NdasheneMbandu
JF-Expert Member
- Jan 2, 2012
- 940
- 308
Ndugu zangu,
Watanzania tumelogwa au ndiyo ule wimbo wa magamba wa amani na utulivu. Nchi nyingi duniani hivi sasa wananchi wanaandamana kupinga maamuzi ya serikali zao kuhusu masuala mbalimbali ya kiuchumi, kisiasa na kijamii lakini watanzania tupo kimyaaaaaaa kana kwamba serikali yetu inafanya vema. Mfano mzuri ni maandamano yanayoendelea nchini Uganda na Nigeria mpaka serikali zao zinaelekea kusalimu amri. Sisi hapa kwetu juzi tu EWURA wamepandisha umeme kwa wastani wa asilimia 40.29 lakini sisi tunaishia kulalamika kwenye vijiwe vyetu tu mitaani. Ifike mahali watanzania tujifunze kwa wenzetu kuwa na ujasiri. Serikali ya ccm imefanya maamuzi ya hasara mengi na makubwa kwenye mikataba ya umeme matokeo yake ni kuendelea kubebeshwa mizigo ya bei kila baada ya muda mfupi. Pamoja na hali hiyo, bado tupo kimya. Hatusikii chama chotechote kitaandaa maandamano ya kupinga ongezeko la bei. Shime watanzania tufanye maamuzi. Tutaangamizwa na maamuzi haya ya kifisadi.
Watanzania tumelogwa au ndiyo ule wimbo wa magamba wa amani na utulivu. Nchi nyingi duniani hivi sasa wananchi wanaandamana kupinga maamuzi ya serikali zao kuhusu masuala mbalimbali ya kiuchumi, kisiasa na kijamii lakini watanzania tupo kimyaaaaaaa kana kwamba serikali yetu inafanya vema. Mfano mzuri ni maandamano yanayoendelea nchini Uganda na Nigeria mpaka serikali zao zinaelekea kusalimu amri. Sisi hapa kwetu juzi tu EWURA wamepandisha umeme kwa wastani wa asilimia 40.29 lakini sisi tunaishia kulalamika kwenye vijiwe vyetu tu mitaani. Ifike mahali watanzania tujifunze kwa wenzetu kuwa na ujasiri. Serikali ya ccm imefanya maamuzi ya hasara mengi na makubwa kwenye mikataba ya umeme matokeo yake ni kuendelea kubebeshwa mizigo ya bei kila baada ya muda mfupi. Pamoja na hali hiyo, bado tupo kimya. Hatusikii chama chotechote kitaandaa maandamano ya kupinga ongezeko la bei. Shime watanzania tufanye maamuzi. Tutaangamizwa na maamuzi haya ya kifisadi.