishia kapuni ama mtaani tu kama ''vapour gossip''.Pia tujenge mazingira ya kuisaidia jamii kwa kwenda mbali zaidi(huu ndio uzalendo) si tu kuishia kusoma na kulalama hapa.<br />
<br />
Otherwise sipingi ''tetesi''ila nachukia tetesi zinazokuja na kuishia hewani bila mtoa hoja kutuambia kwa nini zimepotea kama ilivyotokea kwa ''Shimbo''.Jamani trillion tatu ni fedha nyingi,haiwezekani habari yake kupotea kienyeji hivi hivi tu.Je!tukisema hawa waleta tetesi huwa wanaongwa kuzipotezesha bila shaka hizi nazo zitakuwa ''tetesi'' kutokana na kutokuwa na ushahidi.Tuwe makini si vyote ving'aavyo ni dhahabu.
<br />
Nadhani bado unashindwa kutofautisha habari kamili na chanzo chake, tetesi na mahakama na humu ndani tunapeana taarifa haijalishi kuwa ni tetesi au ukweli na katika hizo tetsi kwa nini asemwe Shimbo yeye ni nani? Kwa nini wasisemwe wengine? Wenye madaraka na biashara kubwa wasitajwe atajwe yeye ni nani? Jamani hebu turuhusu akili zetu zifanye kazi na tuache kuwa wajuaji kupitiliza kiasi ambacho TUNAWEZA KUWAKATISHA TAMAA WALE WANALETA TAARIFA ZA MAOVU YANAYOENDELEA KWENYE NCHI HII hata huko kwenye vijiwe vya kahawa kuna taarifa za maana tu na siyo lazima taarifa za ufisadi ziletwe kwa press conference ndipo tuamini? huu ni utumwa wa mazoea ya kudesa kama marobot hatuajiachii akili zetu kufanya kazi kuna uozo wa hali ya juu sana kwenye nchi hii na huku watu wote tunafanya vipofu tunasubiri hotuba ya mwisho wa mwezi na tbc1 ndio watakatifu wanaosema ukweli wakati wote maana habari zao zimeshathibitishwa na mafisadi na kutufanya mandondocha kwenye nchi yetu na tukisema tunaambiwa ni msimamo wa kisiasa ndiyo unatufanya teseme hivyo na hatuna source!!!?