Kuna haja gani ya watendaji wa namna hii kuendelea na nyazifa zao

Mtini

JF-Expert Member
Apr 28, 2011
1,486
2,332
Shule nyingi nchini haziko kwenye mazingira ya kuridhisha, baadhi hazin madawati, madarasa ya kutosha, walimu wa kutosha pamoja na vitendea kazi vya kutosha. Hali hii hupelekea wanafunzi wengi kufanya vibaya na hata wengine kumaliza elimu ya msingi bila kujua kusoma na kuandika. Majuzi juzi waziri wa elimu katoa agizo kwamba walimu wakuu ambao wanafunzi watafika darasa la tatu bila kujua KKK watafukuzwa kazi, hivi kweli katika mazingira ya shule zetu kama hizi (pichani) watajua KKK kweli au ni kumuonea tu mwalimu mkuu?

Mi kwa ushauri wangu naona kabla ya mwalimu mkuu kufukuzwa, Mkuu wa mkoa, wilaya na mkurugenzi katika maeneo zenye shule kama hizi wafukuzwe kazi maana wameshindwa kusimamia maendeleo ya wananchi
 

Attachments

  • FB_IMG_1450684279979.jpg
    FB_IMG_1450684279979.jpg
    9.2 KB · Views: 99
  • FB_IMG_1450684289145.jpg
    FB_IMG_1450684289145.jpg
    9.6 KB · Views: 85
Back
Top Bottom