Kuna haja ya kuwa na mfumo mbadala wa uchumi...........(kodi za tra ni mfano mmojawapo)

dostum

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
215
110
Ni zaidi ya wiki tatu sasa nafatilia usaliji wa kampuni ambayo itakuwa na kazi kama wakala wa tigo na mpesa na office gen supply. nishakamilisha brela na wiki hii nakamilisha TRA inshallah. Nikiwa TRA nimeambiwa nilipie kama 530,000/- hizo wamesema wamenikadiria stamp duty na withholding tax. halafu nikaenda kwa mkadiriaji mwingine wa income tax wamenikadiria shs 800,000/- na nilipowaomba wanipunguzie wakanijibu kuwa eti mie nina shombe shombe hivyo ninao uwezo wa kulipa. zaidi ya hapo wanaseaa tukichelewa kulipa kutakuwa na faini........ sikukubaliana na malipo hayo nikampigia simu rafkiangu kama ataweza kunisaidia. matokeo yake wamemkubalia nilipe shs 600,000/-income tax. (Ni kigezo gani waliona yafaa kodi iwe 800,000/- na kwa kigezo kipi yaliona yafaa kuwa 600,000/) inavyoonyesha hawa wakadiriaji wanaangalia sura badala ya kutumia sayansi ya biashara zaidi................. kisiasa lengo lao litakamilika kuwa wamevuka malengo kwa kukusanya kodi bt in reality wananchini wa kawaida tunaumia. kwa muono wangu naona kwa mfumo huu badala ya kujikwamua kutoka kwenye lindi la umasikini............. serikali inatulazimisha tuwe masikini. kwani kabla tu biashara haijaanza tunapaswa kuilipia kodi. wenzetu kama afrika kusini hakuna kodi yeyote anayolipia mchuuzi (small to medium entrprenuor) na hivyo hatuhitaji tu mabadiliko ya kisiasa bali kama mabadiliko hayo yatabadili na sera za kinyonyaji za kozi hapa tanzania. kwani wakati wageni wanafaidika na misamaha ya kodi wazawa wanaangamizwa kwa kodi kubwa. ukweli hali hii inasikitisha na kufurahisha..............inasikitisha kwa kuwa tunaumia ndani yanchi yetu na inafurahisha kuona watanzania hao hao tunaung'ang'ania mfumo huu angamizi
 
Back
Top Bottom