Kulikoni Rai, Habari Leo na Mtanzania

Geza Ulole

JF-Expert Member
Oct 31, 2009
59,146
79,300
Wajameni kama ni wafuatiliaji wa mrengo wa haya magazeti mtagundua kubadilika kwa ghafla mtazamo wao kuhusu hali halisi ya Ufisadi katika CCM. Kulikoni? wadadisi wa mambo wanasema Matokeo ya kesi ya Dowans ndiyo inasababisha haya; katika kupumbaza Watanzania aka Wadanganyika magazeti haya yameanza hata kujinyooshea vidole yenyewe katika kile kinachoitwa kuchanganya watu katika agenda ya siku au wataalam wanaita (story/agenda of the day)! Ningependa kama wangejikita zaidi katika suala la Hukumu ya Dowans na sio janja iliyoratibiwa katika kupoteza mawazo ya Wadanganyika na fujo za uchaguzi wa Mameya zinaofanywa kinguvu kwa kutumia jeshi! Tunaona hata Lowassa anakaripiwa ilhali tunajua nguvu yake na uhusiano wake wa Dowans huu ni usanii tunachezewa kwa remote control sasa! Amkeni nani mmiliki wa Dowans?
 
ndo nimetua jf baada ya kufungiwa kwa wiki 2, kisa nilimwita mtu shetani, mtu mkubwa sana mwenye maamuzi yote ya nchi, lakini kamkabidhi mtu mwingine afanye badala yake. hatimaye kila mtu anateseka kwa mtu huyu kukodisha mamlaka yake kwa mafisadi wasiozidi watatu. nitaendelea kuandika na najua sasa nitafukuzwa rasmi hapa jamvini
 
ndo nimetua jf baada ya kufungiwa kwa wiki 2, kisa nilimwita mtu shetani, mtu mkubwa sana mwenye maamuzi yote ya nchi, lakini kamkabidhi mtu mwingine afanye badala yake. hatimaye kila mtu anateseka kwa mtu huyu kukodisha mamlaka yake kwa mafisadi wasiozidi watatu. nitaendelea kuandika na najua sasa nitafukuzwa rasmi hapa jamvini

sijakuelewa mkuu..... Connection ya haya magazeti na wewe kumuita mtu shetani na kifungo chako ni nini hasa????
 
Nashukuru na wewe umeliona ili. Mimi juzi nilitoa thread juu ya jambo hilo lakini huwa sijui inakuwaje thread zangu hazimalizi dakika, uwa zimekwisha ondolewa. Kuhusu haya mabadiliko ya ghafla ya hayo magazeti, kwa maoni yangu uenda kumetokana na kupoteza kwa wingi wasomaji wake walioanza kuchoshwa na propaganda za magazeti hayo. Hali hiyo uenda imeyaathiri kiuchumi,na vile vile kuyafanya yasiwe ya maana. Nahisi kinachofanyika sasa ni kile katika lugha ya kimasoko, kinachoitwa "repositioning." Hii ina maana, magezeti hayo hivi sasa yanajaribu kujenga hisia miongoni mwa watanzania kuwa yako pamoja nao katika masuala ya msingi yanayokuna nyoyo zao. Yakishafanikiwa kwa hilo, ndipo yataweza kupandikiza ajenda yaliyonayo.
 
Nashukuru na wewe umeliona ili. Mimi juzi nilitoa thread juu ya jambo hilo lakini huwa sijui inakuwaje thread zangu hazimalizi dakika, uwa zimekwisha ondolewa. Kuhusu haya mabadiliko ya ghafla ya hayo magazeti, kwa maoni yangu uenda kumetokana na kupoteza kwa wingi wasomaji wake walioanza kuchoshwa na propaganda za magazeti hayo. Hali hiyo uenda imeyaathiri kiuchumi,na vile vile kuyafanya yasiwe ya maana. Nahisi kinachofanyika sasa ni kile katika lugha ya kimasoko, kinachoitwa "repositioning." Hii ina maana, magezeti hayo hivi sasa yanajaribu kujenga hisia miongoni mwa watanzania kuwa yako pamoja nao katika masuala ya msingi yanayokuna nyoyo zao. Yakishafanikiwa kwa hilo, ndipo yataweza kupandikiza ajenda yaliyonayo.
mbona hayagusii "the real story" about Dowans? huoni ajabu katika repositioning huko?
 
mi pia nilipigwa mshangao na haya magazeti , nikajiuliza NINI KIMETOKEA HADI YAKABADIRIKA HIVI, ok all in all NGOJA TUSUBIRI , labla wanalengo FULANI HIVI
 
Back
Top Bottom