Kuna harufu ya kujuana kwenye balozi zetu

Michese huko kwenu Mtu na watoto wake wanakuwa wabunge, ha! Ha! Angalau CCM hamna baba na watoto ubalozini! Au BOT! Ha! Ha! - Le Baharia

William, kwa siku z ahivi karibuni umekuwa ukiandika sana tena vitu vingine vya kustua. Kwa heshima ya mkeo na familia yako, ingekuwa bora zaidi ungenyamaza kwa maana watu wanavyokuandama humu ndani sijui wanajisikiaje hasa unapoitwa mjinga na kila mchangiaji. Mzee hachana na hii milumbano isiyo na tija. Heshima kaka yangu. mimi nakufahamu longi sana kumbuk aenzi zetu YMCA. Msalimie wifi kakangu
 
Hii CHADEMAMANIA msipoangalia itawaua!!! Yaani kila mtu anayeleta hoja kinzania kwa serikali ni CHADEMA!!!!!! Very shameful!!!! Basi na wale wazee wa Kigoda cha Mwalimu lazima watakuwa CHADEMA!!! Mpaka mwaka 2015 ufike hii CHADEMAMANIA itakuwa ishawaua baadhi yenu kwa kiharusi.
Hakuna mtoto wa Mkapa Ubalozi wetu wowote Duniani Mkapa ana watoto Wawili Steve na Nico wapo Bongo, na hawapo Ubalozi wowote hapo Bongo Umekurupuka, nenda Bungeni uone Viongozi wa Chadema na ndugu zao wote ni Wabunge, Halafu uje utueleze hivi Chadema ilibidi Mwenyekiti lazima awe Mkwe wa Mtei tu? Hakukuwa na wengine? Wacheni kuchafua Majina ya watu. - William
 
Wanajamii!!
Shinikizeni Wizara ya Mambo ya nje iwapatie orodha ya wafanyakazi wote waliopo ktk balozi zetu pamoja na Curriculum Vitae zao na hapo ndipo mtakapokoma kulinga maana mtagundua uozo uliopo ktk balozi zetu pamoja na gharama za kuwatunza, Je mnafahamu kuwa wafanyakazi kwenye balozi zetu wenye hadhi ya diplomat huwa hawalipi UMEME,GAS,SIMU(landline) nje ya MSHAHARA AMBAO KWA HAPA ULAYA KTK BALOZI 5 AMBAZO NINA HABARI ZAKE WANACHUKUA WASTANI WA €3000 kwa mwezi bila kulipia kodi wala nini - Fortunately mimi si mlipakodi wa Tanzania lakini inauma ukilinganisha na maisha ya watanzania wa kawaida na hasa ukitilia maanani kuwa most of them hawana sifa zozote zaidi ya undugu wao na mafisadi.
 
WEWE unadhani kila anaeleta hoja ya kuibua jambo ambalo lina walakini kuhusu maamuzi ya serikali kiutendaji basi yumkini mtu huyo ni wa CHADEMA?shame on u!u can't think and analyze objectively?ur groundless attack on CHADEMA indicates how huwezi kujibu hoja kwa hoja.inaonekana ukiambiwa mtoto wa waziri fulani kakutwa na magendo ya nafaka na kutumia influence ya 'BABA' cha kwanza kufikiri na kujiuliza ili kuchangia hoja ni ''kwani ni mtoto gani wa waziri yeyote kivuli wa CHADEMA nae kakamatwa na magendo yeyote?''ndiyo maana hatuwataki watu waliolelewa na siasa za kulalamika badala ya kufikiri na kuchunguza tatizo halisi ni nini,moja.pili suluhu ni nini.



Duuuuh,Mkuu u are a great thinker!! Uovu wa mtu mmoja hauhalalishi Uovu wa Mwingine!!
Lakini sishangai kwa "Mali-Cela" kuchangia hivyo,Its pretty obvious,wht else wud he say?!!
 
Michese huko kwenu Mtu na watoto wake wanakuwa wabunge, ha! Ha! Angalau CCM hamna baba na watoto ubalozini! Au BOT! Ha! Ha! - Le Baharia

La mtu na mwanawe kuwa wote wanafanya kazi fulani, hili si tatizo. Wala hili si la Tanzania tu, kuna kila sababu ya mzazi akawa ni role model wa mwanae. Kuna kina George Bush, baba na mwana, kuna kina Gandhi, mama, mwana, mkwe. Kuna kina Karume, Baba na mwana. Kuna wacheza mpira duniani na hapa kwetu, kuna madaktari na watu wa kazi, biashara na fani mbalimbali ambao watoto zao wanafata nyayo.

Tatizo letu hapa Tanzania ni pale unapokiingiza kijiji kizima, idara fulani au kabila hilo ndio linakuwa dominant pale kwa kuwa tu Mkuu pale ni wa kabila hilo au unapowajaza waumini wa kanisa fulani kwa kuwa mkuu wa hapo ni muumini wa kanisa hilo.

Hili ndio tatizo. Lakini Ubunge, si inabidi uchaguliwe na wananchi? Unless uwe wa kupendelea (viti maalum). Ubunge wa kugombea kama watachaguwa baba na akafanya kazi nzuri na asibwagwe kama alivyobwagwa mzee Malecela Dodoma, kuna kila sababu ya atapokuja mwanae kugombea watu wakamchaguwa.

Tumeona mfano wa Malima. Lakini leo hii unafikiri kuna mtoto wa Malecela anaeweza kugombea akapata? ng'oo! Ikiwa baba mtu kapigwa chini utategemea nini kwa mwanawe? Lakini ingekuwa Malecela kaona kuwa sasa umri umefika na siwezi tena kuwatumikia wananchi kama nilivyokuwa kijana, na akaamuwa kuwachia ngazi yeye mwenyewe bila kuangushwa kisiasa,angeondoka pale na heshima kubwa sana na endapo angetokea mwanae kugombea ingekuwa hakuna mpinzani.
 
wana JF!
wale mliopo humu ndani ya FORUMS kabla yangu au hata waliokuja baadaye kidogo baada yangu watakuwa wamewahi kusikia hili jina(nick name) Field Marshall ES - huyo ni mke wa W.J.Malecela na nilikuwa nipo tempted kuweka full CV yake lakini roho yangu bado inakataa ila husband wake kama anataka tunaweza kufanya hivyo.

by the way William J. Malecela kwa nini na wewe husiwawekee wana jamii CV yako?? ahahahaha watu tuna hamu ya kucheka...
 
Field Marshall we kaa huko huko New York usifikili kuwakilimu wakina Nape wakija huko ndio leseni ya kupata ubunge wa Mtera; wagogo wamejanjaruka hakuna mtu wa jina kama lako atakuja kupata ubunge tena huko mkoa wa IDODOMYA, wazee wenu wameharibu miaka nenda rudi wagogo bado ombaomba tu!!

Field Marshall ni mke wake na tokea tuweke wazi kuwa yeye ni nani na anafanya nini basi hajawahi tia mguu tena humu JF hataki kujiharibia kitumbua ...
 
Mifano ni mingi na inakera
...Ndesamburo na binti yake na mkwe wake.
....Lema, Kiwia, Selasini, Kimaro etc hao ndio wenye nafasi CDM, wengine wanaonekana ni watoka mbali....ndo maana Zitto amekalia kuti kavu.
......Angalia madiwani wa CDM waliofukuzwa Arusha, 75% ni wa kabila lile lile.
NI UKABILA KWA KWENDA MBELE.

Hao Madiwani waliofukuzwa Arusha walijichagua wenyewe? Nonsense!!!!
 
People Mmechemka Mkapa or Malecela hawana watoto ubalozi wowote Duniani, Mmechemka na muwache majungu! - Le Mutuz!


I never could have imagined u could have this low level of reasoning,blv me i never thought!!
After all those years of attending "good schools" nevertheless this is all u have in Brain? Its really sad!!
HAUJIBU HOJA,HALAFU UNAKIMBILIA MANENO YA KISHAMBENGA "ETI ACHENI MAJUNGU"
Unabaki kuchekacheka tu,u must be hysterical,really u are taking after your father!!!
 
Ebu nendeni kule UK ubalozi unawatoto wa vigogo kutoka Ikulu, kunakijana anaitwa Alan Kuzilwa ni Afisa wa ngazi ya juu apa ubalozini kwetu. babayake alikua Afisa usalama kule Ikulu
 
Tatizo la undugunization halipo sehemu fulani tu Tanzania, ni tatizo sugu limeanza zamani, ukienda kwenye Wizara, Idara, Taasisi, Shirika hata NGO ambayo wakubwa ni wakabila fulani basi utafikiri kuwa Tanzania hakuna makabila mengine.

Hili ni tatizo sugu na lipo na siku hizi kuna trend mpya imeanza, toka yameanza haya makanisa ya kiajabu ajabu ya fungu la kumi, tunaona kuwa ukabila unachanganyika na kanisa lipi unasali ndio wanakuwa wengi, hii hususan kwenye mashirika na ma NGO ya nje. Yamelengwa kwa kuwa ndiyo yanayolipa zaidi na fungu la kumi linakuwa la uhakika. Hii haina utata.
Wewe nae bana, sipendi watu waliopofushwa na UCHAMA na UDINI, wananikera kweli maana hawafikiri nje ya box. Badala ya kuzungumzia suluhu dhidi ya tatizo la ajira za kujuana, unakuja na mambo ya kidini, upuuzi mtupu! Tanzania haitakuwa nzuri mpaka watu kama wewe mbadilike!
 
La mtu na mwanawe kuwa wote wanafanya kazi fulani, hili si tatizo. Wala hili si la Tanzania tu, kuna kila sababu ya mzazi akawa ni role model wa mwanae. Kuna kina George Bush, baba na mwana, kuna kina Gandhi, mama, mwana, mkwe. Kuna kina Karume, Baba mwana. Kuna wacheza mpira duniani na hapa kwetu, kuna madaktari na watu wa kazi, biashara na fani mbalimbali ambao watoto zao wanafata nyayo.

Tatizo letu hapa Tanzania ni pale unapokiingiza kijiji kizima, idara fulani au kabila hilo ndio linakuwa dominant kkwa kuwa tu Mkuu pale ni wa kabila hilo au unapowajaza waumini wa kanisa fulani kwa kuwa mkuu wa hapi muumini wa kanisa hilo.

Hili ndio tatizo. Lakini Ubunge, si inabidi uchaguliwe na wananchi, kama watachaguwa baba na akafanya kazi nzuri na asbwagwe kama alivyobwagwa mzee Malecela Dodoma, kuna kila sababu ya atapokuja mwanae kugombe watu wakamchaguwa.

Tumeona mfano wa Malima. Lakini leo hii unafikiri kuna mtoto wa Malecela anaeweza kugombea akapata? ng'oo! Ikiwa baba mtu kapigwa chini utategemea nini kwa mwanawe? Lakini ingekuwa Malecela kaona kuwa sasa umri umefika na siwezi tena kuwatumikia wananchi kama nilivyokuwa kijana, na akaamuwa kuwachia ngazi yeye mwenyewe bila kungushwa kisiasa. Angeondoka pale na heshima kubwa sana na endapo angetokea mwanae kugombea ingekuwa hakuna mpinzani.

Ms. FaizaFoxy!!
salaam kwako!
hii ni mara yangu ya kwanza(I guess so) kujibu hoja zako kwasababu mara nyingi nilikuwa sikubaliani nazo and most of the time you used to be more sarcastical than analytical, anyway tugange yajayo!

Nakubaliana na wewe kuhusu karibu yote uliyoandika ila ningefurahi sana kama unge-introduce the concept of opportunity especially in none elective positions. Mfano, Je ni sawa(miongoni mwa wananchi) mtoto wa Rais kwenda kusoma nje ya nchi kwa kutumia kodi za watanzania(regardless of her qualifications)?
Je ukisikia mtoto wa Waziri anapata nafasi andamizi ktk wizara yoyote hata kama babayake hafanyi kazi ktk wizara husika huwezi kuwa na shaka juu ya kilichopelekea mtoto huyo kufika hapo alipofika??

Mimi mashaka ninakuwa nayo hasa kwa kuzingatia matukio mbalimbali ambayo tayari ninayafahamu - nina hakika hata wewe mashaka utakuwa nayo, au ninakosea???
 
Fikra zako ni finyu sana, na hujui namna ya kuongea. Kumbuka kuwa kuchangia thread si kuingia tu na kuanza kupayuka, hoja hazijengwi namna hiyo, jaribu kujifunza kuangalia approach za watu ili upate labda kujifunza ni nini approach ya mdahalo ni nini "rapport" kama hujui ku "establish rapport" jifunze, usikurupuke.

Bado una mengi ya kujifunza na ikiwa unaingia JF unajifanya ndio unajuwa kila kitu, ujuwe wewe ni bado sana, hujajuwa ku "communicate" hata kidogo. Tazama ulichochangia na utazame wengine wanaelekea wapi, wakati hoja zinaendelea usikurupuke.


Faiza,Embu demonstrate namna ya Kujenga hoja vinginevyo na wewe haujui ila umechagua kujihesabu "Mwerevu"!!
Nevertheless,u are not under any obligation to respond to my comment,No Hard Feelings!!
 
Cv yangu ipo Facebook karibu anytime, ila sifanyi kazi serikali ya Bongo. However ondoeni Boriti kwanza huko kwenu ambako Wabunge wenu na watoto wao wote ni wabunge kwenye hili la undugu wote tumepotea! Ha! Ha! Mzee wa Michigan nana unavyocheza ngoma yako mwenyewe leo, finally! - Le Mutuz
 
W.J.Malecela kawaida kwangu ni kichefu chefu. Umefika hapo kwa mlango upi mpuuzi wewe. Una akili sawa na baba yako miaka 52 Kiongozi lakini hana Landmark yoyote. Ungekuwa unaipenda Tanzania usingeng'ang'ania kukaa nje. Njoo ukae na mama yako wa kambo.
 
Faiza,Embu demonstrate namna ya Kujenga hoja vinginevyo na wewe haujui ila umechagua kujihesabu "Mwerevu"!!
Nevertheless,u are not under any obligation to respond to my comment,No Hard Feelings!!

Naona nimeelezea kwa ufupi hapo, lakini hukunielewa. Lakini kwa kuwa hupenda kutoa darsa, ntakupa darsa kidogo; kwanza unaanza kwa ku "establish rapport". Ukishajuwa hilo. Mengine ni sahali. Jee, unajuwa ni nini hicho? Kama hujuwi itabidi ukafunguwe nyuzi jukwaa la elimu nije kukupa darsa la nguvu.

Undugunaizeshen ni tatizo sugu Tanzania na haukuanza leo na upo toka enzi za Nyerere na ndipo ulipopatia hilo jina "ndugunaizeshen".
 
Cv yangu ipo Facebook karibu anytime, ila sifanyi kazi serikali ya Bongo. However ondoeni Boriti kwanza huko kwenu ambako Wabunge wenu na watoto wao wote ni wabunge kwenye hili la undugu wote tumepotea! Ha! Ha! Mzee wa Michigan nana unavyocheza ngoma yako mwenyewe leo, finally! - Le Mutuz

Mkuu Le Mutuz, suala la nepotism ni janga la kitaifa. Hakuna chama au taasisi inayopona katika hili. Unavyoendelea kusema huko kwenu jamaa unakua unajiweka chini sana...hilo mbona linaeleweka mkuu, just chill out!

Wewe jibu hoja kama kuna kujuana katika balozi zetu ama la!!
 
Well, people this is fun, vyama vyote vinanuka na undugu, isipokuwa Mleta mada amesema Uongo hakuna mtoto wa Mkapa ubalozi wowote Duniani. Tuwache majungu! - Le Mutuz

Ni kweli Benjamin William Mkapa ana watoto wawili - ila MKAPA ana kaka yake (ambaye ninafikiri amefariki a couple of years ago - ninaomba samahani kama nitakuwa ninamuua mimi!) ambaye ni BERNARD WILLIAM MKAPA ambaye alikuwa anaishi maeneo ya Chang'ombe unubini, na huyo BERNARD MKAPA ndiye BABA wa ANDREW MKAPA ambaye ni msajili wa makampuni binafsi nafikiri ndiyo mnaita BRELLA or something like that, huyo anayefanya kazi US bado sijamfahamu lakini kama yupo ni mtoto wa BERNARD maana alikuwa na watoto 5 ukiondoa Acquiline ambaye alifariki miaka 14 iliyopita ambaye ni mkubwa wa Andrew Mkapa - so hakuna majungu yoyote aliyoleta mtoa mada!!!!!
 
Undugunaizeshen ni tatizo sugu Tanzania na hauikuanza leo na upo toka enzi za Nyerere na ndipo ulipopatia hilo jina "ndugunaizeshen".

Sawa. Je, ni sawa kuendelea nao hata kama ulianza kwa Nyerere? Mwalimu mwenyewe alishawahi kusema kwamba tatizo hao aliowaachia kijiti wanachukua yale mabaya yake na kuacha mazuri!!
 
Back
Top Bottom