Bill
JF-Expert Member
- Oct 5, 2007
- 8,277
- 8,492
Katika kile kinachoonekana ni kujipanga dhidi ya uwezekano wowote wa kuugua ghafla au kupata ajali kwa viongozi au makada wake, msafara wa kampeni za mgombea huyo umekuwa ukiongozana na magari maalum ya kubebea wagonjwa mahututi (ambulance).
Mbali na kuanguka jukwaani jijini Dar es Salaam, baadhi ya watu waliohudhuria mkutano wake wa kampeni katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza na waliofuatilia mkutano huo kupitia kituo cha televisheni cha ‘Star Tv', walisema bado Rais Kikwete alionekana mdhoofu na aliyepoteza uchangamfu wake wa kawaida licha ya kujitahidi kuhutubia bila kufikwa na msukosuko mwingine wa kiafya.
Kumbukumbu zinaonyesha kuwa msukosuko wa kiafya wa Jumamosi ni wa nne kumfika hadharani Rais Kikwete.
Akiwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Kikwete aliwahi kuzidiwa ghafla mwaka 1997 katika uwanja wa ndege wa Brussels nchini Ubelgiji akiwa njiani kuelekea nchini Cuba hali iliyosababisha alazwe kwa saa kadhaa kabla ya kuruhusiwa kuendelea na safari.
Mwaka 2005 siku moja kabla ya uchaguzi mkuu, alizidiwa ghafla na kuanguka jukwaani katika viwanja hivyo hivyo vya Jangwani.
Baada ya kupata matibabu ya awali, alizungumza na vyombo vya habari nyumbani kwake na kuwaeleza kuwa kilichomfanya aanguke ni uchovu wa kampeni na hasa kwa kuwa siku hiyo alikuwa amefunga.
Akihutubia umati wa waumini wa Kanisa la Africa Inland (AIC) jijini Mwanza Oktoba 4 mwaka jana, Rais Kikwete aliishiwa nguvu hali iliyomlazimu daktari wake, Peter Mfisi, kutoa ufafanuzi kwa vyombo vya habari kwa kusema Rais Kikwete alikuwa hana tatizo lolote la kiafya ila aliishiwa nguvu kwa uchovu.
".......uchaguzi ule alidondoka kwa sababu ya uchovu sasa kuanguka hivi jamani kunashtusha maana safari hii ndio alikuwa anazindua hizo kampeni kwa hiyo suala la uchovu hapo halipo. Kuna kitu wanatuficha......wanajua wenyewe, ndio mambo ya wakubwa hayo lakini tutakuja kujua tu, dunia haina siri bwana, lakini namtakia afya njema", alisema mwanaharakati mmoja kwa sharti la kutotajwa jina lake.
Hata hivyo, alipoulizwa na mhariri wa chombo kimoja cha habari kuwa chama hicho kimejipangaaje kumpunguzia uchovu Rais Kikwete katika kampeni za mwaka huu, Kinana alisema watatumia usafiri wa helikopta kumnadi mgombea huyo ili kumpunguzia umbali mrefu wa kusafiri kwa njia ya barabara.
Mbali ya kupunguziwa umbali wa kusafiri kwa njia ya barabara, Kikwete atapata muda wa kupumzika wa siku 16 katika kipindi chote cha siku 68 za kampeni na hivyo kumfanya kuwa katika mchakato huo kwa siku 52.
Uamuzi huo utamwezesha mgombea huyo wa urais wa CCM kupunguza umbali wa kusafiri kwa njia ya barabara kwa urefu wa kilomita 58,000 ikilinganishwa na ilivyokuwa mwaka 2005. Kumbukumbu zinaonyesha kuwa wakati wa kampeni za mwaka 2005 Kikwete alisafiri kwa njia ya barabara umbali wa kilomota 96,000. Alisema katika kampeni za mwaka huu mgombea huyo atasafiri kwa njia ya barabara kwa umbali wa kilomita 38,000 tu.
Ili kuhakikisha Rais Kikwete anapata muda mrefu wa kumpumzika na kumpunguzia uchovu, CCM imepunguza muda wa kuzungumza kwa mgombea huyo katika mikutano yake ya kampeni. Hali hiyo imeonekana mjini Mwanza na maeneo mengine alikopita ambako alitumia muda usiozidi dakika 30 kuomba kura kwa wananchi.
SOURCE: Tanzania Daima - 25/08/2010
Mytake: JK kapunguziwa uchovu kwa kupewa usafiri wa anga na kupunguziwa muda wa kuhutubia, mbona ambulance tena? Si JK kaacha kufunga ambalo ndio ilikuwa kiini cha kuishiwa nguvu/sukari! Mbona ambulance tena na kupunguziwa muda wa kuhutubia???? Yangu masikio na Macho.....
Mbali na kuanguka jukwaani jijini Dar es Salaam, baadhi ya watu waliohudhuria mkutano wake wa kampeni katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza na waliofuatilia mkutano huo kupitia kituo cha televisheni cha ‘Star Tv', walisema bado Rais Kikwete alionekana mdhoofu na aliyepoteza uchangamfu wake wa kawaida licha ya kujitahidi kuhutubia bila kufikwa na msukosuko mwingine wa kiafya.
Kumbukumbu zinaonyesha kuwa msukosuko wa kiafya wa Jumamosi ni wa nne kumfika hadharani Rais Kikwete.
Akiwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Kikwete aliwahi kuzidiwa ghafla mwaka 1997 katika uwanja wa ndege wa Brussels nchini Ubelgiji akiwa njiani kuelekea nchini Cuba hali iliyosababisha alazwe kwa saa kadhaa kabla ya kuruhusiwa kuendelea na safari.
Mwaka 2005 siku moja kabla ya uchaguzi mkuu, alizidiwa ghafla na kuanguka jukwaani katika viwanja hivyo hivyo vya Jangwani.
Baada ya kupata matibabu ya awali, alizungumza na vyombo vya habari nyumbani kwake na kuwaeleza kuwa kilichomfanya aanguke ni uchovu wa kampeni na hasa kwa kuwa siku hiyo alikuwa amefunga.
Akihutubia umati wa waumini wa Kanisa la Africa Inland (AIC) jijini Mwanza Oktoba 4 mwaka jana, Rais Kikwete aliishiwa nguvu hali iliyomlazimu daktari wake, Peter Mfisi, kutoa ufafanuzi kwa vyombo vya habari kwa kusema Rais Kikwete alikuwa hana tatizo lolote la kiafya ila aliishiwa nguvu kwa uchovu.
".......uchaguzi ule alidondoka kwa sababu ya uchovu sasa kuanguka hivi jamani kunashtusha maana safari hii ndio alikuwa anazindua hizo kampeni kwa hiyo suala la uchovu hapo halipo. Kuna kitu wanatuficha......wanajua wenyewe, ndio mambo ya wakubwa hayo lakini tutakuja kujua tu, dunia haina siri bwana, lakini namtakia afya njema", alisema mwanaharakati mmoja kwa sharti la kutotajwa jina lake.
Hata hivyo, alipoulizwa na mhariri wa chombo kimoja cha habari kuwa chama hicho kimejipangaaje kumpunguzia uchovu Rais Kikwete katika kampeni za mwaka huu, Kinana alisema watatumia usafiri wa helikopta kumnadi mgombea huyo ili kumpunguzia umbali mrefu wa kusafiri kwa njia ya barabara.
Mbali ya kupunguziwa umbali wa kusafiri kwa njia ya barabara, Kikwete atapata muda wa kupumzika wa siku 16 katika kipindi chote cha siku 68 za kampeni na hivyo kumfanya kuwa katika mchakato huo kwa siku 52.
Uamuzi huo utamwezesha mgombea huyo wa urais wa CCM kupunguza umbali wa kusafiri kwa njia ya barabara kwa urefu wa kilomita 58,000 ikilinganishwa na ilivyokuwa mwaka 2005. Kumbukumbu zinaonyesha kuwa wakati wa kampeni za mwaka 2005 Kikwete alisafiri kwa njia ya barabara umbali wa kilomota 96,000. Alisema katika kampeni za mwaka huu mgombea huyo atasafiri kwa njia ya barabara kwa umbali wa kilomita 38,000 tu.
Ili kuhakikisha Rais Kikwete anapata muda mrefu wa kumpumzika na kumpunguzia uchovu, CCM imepunguza muda wa kuzungumza kwa mgombea huyo katika mikutano yake ya kampeni. Hali hiyo imeonekana mjini Mwanza na maeneo mengine alikopita ambako alitumia muda usiozidi dakika 30 kuomba kura kwa wananchi.
Ambulance ya Hospitali ya Rufaa Bugando ikiwa kwenye msafara wa mgombea wa CCM, Rais Jakaya Kikwete. Sina uhakika kama imelipiwa na chama au itakuwa inasaidia misafara ya wagombea wa vyama vyote.Picha na Katulanda
SOURCE: Tanzania Daima - 25/08/2010
Mytake: JK kapunguziwa uchovu kwa kupewa usafiri wa anga na kupunguziwa muda wa kuhutubia, mbona ambulance tena? Si JK kaacha kufunga ambalo ndio ilikuwa kiini cha kuishiwa nguvu/sukari! Mbona ambulance tena na kupunguziwa muda wa kuhutubia???? Yangu masikio na Macho.....