Lutala
JF-Expert Member
- Jun 17, 2010
- 848
- 103
Ndugu wanajamii, napenda kuwashirikisha kumbukumbu ya miaka 11 tangu marehemu baba yangu alipoaga dunia. Ilikuwa ghafla sana, bila kuugua, bila kusema neno la mwisho alipokuwa safarini. Uchunguzi wa kidaktari ulibaini kuwa chanzo cha kifo ilikuwa ni blood pressure. Kila inapofika tarehe ya leo huwa natafakari sana juu ya tukio hilo. Namshukuru baba kwa kuwa alituachia misingi imara amabayo imetuwezesha kuwa pamoja katika familia na mwaka huu mtoto wa mwisho katika familia amefanikiwa kuhitimu masomo yake pale Tumaini Iringa.
Naposikia kibwagizo cha Twanga Pepeta cha "baba babaaaaaa - upo wapi wapi baba, nakuita baba" huwa kinanifanya kuimarisha tafakari yangu.
Bwana alitoa na bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe daima ........ Amina
Naposikia kibwagizo cha Twanga Pepeta cha "baba babaaaaaa - upo wapi wapi baba, nakuita baba" huwa kinanifanya kuimarisha tafakari yangu.
Bwana alitoa na bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe daima ........ Amina