Kumradhi Mh Zitto Kabwe

Mwizi akija na kukuibia kitu ambacho ulikuwa unakihitaji kwa kiasi halafu akaja kukuuzia ukakataa wewe ni mtu makini. Hitaji la kitu chako likikuzidia utapiga magoti kwa mwizi wako akuuzie? Dowans a.k.a Loliondo ni kampuni ya kilaghai kama ilivyokuwa Richmond. Iliingizwa nchini kwa baraka za JK (akilipa deni x) na kwa msaada wa Ra. Nilishasema kuwa hii mitambo ni lazima inunuliwe. Kununuliwa kwake hakuhusiani hata chembe na hali ya umeme nchini. Kwa maneno mengine deni lazima lilipwe na hakuna wa kulilipa isipokuwa serikali. Kama vichwa vyote vya wasomi wetu vinategemea dowans kuiokoa nchi na tatizo la umeme basi inatubidi tuwaulize walipokuwa watoto walikuwa wanapata lishe ya namna gani.
 
Mwizi akija na kukuibia kitu ambacho ulikuwa unakihitaji kwa kiasi halafu akaja kukuuzia ukakataa wewe ni mtu makini. Hitaji la kitu chako likikuzidia utapiga magoti kwa mwizi wako akuuzie? Dowans a.k.a Loliondo ni kampuni ya kilaghai kama ilivyokuwa Richmond. Iliingizwa nchini kwa baraka za JK (akilipa deni x) na kwa msaada wa Ra. Nilishasema kuwa hii mitambo ni lazima inunuliwe. Kununuliwa kwake hakuhusiani hata chembe na hali ya umeme nchini. Kwa maneno mengine deni lazima lilipwe na hakuna wa kulilipa isipokuwa serikali. Kama vichwa vyote vya wasomi wetu vinategemea dowans kuiokoa nchi na tatizo la umeme basi inatubidi tuwaulize walipokuwa watoto walikuwa wanapata lishe ya namna gani.
At last nimekusikia mkuu wangu maanake nilianza kujiuliza mengi sana!...kumbe tupo bus moja! Ufuuuuuuuuh, raha ilioje, nashusha pumzi zangu.
 
viongozi wa upinzani kuweni macho (kama kweli ninyi ni genuine wapinzani), CCM wajanja sana...mnajua wazi kwamba kuwepo kwenu kwenye hizo kamati zao sio bure...unless na nyie mnaweka maslahi binafsi mbele ya maslahi ya taifa

tulitegemea viongozi wa upinzani ndio muwe mstari wa mbele angalau kututetea bungeni, lakini matokeo yake inaonekana CCM wamesha take advantage na kutumia umaarufu wenu kuhalalisha ulaji wao

in the future mtashindwa kuwawajibisha au kuwakemea mafisadi au hata ku mention ufisadi kwa sababu ya haya mnayofanya sasa.
 
Mwakyembe+1.jpg

wakati tunasota na giza huyu mheshimiwa alisema hivi:

"LIWALO NA LIWE NA HATA IKIBIDI TAIFA KUINGIA GIZANI SITOJALI"


haya uko wapi huyu na wale wapiganaji wake ambao wengi wao wako Ulaya,USA na CANADA wakishinda kwenye computer zao na sana sana the closest wamefika Tanzania ni issa michuzi blog
 
I'm a good supporter of national benefit regadless of my party stance toward the ruling party and I would like to congratrulate mhe. Kabwe, Hongera, whatever you think is good for the country then it's your duty to do your paliamentary obligation. Don't always follow some members stance that "we are against this party,no matter what" Please always follows your instinct and do the right thing for your country, sio eti kwa kuwa you're against most of CCM policies ndio ubakie kimya hata kama kuna issue itakayoleta manufaa kwa kutoa sauti yako.
Hizi ndio siasa tunazozitaka, you are against bad ventures but also reasonable on few good ones for te benefit of your country. Nasema kudos Kabwe! you're doing the right thing. Don't worry about the moaners, you will always have some through your political journey.
 
Hahahahah,

Yaani Zitto atakuwa mtu wa ajabu kusikiliza porojo kama hizo. Hata nikibaki peke yangu, sitasita kusema kuwa Zitto hakuwa sahihi katika ushauri wake kwamba tumwage pesa nyingine kuwalipa wezi (DOWANS a.k.a Richmond). Na kama ni kulipa fadhira basi aendelee na kampeni zake! Dowans ni wizi hata ikibidi kukaa gizani hadi JK aondoke madarakani ni poa tu! Wasitufanye wajinga. Ipo siku siri iliyojificha ya Zitto kuwa kipenzi cha watawala na CCM kwenye hili suala la Dowans itafichuka. Nitabki Tomaso milele!

DC, na wala hutabaki pekee yako kamwe, Watanzania tumeshaamka siyo tena kama wa mwaka 47. Zitto alipopigia debe ile mitambo ya kifisadi alichemsha tena sana tu wala siyo siri.
 
nchi iko gizani na sie tulio on the ground ndio tunasulubika

walioko ulaya ahhh wao wamekaa kwenye viti kupinga na kutoa hoja ndefuuuu

kazi kweli kweli
 
Mwakyembe+1.jpg

wakati tunasota na giza huyu mheshimiwa alisema hivi:

"LIWALO NA LIWE NA HATA IKIBIDI TAIFA KUINGIA GIZANI SITOJALI"


haya uko wapi huyu na wale wapiganaji wake ambao wengi wao wako Ulaya,USA na CANADA wakishinda kwenye computer zao na sana sana the closest wamefika Tanzania ni issa michuzi blog
Kwa hiyo wewe unaunga mkono ununuzi wa mitambo ya kitapeli ili mradi taifa lisiingie gizani?
 
Mie hamu yangu ni kusikia yale atakayowaambia waandishi wa habari kesho. Baada ya hapo hunda nikapigia mstari maneno ya wahenga, "SIKIO LA KUFA HALISIKII DAWA".
 
Yani hawa Tanesco wangekuwa China sijui ingekuaje.Wewe pesa mmepewa mwaka mzima hawajaagiza mitambo !halagfui leo wanatukuimbusha Dowans?k
 
Sijajua wala siamini kama watanzania ni wagumu sana kuweza kuzuia mitambo ya Dowans isinunuliwe.Kama JK angetaka inunuliwe bila shaka hakuna wa kuzuia, jamani nchi hii hatuna hizo sifa , ni wapigaji wa kelele.

Swala ni je mwananchi wa kawaida anafaidika nini na hali ya sasa na hii mivutano??

Yaani nguvu za kupinga ufisadi Tanzania zimefanikiwa kwenye kuzuia Dowans!!!!! sitaki kuamini hilo

Hii ishu inanichanganya wakuu, kama tunaweza kununua Dowans si tunaweza kununua mingine badala yake, kama ishu hii waamuzi wa mwisho ni wakubwa, ambao hakuna mtu yeyote wa kuwafanya lolote(kama hupo jitokeze) kwa nini basi tusikubaliane nao??? People are dying out there!
 
Huu wote ni ukosefu wa principles tu, hamna geni!

Tuwafungulie kutoka jela walawiti, wauaji, majambazi, n.k. kwa vile nchi yetu haina pesa za kutosha?!!

Watu wengine mnaonekana mko tayari kulala (kimapenzi) na wazazi wenu eti kwa vile tu jambazi limewashikia mtutu kichwani!! Let's suffer na vibatari vyetu, lakini Dowans na nduguye Richmond nasema NO!!!

heshima mbele mkuu.......tuko ukurasa mmoja............
 
mh zitto, nianze kwa kukiri mimi nilikuwa miongoni mwa wana jf wengi tuliokuzonga kwa kejeri, shutma, kashfa na dhihaka kadha wa kadha kuhusiana na msimamo wako kwenye suala zima la ununuzi wa mitambo ya dowans.

Mheshimiwa, ulikuwa sahihi kwa kusimamia kile unachoamini ni sahihi. Hii ndio sifa adimu ya kiongozi. Naamini hata wewe mwenyewe ulijua toka mwanzo kuwa uamuzi wako wa kutetea ununuzi wa mitambo ile hautakuwa popular na pengine ni kitanzi cha kisiasa. Lakini kwa ujasiri usiomithilika uliendelea kujenga hoja na wengi tulitia pamba masikioni mwetu na kukuita majina mabaya lukuki. Binafsi nilikwenda mbali zaidi na kukuita fisadi. Hili ndilo limenisukuma kuandika waraka huu mfupi ili kukuomba msamaha kwa maandishi yote machafu juu yako. Naamini tupo wengi wa aina hii lakini wenzangu wanakosa uthubutu wa kukiri na wanajichimbia kwenye keyboard zao.

Taifa leo lipo latika kiza, kwa sababu ya watu wachache waliokataa ushauri wa wataalam. Wale "wapiganaji" wanaona soni nyuso zimewashuka wanatapatapa kutafuta justification ya uamuzi wao mbovu ambao umeligharimu na utaendelea kuligharimu taifa kwa hasara kubwa.

Mheshimiwa watani zangu wazaramo wana msemo ufuatao "akutukanae kilabu cha pombe usisubiri kesho yake na wewe mrudishie matusi yake huko huko kilabu cha pombe" kwa kuwa kashfa nilizitoa hapa jf nalazimika kuomba msamaha hapa hapa jf na ni matumaini yangu utanisamehe.

Nimalizie kwa kukiri na kusema kuwa mh, wewe ni hazina ya taifa hili. Kama kiongozi vision yako ni kubwa kuliko umri wako. Pamoja na kuwa wanasiasa wanaepuka sana kujiingiza katika masuala tata kwa kuchelea kushusha credibility zao wewe umeweka utanzania wako mbele bila kuogopa kupoteza umaarufu wako wa kisiasa and spot on, you got it right.

Bravo mh zitto na endelea na misimamo yako thabithi yenye manufaa kwa taifa letu.

Mheshimiwa naomba kuwasilisha

walewale mafisadi, yaleyale mafisadi yanaji-recycle kama ma-vyuma chakavu...
 
Masatu,
Mkuu wangu labda wewe omba radhi kwa sababu unachobishana hapa JF ni ubishi tu usiozingatia umuhimu wa hoja nzima ya mahitaji yetu.
Zitto na viongozi wengine wote wanafikiria kama wewe, yaani kutatua tatizo ndio mpango yakinifu wa maendeleo yetu..kwa njia hiyo hatuwezi kuwa wabunifu hata kidogo..Hatuwezi kujenga mipango bora ya ujenzi wa taifa letu changa na maskini ikiwa tunafikiria kutatua marttatizo kama vile maskini mwenye njaa anayetafuta mlo wa siku..
Mawazo ya Zitto yaweza kuwa mazuri kwa sasahivi kwa sababu tu tuna njaa, lakini ktatizo mloshindwa kuliona ni kuuza mwili wetu kwa sababu ya mlo wa siku. Kesho tutaendelea kuuza mwili na mwisho wake kuzoea umalaya wa kuuza mwili, jambo ambalo Zitto, Lipumba na viongozi wengine wameshindwa kuliona.
Mkuu wangu kama serikali imeshindwa kutekeleza hata mradi mmoja wa ufaji umeme kama tulivyoahidiwa, Zitto alitakiwa kusimama upande wa pili kama kiongozi wa Upinzani ambaye analitakia mema Taifa letu badala yake amejiunga na mpango wa kutatua matatizo tuliyokuwa nayo kwa njia ya Umalaya.

Well wewe unaweza kuomba samahani lakini navuyojua mimi njaa hiyo ya siku mbili tatu, hatujafa bado.. kweli tuna shida lakini hatuwezimkuuza mwili wetu kwa sababu Zitto kasema.
As a fact mimi naunga sana mpango wake wa kuachana na siasa kutogombea Ubunge arudi kazini akafanye kazi alosemea..I thought he stand with us kama wapinzani wa utawala huu unapofikia maswala mazito kama haya lakini anapounga mkono upotoshaji huu kwa sababu tu matokeo yake yamepangwa kuwa hivyo... nasikitika kusema kachuuzika! He is a Lost boy kisiasa!


Mkandara,

Watz kama hawa ndo wanaohitajika. Unajua unaweza ukawa Chadema tena kada, mwanzilishi na kweli mzalendo lakini mawazo yako yakajengwa na kwenye misingi ya CCM. Afadhali ingekuwa misingi ya Mwl. JKN.
 
nchi iko gizani na sie tulio on the ground ndio tunasulubika

walioko ulaya ahhh wao wamekaa kwenye viti kupinga na kutoa hoja ndefuuuu

kazi kweli kweli

Nasisi tulioshimoni je? No Dowan even the sun. Better to stay as always
 
Zitto is a champion on this issue.
After being given technicalities of buying,transportation and installation of new machines he realized that,no way can new machines be bought and operate in time before the country be in DARK.
It could be wise to buy those for emergence while procedures are made to tackle the problem once and for all.
"Strong man is the one who stands alone". Zitto you're the one.
 
Back
Top Bottom