Mimibaba
JF-Expert Member
- Jul 1, 2009
- 4,557
- 1,291
Hivi karibuni mbunge wa Arumeru Mashariki J. Nassari alikaririwa na vyombo vya habari akitoa matamshi fulani (yanayoonekana kama ya kichochezi) juu ya kanda ya kaskazini kujitenga na kumzuia raisi kufika/kuitembelea Arusha. Kauli hizo za Nassari kwa kiasi chake sio nzuri na wala hazipaswi kutamkwa na kiongozi yeyote na haswa haswa kutoka CHADEMA (kumbuka CHADEMA inahusishwa na ukanda).
Wengi wamejitokeza haswa hapa JF kumtetea Nassari huku wengine wakirefer kauli nyingine mbovu zilizowahi kutolewa na viongozi mbalimbali. Mi naamini kumtetea Nassari hatumsaidii wala hatumjengi kisiasa, jambo la msingi ni wote tukubali kuwa Nassari alikosea na kama tunampenda basi tumlazimishe aombe radhi na kufuta kauli na sio kumtetea wakati kosa lipo wazi na linaonekana kwa kila mtu.
Upuuzi wa kiwango cha daraja la kwanza