Kumekucha ubungo terminal

Huwezi kupanga mji kwa kuondoa wakazi ambao mji wao umepangika vizuri kama Ubungo. Lengo lao ni kupanua Stand ya Mkoa ili kupata maslahi kwa matumbo yao kama ilivyo sasa bila kujali hasara na usumbufu kwa wakazi.
Moja ya upangaji wa mji, ni kuwepo kwa huduma za jamii. Stendi ya kutosha ni moja ya huduma muhimu za jamii. Ni kwa bahati mbaya kuwa miji mingi yetu (Tanzania) ilitangulia kabla ya Afisa mipango miji. Hivyo katika kupanga, watu lazima wahamishwe, na hii inapo kugusa, lazima uumie, na kulalamika ni lazima. Wakati mwingine, ili kukwepa lawama, serikali huhamisha miji, na ndiyo maana unasikia miji kama "Old ....." Kwa kuwa Dar haiwezi kuhamishwa, basi lazima serikali ukubali lawama hizo. Najua inauma sana, lakini haina dawa.
 
Nafikiri bado hatujui matumizi sahihi ya ardhi.Kiluvya ni mbali sana na jiji kama nakaa temeke nimefika usiku itakuwa safari nyingine kuja hadi ninakoishi.Pale pale Ubungo wanaweza kuipanua bila kulazimisha kuhamisha watu.Tunatakiwa ujenzi wetu uendane na matumizi ya ardhi kwa mfano stand ingekuwa kuanzia chini kama sokoni kariakoo sehemu ya kati na ghorofa kama stand za baadhi ya nchi za nje lakini tukishatengeneza stand tusiwe na huduma kama za bar,viduka kwani hizi sehemu zinatakiwa ziwe kwa ajili ya mabasi na huduma nyingine zipatikane nje ya stand
 
happiness win mawazo yako yanaweza kuwa mazuri ila unayasema sehemu ambayo tunaosoma sio tunaopanga mipango ya maendeleo; unaweza kuwasilisha mawazo yako kwa baadhi ya madiwani unaofahamu au wewe mwenyewe kagombee udiwani ili ukatetee kile unachokiamini

Ndachuwa, ujue habari zote zinazoandikwa humu JF zinawafikia vizuri sana. Usijali, ujumbe hata wakiupata ana kwa ana serikali t=ya CCM ina desturi ya kupuuza tu kila kitu, mbaya zaidi ikihisi huwaungi mkono na sio mwenzao. Hata miongoni mwao wenyewe wanapingana hadharani, sembuse wewe ambaye hawakujui ila kwa kodi yako tu?
 
Moja ya upangaji wa mji, ni kuwepo kwa huduma za jamii. Stendi ya kutosha ni moja ya huduma muhimu za jamii. Ni kwa bahati mbaya kuwa miji mingi yetu (Tanzania) ilitangulia kabla ya Afisa mipango miji. Hivyo katika kupanga, watu lazima wahamishwe, na hii inapo kugusa, lazima uumie, na kulalamika ni lazima. Wakati mwingine, ili kukwepa lawama, serikali huhamisha miji, na ndiyo maana unasikia miji kama "Old ....." Kwa kuwa Dar haiwezi kuhamishwa, basi lazima serikali ukubali lawama hizo. Najua inauma sana, lakini haina dawa.

Ni kweli unachokiongea. Lakini huoni serikali inapaswa kuangalia kama kuna ulazima wa kuwahamisha wakazi wa Ubungo? Stand ya Mkoa si lazima iwe Ubungo, kuna maeneo mengi tu nje ya mji ambayo yanajengeka kwa kasi sasa na yangefaa kuwa na Stand ya Mkoa. Serikali ingeweza kujenge Ma-stand mengi tu ya mkoa, kwa mfano, Mkulanga, ingekuwa kwa Mabasi yanatokea mikoa ya njia hiyo, Kiluvya, na maeneo mengine mengi ambayo bado yana sehemu kubwa tu. Ubungo ingeweza kubaki stand ya kisasa tu bila kuwahamisha walala hoi.
 
Miradi ya wakubwa hii.

Miradi ya wakubwa au Miradi ya MAFISADI,wakubwa wafanyapo miradi huwa ni kwa manufaa ya taifa hata kama wao pia wananufaika kutokana na miradi hiyo,miradi ya MAFISADI haingalii manufaa zaidi ya nini watafaidi kama wao kwa mradi ambao kimsingi unakuwa ni kiini macho tu,ni wakati mwafaka wa kutawanya JIJI hili kwa miradi mikubwa kama mradi wa KITUO KIKUU CHA MABASI ya masafa marefu...Ubungo hapatoshi hata wakibomoa nyuma yake na hata pembeni bado kwa jiji lenye mipango endelevu lenye maona ya miaka 50 na kuendelea huwezi kuanzisha mradi mkubwa kwenye eneo ambalo ni dogo na linagombaniwa na huduma nyingine nyingi zitakiwazo jijini kwa kadri ya maendeleo yalivyo.

Ni sawa na upuuzi wa kuwaondoa watu KIPAWA badala ya kuangalia eneo mbadala na kujenga uwanja mkubwa utaoweza kuendana na kasi ya ukuaji wa uchumi wetu PINDI inchi ikipata waendeshaji wazuri (Nategemea kasi ya ukuaji ambayo hata rekodi zilizopo hazina kama tutapata VIONGOZI NA SIO WASANII kama waliopo)
Ubungo imezungukwa pande zote,Airport imezungukwa pande zote,bado tunayo maeneo makubwa sana na mazuri kwa miundominu bora tukiwa na mipango mizuri ambayo bado inaweza tumika hata ya miaka 300 ijayo.
 
Unafikiri utabadili mipango ya serikali kwa kujadili hapa jf

Kwa hiyo tufanyeje? tusijadili hapa kwa kuwa serikali haitatusikiliza? Ni vizuri kujua nini kinaendelea nchini kwetu na kupata mawazo ya Ma Great thinkers, inatusaidia hata kupanua uelewa wetu; bila shaka ndio maana uko hapa.
 
Upanuzi utakuwa nyuma ya stand ila kibadado itamegwa kidogo kwa pembeni kwa lengo la kunyoosha vizuri hiyo stand yao.

Wewe upo jikoni nini maana unaeleza kama vile unafahamu mpango mzima! Nakumbuka mkuu wa mkoa Sadick this year alisema stand itahamishwa ubungo kupisha mabasi ya mwendo kasi hapo ebu tueleze kuhusu hili Hapiness.
 
Wewe upo jikoni nini maana unaeleza kama vile unafahamu mpango mzima! Nakumbuka mkuu wa mkoa Sadick this year alisema stand itahamishwa ubungo kupisha mabasi ya mwendo kasi hapo ebu tueleze kuhusu hili Hapiness.


Siko jikoni, ila jambo hili linanigusa sana.

Ni kweli Bw. Sadick alisema stand itahamishwa, sasa imekuwa kinyume wakazi ndio wanaotakiwa kuhama na stand itapanuliwa.
 
Hapo kuna wenye maslahi yao hasa wenye magorofa Unungo, Sinza na Manzese watakua wamefanya fitina ili wasipate hasara stand ikihamishwa maana wamewekeza kwa pesa nyigi mahoteli yao !
 
Hapo kuna wenye maslahi yao hasa wenye magorofa Unungo, Sinza na Manzese watakua wamefanya fitina ili wasipate hasara stand ikihamishwa maana wamewekeza kwa pesa nyigi mahoteli yao !



Ndio shida ya inji hii kila kitu ni kwa maslahi ya walionacho!lol
 
Hizo ni dalili za mawazo finyu kwani bado tuna sehemu zenye nafasi kubwa kwa ajili ya kujenga stand kama madau mmoja alivyo pendekeza KILUVYA.Huku ni kutafuta uraji tu.Kwa kumbukumbu zangu eneo hilo la UBT ni mali ya UDA labda kama umiliki wake ulibadilishwa.Nchi hii kila siku jambo jipya la maudhi,dah yaani kichwa kinauma sana!
...halafu baba mwenye nyumba huuuyoooo nje anaenda msibani nyie mvuruane hukuuuu mpaka basi.
 
Ningeelewa kama ungekuwa unashauri ihamishwe kabisa isiwepo eneo lolote hapo Ubungo, sio TBS, Chibuku wala maeneo ya karibu!
 
Back
Top Bottom