Kumkataza Magufuli kubomoa majengo yaliyojengwa kwenye hifadhi za barabara ni ujinga mkubwa

Hakikwanza

JF-Expert Member
Dec 11, 2010
4,034
1,003
Mimi binafsi na muunga mkono Mheshimiwa waziri kwa kubomoa majumba yaliyojengwa kwenye hifadhi za barabara na yote yanayoendelea kujengwa.Unajua kuna watu hadi sasa wanaendelea kujenga majumba ktk hifadhi za barabara ukimuuliza anakwambia kwani zitajengwa leo hizo barabara? Halafu ikibomolewa anataka fidia,pia nyumba hizi zinaleta ajali,unakuta saa nyingine gari limekata breki dreva inatakiwa atafute eneo la usalama wa kujiokoa,sasa eneo la usalama ni hifadhi ya barabara nahapo unakuta nyumba zimejengwa,Dreva anagonga hizo nyumba kujiokoa au anabaki barabarani kuhofia kugonga watu wengi na baadae ni maafa makubwa yanatokea.Halafu watu wanakurupuka kumkataza bila vigezo huu ni upuuzi.Pia mpangilio wa makazi umekuwa mbovu kwa kuwa karibu na barabara kwani barabara ni nyembamba halafu majumba yamezikaribia hivyo hata ukiharibikiwa na gari hakuna sehemu ya dharura ya kuegesha gari hasa mijini,hivyo gari unakuta limeegeshwa barabarani na kuwa chanzo cha ajali.PIA WATANZANIA HATUJAMBO KWA KUVUNJA SHERIA UKIANZA NA VIONGOZI WETU NA BAADAE MWANANCHI WA KAWAIDA sasa mheshimiwa anakomesha wengine wanakuja na matamko ya kumpinga huu ni ujuha haswa.
 
hapo ni sawa na kuahirisha msiba ila kufa mtu kesha kufa kuna siku tutazika.
Hayo majengo yatajabomolewa iwe leo au kesho tena kwa aibu kubwa.

Hifadhi ya barabara inatumika kwa mambo mengi ya kimaendeleo mfano kupitisha mabomba ya maji taka/safi,umeme,simu,gesi na yanatakiwa yapishane kwa distance flani flani.
pia ni njia ya dharura in case things go wrong.(HAPA JK anatuamianisha hayo matumizi yatafanyika huku nyumba zikiwepoo kama si ujinga)?
Pili Magufuli hajavunja sheria wajenzi ndio waliovunja sheria sasa JK anasupport wavunja sheria
 
Uifikilie kubomoa tu, hawa watu waliojenga kwenye maeneo hayo wamepewa viwanja na halmashauri za miji na majiji, hivyo uamzi wa kubomoa bila kufuata utaratibu siyo haki ya msingi, wakulaumiwa ni watu wa mipango miji na idara ya ardhi ya eneo husika , vilevile serikari hawaweki vigingi vya kuonyesha mipaka kwa mda muafaka, unapimiwa kiwanja inachukua miaka 10 kuweka vielelezo vya eneo , lakini yote haya ni kutokana na kutokuwa makini kwa serikali yetu, na ufisadi ndiyo chimbuko la hayo yote
hivyo waliomkataza magufuri wako sahihi . unadhamini ghari kuliko binadamu????????????
 
Wanamzuia Magufuli kwa kuogopa kukosa KURA miaka ijayo... Vile vile wanafikiri wanampunguzia UMAARUFU,.Akili zao hazijajua watu walishachoka nao.. Eti kutetea wananchi ni kuacha kubomoa nyumba zao walizozijenga barabarani... Hapo hakuna kitu..
 
Uifikilie kubomoa tu, hawa watu waliojenga kwenye maeneo hayo wamepewa viwanja na halmashauri za miji na majiji, hivyo uamzi wa kubomoa bila kufuata utaratibu siyo haki ya msingi, wakulaumiwa ni watu wa mipango miji na idara ya ardhi ya eneo husika , vilevile serikari hawaweki vigingi vya kuonyesha mipaka kwa mda muafaka, unapimiwa kiwanja inachukua miaka 10 kuweka vielelezo vya eneo , lakini yote haya ni kutokana na kutokuwa makini kwa serikali yetu, na ufisadi ndiyo chimbuko la hayo yote
hivyo waliomkataza magufuri wako sahihi . unadhamini ghari kuliko binadamu????????????
hapo red sasa kama kosa sio la Magufuli ya nini kumdhalilisha?kwa nini serikali isiwachukulie hatua kali hao maofisa uliowajata?
DECI mchezo mchafu na haramu naunga mkono serikali kuufuta manake lilikuwa janga ILA kwa nini serikali ISIWACHUKULIE HATUA MAOFISA WAKE WALIOWAACHA DECI WAFANYE UPUPU WAO WA KUWALAGHAI WANAINCHI?
JK aliogopa pale Magufuli aliposema 'hata majengo ya CCM napomoa"
 
hapo red sasa kama kosa sio la Magufuli ya nini kumdhalilisha?kwa nini serikali isiwachukulie hatua kali hao maofisa uliowajata?
DECI mchezo mchafu na haramu naunga mkono serikali kuufuta manake lilikuwa janga ILA kwa nini serikali ISIWACHUKULIE HATUA MAOFISA WAKE WALIOWAACHA DECI WAFANYE UPUPU WAO WA KUWALAGHAI WANAINCHI?
JK aliogopa pale Magufuli aliposema 'hata majengo ya CCM napomoa"

haa haaaaaaaaa haaaaaaaaaaa ... mkuu punguza hasira...!
 
Ukifanya kazi na ****** halafu aone au ahisi unapata sifa nzuri kumzidi lazima aweke mizengwe tuu!!
 
Mimi binafsi na muunga mkono Mheshimiwa waziri kwa kubomoa majumba yaliyojengwa kwenye hifadhi za barabara na yote yanayoendelea kujengwa.Unajua kuna watu hadi sasa wanaendelea kujenga majumba ktk hifadhi za barabara ukimuuliza anakwambia kwani zitajengwa leo hizo barabara? Halafu ikibomolewa anataka fidia,pia nyumba hizi zinaleta ajali,unakuta saa nyingine gari limekata breki dreva inatakiwa atafute eneo la usalama wa kujiokoa,sasa eneo la usalama ni hifadhi ya barabara nahapo unakuta nyumba zimejengwa,Dreva anagonga hizo nyumba kujiokoa au anabaki barabarani kuhofia kugonga watu wengi na baadae ni maafa makubwa yanatokea.Halafu watu wanakurupuka kumkataza bila vigezo huu ni upuuzi.Pia mpangilio wa makazi umekuwa mbovu kwa kuwa karibu na barabara kwani barabara ni nyembamba halafu majumba yamezikaribia hivyo hata ukiharibikiwa na gari hakuna sehemu ya dharura ya kuegesha gari hasa mijini,hivyo gari unakuta limeegeshwa barabarani na kuwa chanzo cha ajali.PIA WATANZANIA HATUJAMBO KWA KUVUNJA SHERIA UKIANZA NA VIONGOZI WETU NA BAADAE MWANANCHI WA KAWAIDA sasa mheshimiwa anakomesha wengine wanakuja na matamko ya kumpinga huu ni ujuha haswa.

waziri ngwini.

rais ngwini.

ndiyo maana hata wakikatazana hawawezi kujenga hoja kihandisi.
 
Wanamzuia Magufuli kwa kuogopa kukosa KURA miaka ijayo... Vile vile wanafikiri wanampunguzia UMAARUFU,.Akili zao hazijajua watu walishachoka nao.. Eti kutetea wananchi ni kuacha kubomoa nyumba zao walizozijenga barabarani... Hapo hakuna kitu..

Duuh, mmezugwa mkazugika!! bado mnawaza CCM inaowachapa kazi, Magufuli,jk,Pinda lao moja wanatucheza shere! kajifunze Polituical game uone sio kukumbilia kushika mwenge wa upambe!!
 
hapo ni sawa na kuahirisha msiba ila kufa mtu kesha kufa kuna siku tutazika.
Hayo majengo yatajabomolewa iwe leo au kesho tena kwa aibu kubwa.

Hifadhi ya barabara inatumika kwa mambo mengi ya kimaendeleo mfano kupitisha mabomba ya maji taka/safi,umeme,simu,gesi na yanatakiwa yapishane kwa distance flani flani.
pia ni njia ya dharura in case things go wrong.(HAPA JK anatuamianisha hayo matumizi yatafanyika huku nyumba zikiwepoo kama si ujinga)?
Pili Magufuli hajavunja sheria wajenzi ndio waliovunja sheria sasa JK anasupport wavunja sheria

jk si bingwa wa kusahahu!?

nakumbuka ajali moja ilishawahi kutokea eneo la Kimara ambapo gari iliacha njia na kugonga nyumba iliyokuwa kandokando ya barabara na kuserereka mpaka chumbani na kuuwa watu wawili waliokuwa wamelala.

kikwete is no serious.
 
Mimi binafsi na muunga mkono Mheshimiwa waziri kwa kubomoa majumba yaliyojengwa kwenye hifadhi za barabara na yote yanayoendelea kujengwa.Unajua kuna watu hadi sasa wanaendelea kujenga majumba ktk hifadhi za barabara ukimuuliza anakwambia kwani zitajengwa leo hizo barabara? Halafu ikibomolewa anataka fidia,pia nyumba hizi zinaleta ajali,unakuta saa nyingine gari limekata breki dreva inatakiwa atafute eneo la usalama wa kujiokoa,sasa eneo la usalama ni hifadhi ya barabara nahapo unakuta nyumba zimejengwa,Dreva anagonga hizo nyumba kujiokoa au anabaki barabarani kuhofia kugonga watu wengi na baadae ni maafa makubwa yanatokea.Halafu watu wanakurupuka kumkataza bila vigezo huu ni upuuzi.Pia mpangilio wa makazi umekuwa mbovu kwa kuwa karibu na barabara kwani barabara ni nyembamba halafu majumba yamezikaribia hivyo hata ukiharibikiwa na gari hakuna sehemu ya dharura ya kuegesha gari hasa mijini,hivyo gari unakuta limeegeshwa barabarani na kuwa chanzo cha ajali.PIA WATANZANIA HATUJAMBO KWA KUVUNJA SHERIA UKIANZA NA VIONGOZI WETU NA BAADAE MWANANCHI WA KAWAIDA sasa mheshimiwa anakomesha wengine wanakuja na matamko ya kumpinga huu ni ujuha haswa.
Huyu JK na watendaji wake hasa PM wote ni wa ajabu, ikiwa watamzuia J P Maghufuli kubomoa na wanataka barabara za flyover wanategemea zitajengwa vipi mijini bila kubomoa??????? Vitu vingine lazima uvitoe sadaka kupisha vitu vingine!!!! Kama ujenzi wa nyumba mpya lazima ubomoe ya zamani pamoja na kukata miti ingawa vyote ni muhumu. Maghufuli anafanya kazi yake yuko sahihi ni bora kumuacha ili nchi ipate maendeleo!!!!!!!! Kumzuia ni kudumaza maendeleo!!! Mwenye akili ataona ujinga unaofanywa na hao viongozi!!!
 
Uifikilie kubomoa tu, hawa watu waliojenga kwenye maeneo hayo wamepewa viwanja na halmashauri za miji na majiji, hivyo uamzi wa kubomoa bila kufuata utaratibu siyo haki ya msingi, wakulaumiwa ni watu wa mipango miji na idara ya ardhi ya eneo husika , vilevile serikari hawaweki vigingi vya kuonyesha mipaka kwa mda muafaka, unapimiwa kiwanja inachukua miaka 10 kuweka vielelezo vya eneo , lakini yote haya ni kutokana na kutokuwa makini kwa serikali yetu, na ufisadi ndiyo chimbuko la hayo yote
hivyo waliomkataza magufuri wako sahihi . unadhamini ghari kuliko binadamu????????????


Hapo kwenye red.

Mimi sijajua kama mtu akivunja sheria inahitaji huruma! Vile vile sina hakika kwenye hili kuna haja ya kumwambia Magufuri awache kubomoa. Endapo watu walijenga bila utaratibu NYUMBA na vingine vibomolewe iwekwe miundombinu. Haya mambo ya kuwambia watu wasubiri wawe na utu ndo yalisababisha rais kuwambia wezi wa EPA warudishe hela ikiwezekana wasamehewe, kana kwamba mwizi anaweza kuiba na kukwepa mkono wa sheria. Endapo matatizo yako kwenye halmashauri za wilaya, basi hizo ndo zibanwe na wamiliki wa nyumba na kuwafidia wala si kumzuia Dr Maguifuri kufanya kazi yake
 
Back
Top Bottom