Kumbukumbu ya mauaji ya Daudi Mwangosi

tenende

JF-Expert Member
Jan 10, 2012
6,511
500
Leo tarehe 2/9/2014 imetimia miaka miwili tangu mwandishi wa habari wa Channel ten Ndugu Mwangosi alipouawa kinyama na jeshi la polisi mkoani Iringa tarehe 2/9/2012, na baadaye kuzikwa wilayani Rungwe mkoani Mbeya.

Mwangosi aliuawa na polisi akitafuta habari kwenye mikutano midogo midogo ya CHADEMA iliyoandaliwa kwa ajili ya kufungua misingi na matawi ya chama.

Kutoka katika kutafuta habari akageuka yeye mwenyewe kuwa habari nzito iliyotikisa taarifa za habari za hapa nchini na nje ya mipaka ya nchi.
Ripoti za awali za polisi zilionyesha mauaji hayo yamefanywa na waandamanaji waliomrushia Mwangosi kitu chenye ncha kali.

Lakini picha za mauaji hayo ziliporushwa mitandaoni zilishtua wengi na kunyamazisha polisi kuficha ukweli wa mauaji hayo. Walionekana polisi wakifanya kitendo hicho bila huruma yoyote?

Taarifa niliyoipata leo jioni toka Wilayani Rungwe kwa Saimoni Mwaisope ni kwa kwamba, Leo mchana kutakuwa na mikusanyiko midogo ya kumbu kumbu ya mauaji ya kikatili ya Mwangosi (Iringa - Nyololo na Mbeya - Rungwe). Mwaisope amesema tunamkumbuka kwa kutafakari mambo mbali mbali ya husuyo kifo chake na mengineyo.

Mytake:

Nasi twaweza kuanza kutafakari jambo hili:
1. Kwa nini aliuawa?
2. Nani aliagiza?
3. Wauaji wako wapi?
4. Mjane na watoto wa marehemu wanaishije?
5. Kamuhanda yuko wapi? n.k.

Mnamo mwezi Agosti na September 2012 Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kilifanya ziara ya ujenzi wa Chama (M4C) huko Mkoani Morogoro na Mkoani Iringa. Tarehe 02/09/2012 kulikuwa na ufunguzi wa Ofisi ya Chama katika Kijiji cha Nyololo. Polisi walizuia ufunguzi wa ofisi hiyo kinyume na taratibu na sheria kwa kisingizio cha kuendelea kwa zoezi la sensa ya watu na Makazi ambayo Kimsingi zoezi hilo lilikuwa limeisha na taasis na vyama vingine vya siasa vilikuwa vinaendelea na shughuli zao kama kawaida. Mathalani Chama cha Mapinduzi (CCM) kilikuwa kinaendelea na kampeni huko Zanzibar.

CHADEMA tulisema agizo lile la kusitisha ufunguzi wa ofisi yetu halikuwa halali kwa sababu agizo la awali ilikuwa ni kusitishwa kwa mikutano ya hadhara peke yake na si mikutano ya ndani. Ufunguzi wa Ofisi yetu haikuwa mkutano wa hadhara. Polisi walijipanga kutumia nguvu kupita kiasi ambapo majira ya asubuhi waliwatangazia wananchi wasitoke nje wala kushiriki katika shughuli hiyo. Mchana ulipofika Viongozi na Wanachama wetu wakiongozwa na Mh. Benson Kigaila walifika eneo hilo la ofisi ambapo Polisi kwa upande wao wakiongozwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa Michael Kamhanda waliamua kutumia nguvu kuvunja shughuli hiyo na hatimaye askari wapatao saba wakiwa na silaha za moto walimzingira na kumlipua Mwandishi wa Habari wa Kituo cha Channel Ten ndugu Daud Mwangosi kwa bomu na kumwaga utumbo palepale. Kwa kweli ilikuwa ni miongoni mwa matukio mabaya sana, na la kinyama kuwahi kutokea katika nchi yetu

Ndugu Wananchi Wenzangu leo ni takribani miaka miwili sasa imepita tangu kutokea kwa tukio hilo; hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa na serikali kwa wahusika, Kamanda Kamhanda bado yuko mtaani kana kwamba hakufanya chochote tena alipandishwa na cheo kabisa baada ya tukio lile. Askari aliyefunguliwa kesi ambaye hatumfahamu na hatawahi kuonekana na wananchi hatujui hata kesi yake hiyo imeishia wapi tayari yameshafunika kombe mwanaharamu apite kama walivyosema Wahenga wetu.

Sisi kama Chama kupitia Kamati Kuu yetu tuliitaka serikali kupitia Rais kuunda tume ya kijaji kuchunguza matukio haya ambayo tumekuwa tukifanyiwa na polisi ambapo wanachama na mashabiki wetu wanauawa bila hatia lakini serikali imeziba masikio na isitoshe mauaji yameendelea. Mtakumbuka kule Soweto Arusha ambapo polisi hao hao walitupa bomu kwenye mkutano wetu wa hadhara na kuua watu wengine wanne. Morogoro walimuua Ally Zona, Igunga akafa Mbwana Masoud, Arumeru alichinjwa ndugu Mbwambo na watuhumiwa wakakamatwa lakini tunaambiwa walitoroka wakiwa mikononi mwa Polisi tena wenye bunduki za SMG. Napenda kurudia tena kuitaka serikali iunde tume ya kimahakama ili Taifa lijue ukweli na uhakika wa nani hasa anahusika na mauaji haya ya watu wetu.

Ndugu Wananchi wenzangu wakati umefika wa sisi kupaza sauti zetu kwa nguvu kuungana na vilio vya damu za ndugu zetu hawa na mateso ambayo makundi mbalimbali yanapata bila hatia katika jamii yetu. Tunao ndugu zetu Albino wanakufa na hakuna anayechukua hatua, wengine wanateswa na kudhalilishwa wakiwa mikononi mwa vyombo vya usalama na sheria kisa tu eti hawakubaliani na Serikali. Hivi karibuni tumesikia wanavyofanyiwa Masheikh 19 walioko mahabusu, wanadhalilishwa sana kisaikolojia. Kuna vijana wetu walibakizwa kesi za ugaidi nao waliteswa na kuharibiwa sehemu za siri na jeshi la polisi. Imefika wakati sasa tuunganishe nguvu zetu kupambana na ukatili huu.

Napenda kuchukua fursa hii kutoa salam zangu za rambirambi kwa familia ya marehem Mwangosi na kwa wanahabari wote. Nawatia moyo wanahabari kuwa majasiri hususan wakati huu tunapoelekea katika chaguzi mbalimbali katika nchi yetu. Mwalimu Nyerere alisema ukishakula nyama ya mtu hutaacha hivyo tunatarajia kabisa Polisi na Watawala wataendeleza mauaji haya hasa watakapoona dalili za wao kunyanganywa dola lakini tusiogope tutashinda.

Dr.Wilbrod Slaa
Katibu Mkuu 02/09/2014

Leo ni siku ambayo kaka yetu mpendwa Daudi Mwangosi alifariki, Machungu ya kushambuliwa kwa kipigo, kisha kwa bomu na kikosi cha FFU huko mkoani Iringa katika eneo la Nyololo chini ya amri iliyotolewa na Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Iringa wakati huo RPC Kamuhanda

Tunaweza kujifunza nini juu ya utashi wa viongozi wa dola la Tanzania katika utekelezaji wa sheria mbali mbali? Mimi sijui sana kama kweli tuna nia ya dhati ya kuwatoa wa Tanzania hapa walipo ili wayafikie maisha bora kwa kila mtanzania.

Kwa kuwa nilikuwepo siku ya tukio, nilishuhudia yote na kwa kuwa nilikuwa kiongozi wa chadema wakati huo. Ningeomba niwashirikishe machache juu ya tukio zima. nimeattach document ambayo, nimeiandika mimi mwenyewe kwa kutumia vithibitisho halali vya chama lakini pia vya jeshi la polisi. Mpango wangu ni kuandika kitabu. tutaendelea kuwasiliana pale inapobidi

Justin Mpotwa

Leo ni mwaka wa pili toka aliyekuwa mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari mkoa wa Iringa Daudi Mwangosi auawe pale kijiji cha Nyororo Mufindi wakati akiwa katika kazi yake ya kuandika habari.
Serikali sikivu ya CCM japo imeoneshwa kila aina ya ushahidi imepuuza kuwachukulia hatua stahiki waliofanya ukatili huu.Tumeambiwa waliofanya ukatili huu wamepandishwa vyeo na watawala wetu wasikivu.

Dhihaka nyingi zimefanywa juu ya kifo hiki hata kufikia hatua ya mpiga propaganda Habibu Mchange kusema mauaji yalifanywa na CHADEMA.Anataka tuamini eti watu waliovalia sare za polisi tunaowaona kwenye picha ya mauaji ni CHADEMA na magwanda yao.
Familia yake na ndugu zake, IPC, UTPC na wadau wengine hawawezi kamwe kusahau mauaji ya Daudi Mwangosi kwani yalikua ni mauaji ya kinyama na ukatili wa hali ya juu.

Kuna kila dalili kwamba wauaji wameshajitangaza washindi hapa duniani.R.I.P Mwangosi.

PIA SOMA
- TANZIA - Iringa: Mwandishi Mwangosi auawa katika vurugu kati ya Polisi na CHADEMA
attachment.php
 
RIP Dav Mwangosi, tutakukumbuka uliuliwa ukiwa unatekeleA majukumu yako kwa jamii.

Maccm yakaoana yakukatishe uhai wako.

Tutakukumbuka daima, mzimu wako usiache kuwafuata Majidi na Ludo pia maccm yote yaliokuuwa.

RIP shujuaa Mwangosi
 
Ingekuwa vyema kama hizi nguvu mgezipeleka kwa familia ya marehemu kusomesha watoto wake na kumsaidia mjane kiuchumi.

Na ingekua vizuri zaidi hizi nguvu zingewekezwa kwenye investigation ili wauaji wapate kile kinachostahili.
I keep on wondering... kwanini public inadanganywa kuwa laws zipo kwaajili ya kulinda haki ya mtu.... in my opinion, sheria zimewekwa kwaajili ya kulinda uozo wa watu fulani....
 
Kuna mwendawazimu anayetuhumiwa kupanga mauji ya Dr. Slaa ameibuka na kusema CHADEMA ndio waliomuua Daud Mwangosi kule Iringa. Hivyo kwa mujibu wa wendawazimu wake hao wanaoonekana pichani wakiutoa uhai wa Mwangosi kama vile wanaua nyoka, ni CHADEMA. Kamuhanda yeye baada ya mauaji ya Mwangosi, alipandishwa cheo!
 
Ingekuwa vyema kama hizi nguvu mgezipeleka kwa familia ya marehemu kusomesha watoto wake na kumsaidia mjane kiuchumi.

CDM itaendelea kusaidia familia bila kujitangaza
 
Ingekuwa vyema kama hizi nguvu mgezipeleka kwa familia ya marehemu kusomesha watoto wake na kumsaidia mjane kiuchumi.
Mwambie Gamba mwenzio Chris Lukosi huu ni muda muafaka wa kurudisha rambirambi za marehemu pamoja na riba baada ya kuzifanyia biashara kwa miaka miwili
 
Last edited by a moderator:
Mwambie Gamba mwenzio Chris Lukosi huu ni muda muafaka wa kurudisha rambirambi za marehemu pamoja na riba baada ya kuzifanyia biashara kwa miaka miwili

Mkuu huyu gamba Chris Lukosi hawezi rudisha hata senti tano ndio kwanza Ana tanulia huko ughaibuni.
R.I.P Mwangosi huko uliko pumzika kwa amani ila Chris Lukosi Kala rambirambi zako na hataki kuzirudisha.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu huyu gamba Chris Lukosi hawezi rudisha hata senti tano ndio kwanza Ana tanulia huko ughaibuni.
R.I.P Mwangosi huko uliko pumzika kwa amani ila Chris Lukosi Kala rambirambi zako na hataki kuzirudisha.

Damu ya Mwangosi itamwandama sana huyo jamaa! Hakuna rangi ataacha kuona!
 
Last edited by a moderator:
Hivi ile kesi ya yule polisi aliyekuwa akifichwa sura na askari wenzie, kila alipokuwa akipandishwa kizimbani, hivi ile kesi 'iliyeyukia' wapi?

Kwa sababu hatujaona mwendelezo wa ile kesi na mshiriki mwenzake wa mauaji ya Mwangosi, kamanda Kamuhanda, hatukuona akipandishwa kizimbani, na badala yake, tukashuhudia mkuu wake JK, akimpandisha cheo!
 
Leo tarehe 2/9/2014 imetimia miaka miwili tangu mwandishi wa habari wa Channel ten Ndugu Mwangosi alipouawa kinyama na jeshi la polisi mkoani Iringa tarehe 2/9/2012, na baadaye kuzikwa wilayani Rungwe mkoani Mbeya.

Mwangosi aliuawa na polisi akitafuta habari kwenye mikutano midogo midogo ya CHADEMA iliyoandaliwa kwa ajili ya kufungua misingi na matawi ya chama.

Kutoka katika kutafuta habari akageuka yeye mwenyewe kuwa habari nzito iliyotikisa taarifa za habari za hapa nchini na nje ya mipaka ya nchi.
Ripoti za awali za polisi zilionyesha mauaji hayo yamefanywa na waandamanaji waliomrushia Mwangosi kitu chenye ncha kali.

Lakini picha za mauaji hayo ziliporushwa mitandaoni zilishtua wengi na kunyamazisha polisi kuficha ukweli wa mauaji hayo. Walionekana polisi wakifanya kitendo hicho bila huruma yoyote?

Taarifa niliyoipata leo jioni toka Wilayani Rungwe kwa Saimoni Mwaisope ni kwa kwamba, Leo mchana kutakuwa na mikusanyiko midogo ya kumbu kumbu ya mauaji ya kikatili ya Mwangosi (Iringa - Nyololo na Mbeya - Rungwe). Mwaisope amesema tunamkumbuka kwa kutafakari mambo mbali mbali ya husuyo kifo chake na mengineyo.

Mytake:

Nasi twaweza kuanza kutafakari jambo hili:
1. Kwa nini aliuawa?
2. Nani aliagiza?
3. Wauaji wako wapi?
4. Mjane na watoto wa marehemu wanaishije?
5. Kamuhanda yuko wapi? n.k.

attachment.php
TAFAKARI YANGU KUHUSIANA NA PICHA YA MAUAJI YA MWANGOSI

Nikiwa nalengwa lengwa na machozi nimeiangalia na kuitafakari vizuri sana picha hiyo inayoonesha jinsi Mwangosi alivyotolewa uhai kikatilia sana. Mimi nimeiangalia na kuona kuna askari ambao walikuwa na uchu wa kumpiga na kuangamiza kabisa maisha ya Mwangosi na wale waliokuwa wanajaribu kuzuia wenzao asiendelee kushambuliwa na askari wenye uchu wa kutoa roho za watu. Mfano kuna askaari anayeonekana katikati akiwa ameshikwa kiunoni na Mwangosi huku Mwangosi mwenyewe akiwa ameshika kamera yake, anajaribu kwa kadiri awezavyo kuwazuia wenzake wasiendelee kumshambulia Mwangosi na ndio maana ilibidi Mwangosi ajishike kwake nafikiri wakati akianguka ili kujiokoa. Huyu askari anaonekana ameinua juu kirungu chake kama ishara ya kuwazuia wenzake wasiendelee kufanya unyama waliokuwa wakimfanyia Mwangosi. Kwakweli natamani kulijua jina la askari huyu pamoja na yeye mwenyewe. Alifanya jitihada za pekee lakini alishindwa kutokana na jinsi wauaji walivyokuwa na uchu na hasa huyu wa nyuma yake ambae ndio mlipuaji wa Mwangosi.

Mwingine anayeonekana kutaka kuzuia unyama huu ni huyo aliyeipa mgongo kamera. Huyu anaonekana kumzuia askari aliye kulia kwake ambaye anaonekana kwenda kwa kasi kumshambulia Mwangosi. Kuna huyo pia aliyevaa shati la kiraia akiwa na kofia nyeusi naye anaonekana kutaka kuzuia madhara zaidi.

Sasa askari watoa roho ni hao watatu wa upande wa kushoto au nyuma ya yule askari anayejitahidi kuzuia wenzake na ambaye ndiye ameshikwa kiunoni na marehemu Mwangosi. Hao ndio watoa roho wakuu wakiongozwa na huyo wa kushoto kabisa ambaye wakati huyo wa katikati anajitahidi kuzuia wenzake yeye akapata mwanya wa kufyatua kombora lake na kumtekeketeza kabisa mwanamwema Daud Mwangosi.

Huyo wa katikati ambaye ndiye anayeonekana kuwazuia wenzake huku Mwangosi akiwa amejishika kiunoni mwake anaonekana kama ni mtu aliyeona kuwa, kama ni kipigo alichokipata Mwangosi, basi kilikuwa kimetosha hivyo kuendelea zaidi ya hapo ingekuwa ni madhara makubwa ndio maana anajitahidi kuwazuia wenzake. Lakini kwa bahati mbaya alikuwa amezidiwa na askari waliokuwana uchu wa kumtoa roho Mwangosi.

Mimi binafi nawapongeza sana askari hao niliowaelezea kwa jinsi walivyojitahidi sana kuokoa maisha ya Mwangosi. Laana zote za duniani na mbinguni ziwaendee hao wengine wote waliohakikisha kuwa Mwangosi anafutika katika duniani hii kikatili kabisa, wa kwanza wao akiwa huyo Michael Kamuhanda na huyo mlipuaji wa bomu.

May the almighty God Rest In Peace the Innocent soul of Daud Mwangosi! AMEN!
 
Leo ni siku ambayo kaka yetu mpendwa Daudi Mwangosi alifariki, Machungu ya kushambuliwa kwa kipigo, kisha kwa bomu na kikosi cha FFU huko mkoani Iringa katika eneo la Nyololo chini ya amri iliyotolewa na Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Iringa wakati huo RPC Kamuhanda

Tunaweza kujifunza nini juu ya utashi wa viongozi wa dola la Tanzania katika utekelezaji wa sheria mbali mbali? Mimi sijui sana kama kweli tuna nia ya dhati ya kuwatoa wa Tanzania hapa walipo ili wayafikie maisha bora kwa kila mtanzania.

Kwa kuwa nilikuwepo siku ya tukio, nilishuhudia yote na kwa kuwa nilikuwa kiongozi wa chadema wakati huo. Ningeomba niwashirikishe machache juu ya tukio zima. nimeattach document ambayo, nimeiandika mimi mwenyewe kwa kutumia vithibitisho halali vya chama lakini pia vya jeshi la polisi. Mpango wangu ni kuandika kitabu. tutaendelea kuwasiliana pale inapobidi

Justin Mpotwa
 

Attachments

  • DAKIKA TANO KABLA YA KIFO CHA MWANGOSI.pdf
    411 KB · Views: 440
Hivi na huyo 'pandikizi' Mchange, aliyedai mauaji ya Mwangosi yaliratibiwa na kutekelezwa na watu wa Chadema, hivi ana maana na kamanda Kamuhanda naye ana kadi ya uanachama wa Chadema, kwa kuwa alikuwepo eneo la tukio alipouawa Mwangosi na ndiye aliyetoa 'go ahead' kwa yule askari ambaye alitekeleza amri ya mkuu wake wa kazi, kwa kumlipua Daudi Mwangosi!
 
baada ya polisi kusingizia kwamba aliuwawa na KITU CHENYE NCHA KALI nililidharau moja kwa moja jeshi la polisi .
 
Kuna mwendawazimu anayetuhumiwa kupanga mauji ya Dr. Slaa ameibuka na kusema CHADEMA ndio waliomuua Daud Mwangosi kule Iringa. Hivyo kwa mujibu wa wendawazimu wake hao wanaoonekana pichani wakiutoa uhai wa Mwangosi kama vile wanaua nyoka, ni CHADEMA. Kamuhanda yeye baada ya mauaji ya Mwangosi, alipandishwa cheo!

HABIBU MCHANGE , ameDHARAULIWA DUNIANI NA HATA AKHERA .
 
Mwambie Gamba mwenzio Chris Lukosi huu ni muda muafaka wa kurudisha rambirambi za marehemu pamoja na riba baada ya kuzifanyia biashara kwa miaka miwili

upelelezi umebaini kwamba MTAJI WA BIASHARA ZA LUKOSI ULIONGEZEKA GHAFLA SANA MARA TU BAADA YA UPOTEVU WA RAMBIRAMBI HIYO !
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom