Kumbe Helicopter ya CUF huko Igunga, imetolewa na CCM!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,467
113,567
Wanabodi,

Kwa jinsi nilivyo mkereketwa wa demokrasia ya kweli, nilitakiwa niwepo Igunga kushuhudia ama historia mpya ya ukombozi wa Tanzania ikijiandika, ama historia ile ile ya ukandamizwaji na uminywaji wa demokrasia ikijirudia, lakini kwa sababu zilizo nje ya uwezo wao, nimejikuta ndio kwanza nimelazimika kuwa eneo la Kirua Vunjo, huko Moshi Vijijini kwa tukio fulani.

Ni tukiwa tumekaa huku mgombani, sikutegemea uchaguzi wa Igunga ni main topic mpaka huku!. Ndipo siri za CCM zikaanza kuvuja!. Imeelezwa kuwa CCM inaihofia sana Chadema lakini haiihofi kabisa CUF. Pia adui mkuu wa CUF kwenye uchaguzi wa Igunga ni Chadema na sio CCM.
Kufuatia hilo, CCM imeamua kutumia ule mtindo wa 'Adui wa adui yako ni rafiki yako', hivyo wamejoin forces kwa siri against a common enemy Chadema!.

Mtoa habari huyu ndio akatoa siri kuwa hata ile helcopter ya CUF kule Igunga, imetolewa na CCM ili kuzipunguza kura za Chadema!. Kwa maneno mengine, CCM imeshagundua imepoteza mvuto na Chadema ndicho kinachong'ara, hivyo ili CCM ishinde nilazima ipige kampeni ya nguvu kwa CUF ili kuzi split kura za upinzani na yeyenywe kupeta kwa ushindi kiduchu!.

CUF kwa kukubali kusaidiwa na CCM, imeitumia ile kauli ya ' Baniani mbaya, kiatu chake dawa', kwa kuamini usaidizi huo wa CCM ni ili kukisaidia kushinda!. CUF kilitakiwa kutumia ' I fear the Greeks, especialy when they bring gifts!'.

Kama tetesi hii ni kweli, then ushindi wa CCM huko Igunga ni wazi, lakini ikitokea ikashindwa uchaguzi huu, basi CCM ndio basi tena, itakuwa ni ' La kuvunda hali hitaji ubani'!, safari ya kuelekea kaburini ndio itakuwa imeanza rasmi!

Naomba kuwasilisha

Pasco

Angalizo: Pasco wa jf sio mwanachama wala mshabiki wa chama chochote cha siasa na kwa vile hizi ni tetesi, sitarajii kuulizwa source, ukweli wa tetesi hizi utajihirika baada ya matokeo, maana watu lazima watashikana mashati!.
 
Habari yeyote ile huanzia na tetesi,huo ndio ukweli wenyewe ingawa hatuwezi kuuthibitisha
Hatuna haja ya kutafuta source
 
Wala hainishangazi kwa kuwa CCM na CUF wanakaa pamoja kwenye vikao vya serikali, maana wote ni viongozi wa serikali. Sasa tulitegemea wapingane nini ilhali wanatekeleza sera moja ilani moja katika serikali moja. Chama cha upinzani tannzania kwa sasa ni chadema na DP tu. hawa wengine wote ni waganga njaa tu. Na kwa utaratibu huu, hii nchi haitakaa iondokane na umasikini.
 
Wanabodi,

Kwa jinsi nilivyo mkereketwa wa demokrasia ya kweli, nilitakiwa niwepo Igunga kushuhudia ama historia mpya ya ukombozi wa Tanzania ikijiandika, ama historia ile ile ya ukandamizwaji na uminywaji wa demokrasia ikijirudia, lakini kwa sababu zilizo nje ya uwezo wao, nimejikuta ndio kwanza nimelazimika kuwa eneo la Kirua Vunjo, huko Moshi Vijijini kwa tukio fulani.

Ni tukiwa tumekaa huku mgombani, sikutegemea uchaguzi wa Igunga ni main topic mpaka huku!. Ndipo siri za CCM zikaanza kuvuja!. Imeelezwa kuwa CCM inaihofia sana Chadema lakini haiihofi kabisa CUF. Pia adui mkuu wa CUF kwenye uchaguzi wa Igunga ni Chadema na sio CCM.
Kufuatia hilo, CCM imeamua kutumia ule mtindo wa 'Adui wa adui yako ni rafiki yako', hivyo wamejoin forces kwa siri against a common enemy Chadema!.

Mtoa habari huyu ndio akatoa siri kuwa hata ile helcopter ya CUF kule Igunga, imetolewa na CCM ili kuzipunguza kura za Chadema!. Kwa maneno mengine, CCM imeshagundua imepoteza mvuto na Chadema ndicho kinachong'ara, hivyo ili CCM ishinde nilazima ipige kampeni ya nguvu kwa CUF ili kuzi split kura za upinzani na yeyenywe kupeta kwa ushindi kiduchu!.

CUF kwa kukubali kusaidiwa na CCM, imeitumia ile kauli ya ' Baniani mbaya, kiatu chake dawa', kwa kuamini usaidizi huo wa CCM ni ili kukisaidia kushinda!. CUF kilitakiwa kutumia ' I fear the Greeks, especialy when they bring gifts!'.

Kama tetesi hii ni kweli, then ushindi wa CCM huko Igunga ni wazi, lakini ikitokea ikashindwa uchaguzi huu, basi CCM ndio basi tena, itakuwa ni ' La kuvunda hali hitaji ubani'!, safari ya kuelekea kaburini ndio itakuwa imeanza rasmi!

Naomba kuwasilisha

Pasco

Angalizo: Kwa vile hizi ni tetesi, sitarajii kuulizwa source, ukweli wa tetesi hizi utajihirika baada ya matokeo, maana watu lazima watashikana mashati!.

Pasco ahasnte kwa tetesi na waswahili walisema lisemwalo...
Lakini hata kama ccm itashinda ... safari ya kaburini ni lazima. CCM ya leo imechoka, inatumia rafu na ulaghai kupata kura. Usalama wa taifa, wasanii wa sanaa, polisi, wakuu wa wilaya na mikoa, fujo, ....hvi vyote vina uhusiano gani na kampeni? Imejaribu kurudia hata vikokwe vilivyostaafu siasa kuitetea lakini wapi....
Ni wazi hizi ni siku za mwisha za CCM.
 
Duh! Pasco, kama habari hii ni ya kweli it is scary then!!!!!!. CCM Inachoshindwa kukielewa ni kwamba Igunga si mwisho wa chaguzi ndogo, siri hii ikiwa proved kuwa kweli basi ndio kaburi la CUF.
 
Habari yeyote ile huanzia na tetesi,huo ndio ukweli wenyewe ingawa hatuwezi kuuthibitisha
Hatuna haja ya kutafuta source
makwimoge, sio kweli kuwa habari yoyote huanzia na tetesi, bali habari zenye lengo la kuuficha ukweli ndipo siri huvuja kama tetesi.
 
Ha! Ha! Ha! Huko ni kujiliwaza na kujifariji kwa CDM baada ya kuona mambo magumu Igunga.
Hivi tujiulize Helcopter kukodi ni kiasi gani ambacho CUF watashindwa kugharamia kulipia hiyo Helcopter! CUF wanapata Ruzuku Milioni 110 kwa mwezi, wamejenga Jengo lao wenyewe, CDM bado wanapanga pale Uswahilini Manyanya mtaa wa Ufipa Kinandoni.

Sasa Mkuu Pasco, upo maeneo ya Kirua, Vunjo Moshi Vijijini unategemea, huko utapata habari njema kwa CUF.
Kingine mbona hizo Helcopter zipo pale Nakuru Kenya wanakodisha kama Tax tu, CCM wamewanunulia CUF Helcopter au wamewakodia?
 
Pasco ahasnte kwa tetesi na waswahili walisema lisemwalo...
Lakini hata kama ccm itashinda ... safari ya kaburini ni lazima. CCM ya leo imechoka, inatumia rafu na ulaghai kupata kura. Usalama wa taifa, wasanii wa sanaa, polisi, wakuu wa wilaya na mikoa, fujo, ....hvi vyote vina uhusiano gani na kampeni? Imejaribu kurudia hata vikokwe vilivyostaafu siasa kuitetea lakini wapi....
Ni wazi hizi ni siku za mwisha za CCM.
Mimo naona tetesi hizi zina ukweli, maana CUF hawaaminiki kabisa! Namuonea huruma sana Mtatiro kwa jinsi anavyohangaika bila kujua anapoteza muda wake! Tuombe Mungu mshindi halali apatikane ili kunusuru vurugu.
 
CCM ilizaliwa kwa mbwembwe,ikakuwa kwa maringo na sasa inazeeka na hasira......ccm imeshajifia bado kuzikwa tu.
Mtu yeyote" hasa vijana"....ukikuta anaisapoti ccm,basi ujue huyo mtu akili zake ziko makalioni au ana masilahi kupitia ccm.
 
Na bado CDM mtaendelea kulialia huku mkitafuta sababu!
Kwani Helcopter ndio inapiga kura Igunga, nyie si mnasema mnakubalika Igunga nzima mbona mnalalamikia Helcopter ya CUF hizi ni sababu za kitoto kabisa
 
Ha! Ha! Ha! Huko ni kujiliwaza na kujifariji kwa CDM baada ya kuona mambo magumu Igunga.
Hivi tujiulize Helcopter kukodi ni kiasi gani ambacho CUF watashindwa kugharamia kulipia hiyo Helcopter! CUF wanapata Ruzuku Milioni 110 kwa mwezi, wamejenga Jengo lao wenyewe, CDM bado wanapanga pale Uswahilini Manyanya mtaa wa Ufipa Kinandoni.

Sasa Mkuu Pasco, upo maeneo ya Kirua, Vunjo Moshi Vijijini unategemea, huko utapata habari njema kwa CUF.
Kingine mbona hizo Helcopter zipo pale Nakuru Kenya wanakodisha kama Tax tu, CCM wamewanunulia CUF Helcopter au wamewakodia?
Mke ni mke tuu hata kama ana mshahara kama wako kumnunulia gauni sio jambo geni. Sasa CCM kuikodia CUF huo usafiri sio ajabu maana ni mtu na mpenziwe.
 
Duh! Pasco, kama habari hii ni ya kweli it is scary then!!!!!!. CCM Inachoshindwa kukielewa ni kwamba Igunga si mwisho wa chaguzi ndogo, siri hii ikiwa proved kuwa kweli basi ndio kaburi la CUF.
Baada ya CUF kusaini muafaka na kuundwa kwa SUK, niliandika kuwa huu ndio mwanzo wa mwisho wa CUF haswa baada ya kugundua kumbe wale mawaziri wa CUF ndani ya SUK wanatekeleza sera za CCM!.
 
Mke ni mke tuu hata kama ana mshahara kama wako kumnunulia gauni sio jambo geni. Sasa CCM kuikodia CUF huo usafiri sio ajabu maana ni mtu na mpenziwe.

Mbona siku hizi Wanawake wanawanunulia wanaume vitu!
Nauliza tu Helcopter nao inapiga kura?
 
aah jaman j2 klak2 ktakuwa waz. Kama helkopta o sera ndo zna determine ushnd 2tajua kwan 'ukubwa wa pua cowng wa makamac' mwny kchwa na aelewe

kama unatoa chemsha bongo vile! achana na vifupisho, hueleweki kabisaaaa!
 
tetesi hii naipa 70% ya ukweli, kwani CCM walikuwa na mpango wa kutumia helkopta mbili, ila sasa wanatumia moja, hiyo ya pili imeenda wapi?, au imepatiwa matumizi mengine kwa mamaa? Mama CCM (aka CUF) alikuwa na mpango wa kutumia helkopta,lakini ilichelewa kwa siku moja,je mpango ulikuwa bado unasukwa ndo ikasababisha kuchelewa kufika?
 
Back
Top Bottom