kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 12,298
- 12,600
Nimeduazwa na kampeni za Obama na Romney kwenye mbio za kuelekea IKULU ya Marekani hivi juzi kwenye mdahalo wao wa pili. Obama na Romney yeyote atakaepita sera yake ya kwanza ni kurudisha viwanda Marekani ili wamarekani wapate ajira. Viwanda vingi vya Marekani vilihamishishiwa bara la Asia kwasababu thamani ya USDollar ni kubwa mno inayofanya gharama za uzalishaji ziwe kubwa mno Marekani, hivyo wenye viwanda walikimbilia China, India, Singapore, Japan, Africa kutafuta faida. Baada ya Marekani kushindwa kuishawishi China iongeze thamani ya fedha yake sasa wana mkakati wa kuishusha thamani ya dollar yao ili kuvutia uwekezaji na wamarekani walioikimbia nchi kibiashara kurudisha mitaji yao ya viwanda nchini mwao. Kwasasa Marekani haina viwanda kabisa, ukifika pale Detroit mji ambao ulikuwa chimbuko la viwanda duniani sasa hivi yamebaki magofu tu watu pia wameukimbia mji na majumba yao kwa kukosa ajira. Nikiwanda cha kutengeneza magari ya FORD tu ndicho bado kikubwa kilichobakia pale. Mkakati mwingine wa kukuza uchumi wao ni kuanza kuchimba mafuta na gesi yao wenyewe badala ya kuagiza bidhaa hizo ng'ambo. Hivyo, bei ya mafuta duniani nayo itashuka miserably kwakua mnunuzi mkubwa atabakia China na India tu. Kama Obama atapita atapunguza matumizi ya kijeshi kwa kupunguza ukubwa wa jeshi na kuacha vita Afghanstan. Hivyo nawapa tahadhali watu wanaoiabudu sarafu ya US$ kuwa kuweni chonjo msije mkapata hasara ghafla punde dola inaposhuka kufuatia mabadiliko ya kiuchumi yanayotarajiwa kufanywa marekani baada ya uchaguzi wa NOvemba.