Hakikwanza
JF-Expert Member
- Dec 11, 2010
- 4,034
- 1,003
Mimi binafsi na muunga mkono Mheshimiwa waziri kwa kubomoa majumba yaliyojengwa kwenye hifadhi za barabara na yote yanayoendelea kujengwa.Unajua kuna watu hadi sasa wanaendelea kujenga majumba ktk hifadhi za barabara ukimuuliza anakwambia kwani zitajengwa leo hizo barabara? Halafu ikibomolewa anataka fidia,pia nyumba hizi zinaleta ajali,unakuta saa nyingine gari limekata breki dreva inatakiwa atafute eneo la usalama wa kujiokoa,sasa eneo la usalama ni hifadhi ya barabara nahapo unakuta nyumba zimejengwa,Dreva anagonga hizo nyumba kujiokoa au anabaki barabarani kuhofia kugonga watu wengi na baadae ni maafa makubwa yanatokea.Halafu watu wanakurupuka kumkataza bila vigezo huu ni upuuzi.Pia mpangilio wa makazi umekuwa mbovu kwa kuwa karibu na barabara kwani barabara ni nyembamba halafu majumba yamezikaribia hivyo hata ukiharibikiwa na gari hakuna sehemu ya dharura ya kuegesha gari hasa mijini,hivyo gari unakuta limeegeshwa barabarani na kuwa chanzo cha ajali.PIA WATANZANIA HATUJAMBO KWA KUVUNJA SHERIA UKIANZA NA VIONGOZI WETU NA BAADAE MWANANCHI WA KAWAIDA sasa mheshimiwa anakomesha wengine wanakuja na matamko ya kumpinga huu ni ujuha haswa.