Elections 2010 Kuna aliyetarajia dr. Slaa kushinda urais?

Mukuru

Member
Apr 14, 2009
40
0
Kwa mazingira ya kisiasa ya sasa nchini ni kujidanganya kuwa kiongozi wa upinzani anaweza kuwa Rais kupitia njia ya kura. Kwa hiyo yeyote aliyetarajia kuwa Dr. Slaa angekuwa Rais ama hayafahamu vizuri mazingira halisi ya kisiasa au anajidanganya kwa kujipa matumaini 'hewa'. Haiwezekani kuwa Rais nje ya CCM kwa mazingira ya sasa kwa sababu nyingi tu - nitaorodhesha chache:

  • CCM inatumia rasilimali 'zake' na za nchi kuhakikisha mgombea wake anakuwa 'celebrity' na hivyo kuwazuga wapiga kura wengi hasa wa vijijini.

  • Tume ya uchaguzi inaundwa na mwenyekiti wa CCM - hivyo wajumbe wake lazima watalinda 'ulaji' wao. Hawawezi kuhatarisha 'ajira' yao kwa kuzingatia haki.
  • Katiba imeionyoonyeshea njia CCM kwani inatamka wazi kuwa NEC ikishatangaza matokeo ya urais, hakuna mahakama yoyote inayoweza kuhoji matokeo hayo.
  • Bado Dr. Silaa anahitaji walau kipindi kingine kuweza kuwashawishi watanzania hasa wa vijijini umuhimu wa mabadiliko. Inachukua muda kwa walio wengi kuelewa hasa ukizingatia tumekuwa katika mfumo wa chama kimoja kwa muda mrefu.
  • CCM inatumia mtaji wa umaskini na elimu duni kwa wa watanzania walio wengi. Ukiwa maskini wa hali na elimu, uwezo wako wa kuangalia mbali unapungua, hivyo faraja ya muda mfupi ni kitu kikubwa bila kuangalia athari hasi za muda mrefu. Hivyo CCM hutumia vitu kama tisheti, kofia, vitambaa na vijisenti kama kivutio kwa wapiga kura. Kwa mwananchi ambaye hata uwezo wa kununua aspirini 2 hana, kitu kama kofia ni kitu cha thamani kubwa kwake.
 
Tunaweza, nia hamna tu ususani hawa wanaojiita wapinzani maana wanashindwa kuunganisha nguvu...wakati wanelewa umoja ndiyo ulitufanya tupate uhuru, ulileta mabadiriko kenya, zambia, malawi, etc...Pili ni sisi wapiga kura, hivi tungejitokeza at leat asilimia 70, nadhani vibao visingesoma hivi....kuna zaidi ya wapiga kura million 20, waliojitokeza ni million 8. Hapa je tunaweza kuleta mabadiriko? N a tutambue kuwa wasiojitokeza kupiga kura ni wale wanaojiita wasomi na walalamikaji wa kila siku kuwa serikali utendaji wake hupo chini...let us think twice, we can, tumuandae kijana kama vile Zitto ili 2015 agombee tuone na watu tujitokeze. :doh:
 
Nakubaliana kabisa na mdau kwa uchambuzi wako, lakini nina uhakika hata hao wachache wenye elimu tanzania (sio wote) bado wanatatizo kubwa la kufikiri yaani upeo wao ni duni sana kwa sababu zifuatazo. Kwa wachache nilowadadisi baada ya kujua mtazamo wao niligundua sababu zifuatazo:
1. Pamoja na elimu yao lakini waoga wa kuangalia na kuchambua ukweli.
2. Hawajui wanahitaji nini na nini ni haki yao hivyo chochote kwao ni sawa.
3. Hawajui haki zao, though hawawezi kupata katika mfumo wetu.
4. Ubinafsi wakifikiria kuwa siku moja hao walio kwenye system watawapa nafasi.
Sasa hili ni tatizo sana ukiongezea na mfumo wenyewe. Tunahitaji elimu ya uraia ya ziada ili watu wajue haki yao na wawe tayari kuidai kwa hali yoyote pale wanapodhulumiwa.:bowl:
 
Back
Top Bottom