Nilisoma jana thread ya kilichomtoa Kikwete Monduli,Mwandishi wa thread hiyo alionesha hisia zake kwa kile alichokiita kuwa aliondoka kwa aibu kubwa kutokana na kumchongea bosi wake.
Mimi nilivyofuatilia vizuri mjadala huu nikaona kuwa Kikwete alichofanya alitekeleza wajibu wake kumfahamisha Raisi kuwa kuna ukiukwaji wa taratibu kwani JWTZ ni chombo cha uma,hakiwezi mtu tu kwa kuwa ni bosi aanze kuliuzia jeshi bila ya Kuomba tenda ambayo imetangazwa kiuwazi kwa Watanzania wote ili washindane katika kutaka kuliuzia jeshi.
Nyerere kwa kusema nendeni mkamalizane wenyewe inanitia shaka kwamba aliridhia hali hiyo ya kuchanganya utumishi na kufanya biashara au la.
Pia nilitarajia kuona kama katika makala ile Nyerere amefuatilia kutaka kujua kama wameyamaliza vipi ili ajue kama kulikuwa na uadilifu au la.
Mwisho nawauliza wana JF kama Nyerere aliridhia hali hii ya mkuu wa kambi kubwa kama ya Monduli kufanya BIASHARA ya kuliuzia JWTZ bidhaa zake ni sawa au?
NAWASILISHA.
Mimi nilivyofuatilia vizuri mjadala huu nikaona kuwa Kikwete alichofanya alitekeleza wajibu wake kumfahamisha Raisi kuwa kuna ukiukwaji wa taratibu kwani JWTZ ni chombo cha uma,hakiwezi mtu tu kwa kuwa ni bosi aanze kuliuzia jeshi bila ya Kuomba tenda ambayo imetangazwa kiuwazi kwa Watanzania wote ili washindane katika kutaka kuliuzia jeshi.
Nyerere kwa kusema nendeni mkamalizane wenyewe inanitia shaka kwamba aliridhia hali hiyo ya kuchanganya utumishi na kufanya biashara au la.
Pia nilitarajia kuona kama katika makala ile Nyerere amefuatilia kutaka kujua kama wameyamaliza vipi ili ajue kama kulikuwa na uadilifu au la.
Mwisho nawauliza wana JF kama Nyerere aliridhia hali hii ya mkuu wa kambi kubwa kama ya Monduli kufanya BIASHARA ya kuliuzia JWTZ bidhaa zake ni sawa au?
NAWASILISHA.