Elections 2010 Kumbe kuna wabunge kumi wa chadema hawajatoka Bungeni Rais alipokua akihutubia bunge

kutokana na mdahalo wa jana nimesikia kua kuna wabunge kumi waligoma kutoka bungeni wakati wabunge wa chadema wakitoka nje ya bunge, yalielezwa na Hamad akijibu hoja ya Mbowe kuwa CUF inaonyesha kutowaunga mkono

jamani kwa nn hili hamlitaki kuliongelea

mjadala huo unaweza kuupata MZALENDO.NET « …Ni wakati wa ukweli na uwazi

Walikuwa wanaogopa kuvunja kiapo walichokula. Kumbuka walikula kiapo kuilinda katiba ya bongo ambayo ndo imemuweka madarakani rais. Na pia kuvunja ahadi ya kuwatumikia wananchi waliowachagua kuingia madarakani. Waliona bora lawama kuliko fedheha.
 
Sikweli asemalo Mtu wa pwani ukweli ni kwamba wabunge 10 hawaku ingia kabisa bungeni siku hio na sio waligoma kutoka bungeni
:hungry:

Kwenye mdahalo kati yake na Mbowe, Hamad alitamka kuwa Wabunge hawakuwalk out hotuba ya Rais. Mbowe hakubisha.
 
Walikuwa wanaogopa kuvunja kiapo walichokula. Kumbuka walikula kiapo kuilinda katiba ya bongo ambayo ndo imemuweka madarakani rais. Na pia kuvunja ahadi ya kuwatumikia wananchi waliowachagua kuingia madarakani. Waliona bora lawama kuliko fedheha.

mbona mwanasheria mkuu ametamka kuwa wabunge wa chadema hawajavunja sheria yoyote kwa kutika nje ya bunge, katiba sheria mama waliogopa kuvunja kifungu gani?
 
- The FACT ni kwamba yote Mh. Hamad aliyosema ambayo sio kweli Mh. Mbowe alijibu, lakini hili hakujibu hiyo ni FACT sihitaji zaidi in that case of the FACT, as a FACT!

William.

Lakini HR nadhani sio mtu makini katika kutoa matamshi... Hadithi aliyoitoa kuhusu mazungumzo yake na Ndesamburo kuwa Chadema ni wakatoliki na CUF waislamu haikupaswa kuongelewa kwenye jukwaa kama lile. Yaani hapo aliharibu pande zote mbili. Ni maneno usiyotegemea kutoka kwa viongozi makini, isipokuwa tu kwa wale wasioweza kuzuia hisia zao.
 
lakini hr nadhani sio mtu makini katika kutoa matamshi... Hadithi aliyoitoa kuhusu mazungumzo yake na ndesamburo kuwa chadema ni wakatoliki na cuf waislamu haikupaswa kuongelewa kwenye jukwaa kama lile. Yaani hapo aliharibu pande zote mbili. Ni maneno usiyotegemea kutoka kwa viongozi makini, isipokuwa tu kwa wale wasioweza kuzuia hisia zao.

ila huu ni ukweli na hamna haja ya kuuficha ila kwa chadema na ukatoliki nakataa waluteri tumo,walokole wengi sana wakatoliki wapo na waislam wengi sana cdm
 
kutokana na mdahalo wa jana nimesikia kua kuna wabunge kumi waligoma kutoka bungeni wakati wabunge wa chadema wakitoka nje ya bunge, yalielezwa na Hamad akijibu hoja ya Mbowe kuwa CUF inaonyesha kutowaunga mkono

jamani kwa nn hili hamlitaki kuliongelea

mjadala huo unaweza kuupata MZALENDO.NET « …Ni wakati wa ukweli na uwazi

Usipotoshe maana wabunge wote wa chadema waliokuwa ukumbini walitoka wale ambao hawakukubaliana na hoja ya kutoka hawakuingia kabisa ukumbini. Acheni upotoshaji!
 
“…fighting with a large army under your command is nowise different from fighting with a small one: it is merely a question of instituting signs and signals” …. Sun Tzu art of war
 
- Hapa sasa mkuu ndio kabisaa unakubaliana na hoja yangu kwamba mambo ya haraka haraka kabla ya wakati ndio yametufikisha hapa tulipo, ukweli ni kwamba matokeo ya uchaguzi yanaonyesha exactly wananchi walichosema then kwamba bado wanataka chama kimoja, Mwalimu alitakiwa kuwasikiliza wananchi maana ndio Demokrasia yaani wananchi kuamua wanachotaka, kuwalazimisha wasichotaka ndio matokeo yake haya ndugu yangu, wananchi bado wanachagua CCM tu!

- Maana yake ni kwamba tulifkiri kwamba vyama vingi ndio jawabu, sasa sio siri kwamba hatukuwa tayari, naona imeanza ya katiba sasa utabadili vipi katiba na majority ya CCM, ndio ninasema tusidanganyane jamani, mambo badooo kidogo tusitafute njia za mkato mkato ndio zimelifikisha hili taifa tulipo sasa, yaani kwenye dead end!

William.

Kaka William nadhani Tanzania ya sasa ina watu wachache sana wanaopaswa kupiga kura. Japo kwenye sheria za kupiga kura kuna watu ambao hawaruhusiwi kupiga kura kwa sababu ya umri au "afya ya akili" (kwa ufupi asiwe kichaa) nadhani hizo exclusion criteria hazitoshi. Tuna watanzania wengi ambao akili ya mambo ya siasa na maendeleo hawana kwa kuwa hawakwenda shule na hivyo kuwa na uwezo mdogo wa kujua mambo; na ingekuwa amri yangu nisingewaruhusu kupiga kura. Hata CCM hufanya hivyo kupitia CC. Mtu anapiga kura ya kitu asichojua, hii si haki. Hawa wote hatuhitaji tuwasubiri waelimike mpaka tufikishe asilimia 50%. Hivyo twaweza kuwawakilisha kwa sisi wachache kusikilizwa. Na hiyo theory ya kwamba taifa letu ni changa waitoa wapi mkuu? Kwani Kenya, Zambia na Tanganyika ipi ni taifa changa zaidi?
Lakini ukweli bado unabaki palepale, kwamba hata ikiwa watanzania wengi watahitaji mabadiriko ya katiba na kwa bahati mbaya wakuu wa serikali kutohitaji mabadiriko husika, basi hatutoweza kushinda. Na hizo kura zetu zenyewe nani kahakikisha kwamba zinakuwa hazitoshi? Uchakachuaji tu. Josef Stalin anasema "It's not the people who vote that count. It's the people who count the votes". So it doesn't matter how many people will cast their votes, since they will decide nothing. What matters, is for those people who count the votes (the government) who can decide everything, if they also believe and embrace changes in question.
 
Pengine ni kweli kwamba HR alichokisema hakikuwa sahihi...lakini hoja yake kwa namna nilivyomuelewa ni kuwa, CDM hawawezi kuwalaumu CUF kwamba hawakuwaunga mkono wakati kuna baadhi ya wanaCDM hawaungi mkono pia!
 
- Kuongezeka kwa Demokrasia hakuwezi kulazimishwa kwa nguvu na kubadili katiba under our current political situation ndio ndoto zenyewe hasa, maana utakua unabadili katiba under expense ya CCM na wananchi walioichagua kutawala, siamini kwamba hao walioandika kuhusu Demokrasia ndicho walichosema!

- Nimetoa mfano mdogo sana, eti ili NEC iwe fair itachaguliwa na nani under hiyo katiba mpya ya Chadema?



William.

Kuna mapungufu makubwa katika hoja yako:
Kama kweli wananchi wameichagua CCM kuendelea kutawala na una imani kuwa hata 2015 wataendela kuichagua, basi wataendelea kuichagua hata kama katiba itarekebishwa - sasa woga wa kubadili katiba wa nini? Kama unafikiri kubadili katiba itakuwa expense kwa CCM then ujue kuwa katiba purposely inawa-favour wao na katiba ya namna hiyo si ya haki. Kama unasimamia ukweli basi katiba hiyo unapaswa kuipinga.
Ili NEC iwe huru, bado mwenyekiti anaweza kuteuliwa na rais lakini kuwepo n vigezo vilivyoainishwa mapema. Na akishateuliwe kuwepo na chombo tofauti kama bunge kinachoweza kumjadili ili kupima neutrality yake. Halafu wajumbe wa tume watoke kwa wadau mbalimbali - vyama vya siasa, NGOs, dini/madhehebu mbalimbali nk wote wawakilishwe. Na uwakilishi huu uende down hadi ngazi ya jimbo. Kama kweli CCM inashinda kihalali kabisa basi itaendela kushinda hata ukiwepo uwazi wa aina hii maana uwazi huu hauondoi imani ya watu kwa CCM - woga wa nini?
Mbowe kasema hali inaweza kuwa mbaya zaidi 2015 endapo katiba haitarekebishwa - ni kweli - kwa nini kuendelea kuwepo kwa hofu, si ushirikishwaji wa kutosha uwepo ili hofu zipungue?. Mimi kama najiamini kuwa nashinda kihalali basi hata ukimleta refa toka wapi nitashinda, lakini kama naendelea kung'ang'ania refa na linesmen wawe wangu ndipo nishinde, niwazi ushindi huo utakuwa na kasoro.
Hivi kweli W.J.Malecela unaamini kwa dhati kabisa kuwa ni haki kwa rais kumteua mwenyekiti wa NEC na hakuna wa kuhoji uteuzi huo, na mwenyekiti huyo huyo akimtangaza huyo aliyemteua kuwa ndiye kashinda urais hakuna wa kuhoji?
Je katika suala la mihimili mitatu, Rais kwa kofia ya mwenyekiti wa CCM anamteua fulani kuwa kiongozi wa mhimili wa bunge (spika) - wale wengine wawili walikuwa geresha tu, na pia kwa kofia ya urais anamteua kiongozi wa mhimili wa mahakama - jaji mkuu, je unaamini kwa dhati kabisa kuwa wiongozi wa mihimili hii miwili hawatakuwa chini ya aliyewateua?
Kuendelea kuwa na katiba mbaya ari mradi walio madarakani katiba hiyo inawasaidia kuendelea kuwepo madarakani ni jambo la hatari. Akija penya dikteta mmoja hakika atatumia katiba hiyo hiyo kutuumiza sote. Unakumbuka suala la Balali - kwamba mengi aliyofanya sheria za fedha zilimruhusu kufanya hivyo na katumia sheria hizo hizo kufisadi fedha nyingi sana. Je akitokea mtu kama huyo ngazi ya urais si itakuwa hatari?
TAHADHALI KABLA YA HATARI!
 
Unaongelea ulichokiona kwenye mdahalo ,hata ungeona matusi ungeyaleta hapa!?kwa hiyo ulitaka mbowe ajibu hata upuuzi!?
 
Thanks kwa taarifa, mbona hata vyombo vya habari havijatamka juu ya hilo. Tupatie majina yao tuwajue "MATRAITORS".

JAMANI ujinga huu haujaanzia hapo tu, lazima tufuatilie tujue tabia zao toka utotoni na hata walipokuwa shuleni walikuwa ni watu wa aina gani.

hili ni funzo tunapochagua viongozi tusisome CV zao tu, maana CV za utotoni huwa hawaziweki.

Wengine unakuta walikuwa ni kina "TOTO TUNDU" waioambilika.

Wengine "TOTO JOGA" likigomwa kidogo tu Kiliooooo hadi majirani wasikie

Wengine " TOTO DEKA" kila kitu ng'eee ng'eee mama mie nataka ileee, mmm hii sitaki mama nataka ileeee!

wengine "TOTO JIZI" mama na baba wakiondoka nyumbani kazi kupekua masanduku au kuramba sukari.

sasa tusikurupuke kuchagua viongozi kwa kuangalia CV zao za masomo tu haya ndio matokeo yake.

kumbuka hata mashuleni tulipokuwa tukisoma, ukiwekwa msimamo fulani unakuwa wengine wanasepa haoooo huwaoni, au wale wanafunzi wa kujipendekeza, yaani likimwona teacher na mkoba, utaona hilo mbio kwenda mkumpokea, "shikamoo mwalimu".

VIJITABIA ni Kadhia kubwa inayotukabili ktk viongozi wetu wengi maana hawajaviacha vijitabia hivyo hadi sasa.

Tatizo ni kuwa media ikiwa upande mmoja nasi hauwezi kuwabalance media ikiamua kushabikia chama au mtu ujue ukweli wa upande wa pili hutaupata kwani mmesahau sakata la CCJ kwenye vyombo vya habari ilivyokuwa ina draw intentions za watu. Mie nilikuwa nakiona CCJ kama chama kikubwa sana kwa jinsi kilivyokuwa kinaripotiwa lakini hata leo hii ukimuuliza yule jamaa aliekimbia kutoka CCM kwenda CCJ na baadae CDM hajui ukubwa wa CCJ.
 
- The FACT ni kwamba yote Mh. Hamad aliyosema ambayo sio kweli Mh. Mbowe alijibu, lakini hili hakujibu hiyo ni FACT sihitaji zaidi in that case of the FACT, as a FACT!

William.

Willy, Hamad Rashid ndo source ya kuaminika? Why not CCM ambao kama Wachadema hao wasingetoka reaction isingekuwa zile walizozitoa kina Chiligati na Makamba, lazima wangezigusia tena hata JK aliyekuwa anatoa hotuba siku ile asingehamanika vile. Naamini Hamada Rashid ana agenda yake katika taarifa hiyo na kama si hiyo basi kauli yake mliyoinukuu kutoka kwenye mdahahalo mmeitafsiri vinginevyo.

Kwa mwenye ushabiki wa vyama hii ni habari ya kuaminika, lakini kwa mchambuzi wa mambo kauli hiyo ina malengo. Hata hivyo tujiulize, mbona nafasi rasmi ya Upinzani ilibaki wazi? Tena mbona CUF walikwenda kuikalia? Kama wangebaki Wabunge wa CHADEMA 10, CUF wasingeenda kuchukua nafasi ya upinzani, wangeendelea kuwepo walipokuwa wakati JK akihutubia.
 
Mheshimiwa Willima, Heshima sana,
Kwanza napenda kukupongeza kuwa kila mara wewe huleta hoja zinazojadilika na kuzungumzika humu jf. Leo umenichosa na mtazamo wako hasi juu ya suala la mabadiliko ya katiba na hata mfumo mzima wa NEC. Nadhani haya ni matokeo ya kutoshiriki siasa za nyumbani moja kwa moja na kuona matatizo yanayotuzunguka kama taifa.
Wakati huu tusipoziba ufa ujuwe kwa hakika tutajenga ukuta na utakuwa huko ulipo ukitoa ushauri na maoni kwenye mtandao kama unavyofanya leo. Ziko sababu za kutosha za katiba yetu kutazamwa upya kabisa
1. Suala la Muungano: Mfumo wa sasa hauturidhishi watanzania tlio wengi, na Kataba haiko clear kuhusu jambo hili, leo Zanzibar wana Makamu wa rais wawili ambao hawapo katika katiba yetu ya Jamhuri kwa sababu tu ya mfumo wa Zimamoto, Uwiwano wa uongozi na mzigo mkubwa unaobebwa na raslimali za bara kuendesha Zanzibar ni moja ya Changamoto kubwa.
2. Upatikanaji wa tume ya uchaguzi na namna inavyofanya kazi; Uchaguzi huu tume bila aibu inawaambia watanzania matokeo ya kawe na Ubungo yamechelewa kutangazwa kwa sababu ya matatizo ya miundombinu ya usafiri huku ikiwa tayari imetangaza matokeo ya Ngorongoro, Hivi Will huko US ndivyo mnavyofanya kazi kweli? Tume inasubiri watu wapigwe mabomu Mwanza ndiyo itangaze matokeo alafu unaipigia makofi Willy? Uko wapi uwiano wa Demokrasia unaouzungumzi! Alafu hakuna sheria ya kuwawajibisha hawa watu kisha unasema katiba inatosha iko sawa!! Ahaaa mzee think twice hapo, Tumeona katika kampeni hizi wakuu wa wilaya wakisoma taarifa za kazi kwa RizI ili mtoto asiharibu unga kwa baba, nguvu nyingi za serikali zimetumika kwenye kampeni kubeba chama tawala kwa sababu ya ubovu wa katiba, Hakuna mwenye chuki na RZ1 mbona nyie hatukuwaona mkitumia nafasi za wazee wenu ku propage siasa?? Rais ana vyeo vyingi mno vya kuteua watu na hivyo wanalazima kutumika kwa namna yoyote ili walinde nafasi zao alafu unasema hatutaki katiba itakayopunguza nguvu ya Rais, Bunge liliazimia mambo mengi baada ya Saga ya richmond, kwa sababu ya katiba mbovu hayakuenda popote maan na hiari ya Mkulu kuyafanyia kazi au kuyashiti, Hii ni aibu Willy nchi inahitaji katiba kabla kina Kayumba hawajachoka, watauana vibaya watakapochoshwa na mfumo unaoongeza mzigo wa umaskini vichwani mwao na kwa kuwa hutakuwepo utafuatilia kwenye Luninga na mtandao huku ukishaa. Mzee nchi inahitaji katiba iweke mambo sawa.
Mimi sikupiga kura mwaka huu, nina sababu nyingi za hovyo hovyo tu, moja ni kuchoshwa na mfumo mbovu usio na matumaini ya kumkomboa mtanzania, huko US manesi na madaktari ni moja kati ya makundi yanayolipwa vizuri hapa kwetu malipo mazuri yako kwenye siasa (Consumer unawalipa vizuri kuliko wanasayansi producer) Alafu Willy bado hutaki katiba eti tukuwe, hatuwezi kukuwa chini ya mfumo mbovu huu tuliionao ila tutadidimia
Mzee nina mengi lakini ngoja niache tu. nCHI INAHITAJI MABADILIKO YA KATIBA KABLA AKINA KAYUMBA WA MANZESE, BUGARIKA, MABATINI, HAWAJACHOSHWA NA HUU UFUKARA WA KUPINDUKIA




- Mkuu heshima yako sana, sikatai kwamba katiba yetu ina mapungufu ni kweli sana isipokuwa tatizo langu ni how to go about kuirekebisha kwa maudhui ya wananchi wote, wengi mnaolilia kubadilishwa mnaonekana kuwa na hisia kali sana bila kujali POLITICAL FACTS on the ground, hamuwajali kabisa wananchi wengi walioichagua CCM kushika power kwenye huu uchaguzi. Mnaonekana kuamini sana kwamba ni nyinyi tu Chadema wenye wabunge 46 ndio wenye mandate ya wananchi kuhusu the political future of our nation.

- Mnakosea sana, ushauri wowote wa kubadili katiba lazima uwajali CCM kwanza kwa sababu wananchi ndio wamewachagua for the last 50 years, nimesema na ninarudia kwamba Demokrasia, inataka wananchi wazungumze kupitia kwenye kura, kama kweli unaamini in Demokrasia then utaelewa point yangu kwamba ni vigumu sana kuibadilisha katiba under political system ya CCM wabunge 270 Vs Chadema wabunge 46, it is simply impossible. Otherwise inaonekana mnashauri tuvunje katiba, yaani tutumie njia za mkato kuirekebisha kwa ku-overpass katiba inayodai 2/3 ya wabunge kuirekebisha kikatiba,

- Kwa maneno mengine tuvunje katiba kwa ajili ya kuirekebisha katiba, ili wabunge wa upinzani 46 wawe na nguvu sawa na wabunge 270 wa chama tawala, hivi mkuu huoni kwamba itakua the joke of the century! Ninawaulizeni swali dogo sana, under your new proposal ya katiba mpya ili NEC iwe fair inatakiwa kuchaguliwa na nani?



William
Mkuu Willy,
Point of Correction, Mimi si mwanachama wa CDM, Mimi ni mwanachama wwa ccm hai anayelipa ada na michango yote ya chama. Kwa hiyo kudhani kuwa wanaotaka mabadiliko ya Katiba ni CDM tu hili kosa kubwa sana unalofanya.
Unapoangalia mwenendo wa siasa ya nchi ni muhimu kuwa makini zaidi kwenye maslahi wa nchi kuliko maslahi ya ccm, ni kweli CDM ina wabunge 48 tu lakini unatakiwa ukumbuke kuwa CDM wana madiwani 600 tena kutoka miji mikubwa yenye population kubwa ya wapiga kura wa nchi yetu. Sasa Jiji la Mwanza, nusu ya Arusha, Mbeya, Iringa, Moshi zote ziko mikononi mwa wapinzani, hata KAWE iko mmikononi mwa wapinzani. Kama ccm itaendelea kutumia mawazo yako hayo ya kupinga kila kitu kwa kuwa tu hakikuanzishwa na ccm nchi yetu itazama katika dimbwi baya sana.
NARUDIA TENA NI VEMA TUANGALIE SUALA LA KATIBA NA KUREKEBISHA MAPUNGUFU MENGI YALIYOMO KABLA KINA KAYUMBA HAWAJACHOKA, NCHI HII HAITAKALIKA. Majaji wawili Kisanga Nyarari wote kwenye tume zao zilizowafikia wananchi zilipendekeza mabadiliko ya katiba sasa sijui unazungumzia wananchi gani tena Willy,
Nawasilisha
 
Kuna watu wanajifanya wagumu kuelewa, wanajifanya kuwa Hamad ndo siku zote yupo sahihi. Ila juzi tuu walikuwa wanaita CUF chama cha kidini.
 
Hamad amegeuka kuwa mtu mwongo na mlaghai hasa kwa watu wenye uelewa mdogo kama hao waliolipokea hili kama ndiyo ukweli wenyewe. HAMAD KUSEMA KWAMBA WABUNGE 10 WA CHADEMA HAWAKUTOKA WAKATI WENZAO WALIPOTOKA, ALITOA KAULI HIYO MAKUSUDI AKIJUA KUTAKUWA NA WATU WENYE AKILI NYEMBAMBA AMBAO WATAONA AMEWALETEA HABARI MPYA. UKWELI NI KUWA HAMAD KUITOA HABARI HIYO NI UJINGA NA ULAGHAI WA HALI YA JUU KWA VILE WABUNGE HAO 10 AMBAO ANASEMA HAWAKUTOKA, WASINGEWEZA KUTOKA WAKATI HAWAKUINGIA UKUMBINI. Ametoa kauli hiyo makusudi kwa nia ya kupotosha watu wenye upeo mdogo kama hawa walioileta hii hapa wakiamini kauli aliyoitoa Hamad ilikuwa kama walivyoelewa wao.

Anayekupinga anaweza kuwa ni adui yako lakini mtu anayetumia hila na uwongo kuwadanganya watu ili tu kutaka kukubalika ni hatari sana. Tunashukuru sana kwa CUF kukosa uongozi wa kambi ya upinzani kwa sababu tumeweza kumwelewa vizuri Hamad, huyu ni hatari katika mabadiliko tunayoyataka kuliko CCM.
 
Lakini HR nadhani sio mtu makini katika kutoa matamshi... Hadithi aliyoitoa kuhusu mazungumzo yake na Ndesamburo kuwa Chadema ni wakatoliki na CUF waislamu haikupaswa kuongelewa kwenye jukwaa kama lile. Yaani hapo aliharibu pande zote mbili. Ni maneno usiyotegemea kutoka kwa viongozi makini, isipokuwa tu kwa wale wasioweza kuzuia hisia zao.

Hamad Rashid ni kama alikuwa akifanya jitihada kuwa Chadema ionekane ni Chama cha watu fulani tu. Tena akajaribu kuwagawa wakristo vipandevipande kwa kusema kuwa alimwambia Ndesa kuwa Chadema ni chama cha wakatoliki.
Ni jealous fulani hivi kwani CUF wanaona Chadema imechukua nafasi yao, hivyo wanatafuta jinsi ya kui-discredit Chadema.

Chadema ni chama cha watu wote wanaotaka mabadiliko, bila kujali jinsia, kabila, dini, rangi, wala chama (yes, wala uanachama wa Chama).

Amejiita kuwa ni kiongozi mkongwe, lakini alikuwa mwepesi kukimbilia kwenye issue za udini, akijifanya anaukemea, kumbe anatumia style ya Kikwete kuufanya ndio mjadala.
Viongozi wanaojaribu kutupeleka kwenye udini hawafai.

Je ni bora niwe na kiongozi wa dini yangu (jambo ambalo halinisadii chochote) mwenye sera za ukandamizi? (mfano Elimu na Afya vitalipiwa na wananchi moja kwa moja) au niwe na kiongozi ambaye ni tofauti na mimi kwa dioni, kabila, chama, rangi au jinsia ambaye atakuwa na sera zinazonufaisha wananchi wengi? (mfano wananchi hawatalipa kupata huduma za Elimu na Afya)
Bora nimchague huyu wa pili, awe dini za jadi au baniani.
 
Duu. mengine tutajadili madudu. Mbona hakuwataja. Ukijadili ya zuzu nawe utakuwa zuzu.
 
Back
Top Bottom