Kumbe soksi chafu dili!

Jaguar

JF-Expert Member
Mar 6, 2011
3,438
1,026
Wachunguzi wa gonjwa sugu la malaria kutoka ifakara health centre wakiongozwa na doctor okumu,wamegundua kuwa soksi chafu zinazonuka uvundo zafaa katika mapambano dhidi ya malaria.Ule uvundo wa soksi ni harufu kutoka mwili wa binadamu hivyo mbu waipatapo harufu hii,kwa haraka huzivamia soksi na kuzengea hapo muda wote wakidhani kuna mwanadamu around.Kwa hiyo unaweza weka soksi chafu zenye uvundo kwenye kona ya chumba chako cha kulala,mbu wote watajaa huko na wewe utalala salama salimini kwa sababu ukali wa harufu ya soksi unazidi hata harufu ya mwili wako,mbu hawatakuwa na habari na wewe,watakuwa busy na soksi usiku kucha.Pia ukitaka kuwaua,ni rahisi tu,wakishajaa eneo la soksi zenye uvundo ni rahisi kuwaangamiza kwa dawa ya kupuliza.Lakini watafiti wanaendelea kutafuta dawa yenye kufanana na harufu ya soksi zenye uvundo(source,BBCSWAHILI).MALARIA HAIKUBALIKI,TUSHIRIKIANE KUITOKOMEZA!
 
Dah! Imeshafika humu?

Watu wako 'fasta'....I had an honour of working with Fredros Okumu at IHI, he is a brilliant young scientist (not a doctor yet) with lots of crazy but smart innovations on fight against malaria vector (mosquitos)! Bravo Fredos..
 
that means net kushusha tena basi..... huuuuureeeeeeee. ila mh? watu watalala kweli.
 
inabidi watu wakifika baa wavue viatu soksi zinuke uvundo na mbu hawatawang'ata
 
Hii habari nimeisoma mahali pengine. Tuseme iwe ni kweli, bado kuna maswali mengi ya kujiuliza.
Kwa nini zisiwe nguo alizovaa mtu mchana kutwa?
Ikiwa soksi zinazonuka uvundo ndio "Rungu" kwa mbu ikiwa utaziweka kipembeni, hicho chumba kitakuwa kinakalika kwa uvundo huo?
Anyway, mimi kwa hili sina la kuchangia saaaana, bora niendelee kusoma michango ya wengine kwanza. "It sounds me too local to be true"
 
Back
Top Bottom