Kulikoni Mzee wetu Aboud Jumbe

Brooklyn

JF-Expert Member
Mar 17, 2009
1,459
284
Ndugu wadau naomba kuelimishwa kidogo kuhusu mzee Aboud Jumbe. Naambiwa aliwahi kuwa Rais wa Zanzibar na Makamu wa pili wa Rais wa JMT. Ninachoshangaa ni kwamba sijawahi kumuona hata siku moja kwenye dhifa za kitaifa au matukio mengine ya kitaifa kama vile sherehe, misiba ama hata vikao vya NEC Dodoma.

Nimezoea kuona viongozi wengi wastaafu wakihudhuria lakini yeye sijawahi kumuona hata siku moja (hata Salmin naye amekuwa haonekani kabisa).

Naombeni wajuzi wa mambo tufahamishenbi kulikoni...naambiwa anaishi hapo kigamboni tu!
 
Yule mwisho wake kama kiongozi ulikuwa mbaya sana, kwahiyo ameachwa ajizeekee taratibu huko shamba!
Kumbuka alisimamiwa na kulazimishwa ajiuzulu.
 
Alitaka kuua muungano na Nyerere akampindua kumuweka jamaa yake ili muungano uendelee baada yapo akapumzishwa Kigamboni na kutelekezwa huko maskini
 
WOULD anyone knowing about this Jumbe saga tell us please,cause it seems history has cast him aside
 
Lemme shooting off the hip, according to credible sources.

Jumbe alitaka kuvunja muungano, wakati huo Seif Sharif Hamad Waziri kiongozi Zanzibar. Hamad aliposikia habari hizi akamtonya Nyerere, wakamtumia katibu muhtasi wa Jumbe kuiba makaratasi ambayo Jumbe angeyatumia kuuvunja muungano, yakiwamo yale ya kuupitia muungano kwa review kila miaka 10. Na hati nyingine za muungano ambazo Wazanzibari mpaka leo wanazidai. Inasemekana hizi hati zilipochukuliwa na Nyerere hazikurudishwa Zanzibar mpaka Nyerere alipofariki. Wengine wanasema hii ni siri kali kati ya Nyerere na Hamad, na pengine katibu muhtasi huyu ambaye anaonekana amenyamazishwa (na labda hakujua hata umuhimu wa makaratasi haya) sijui kama yuko hai bado .

Ndiyo maana mpaka Nyerere anafariki, na hata baada ya Seif Sharif Hamad kuingia upinzani. Nyerere na Hamad walikuwa wanateta, na kuna mengine Nyerere kaenda nayo kaburini na Hamad mpaka leo hataki kusema alipokuwa anateta na Nyerere walikuwa wanaongea nini. Wametoka mbali.

Nyerere alipopata vielelezo vyote akamlazimisha Jumbe ajiuzulu, kukatangazwa "mchafuko wa hali ya hewa ya kisiasa" Zanzibar. Nyerere akamchagua Spika wa baraza la wawakilishi Zanzibar, balozi Ali Hassan Mwinyi (no relation), kuwa "rais wa muda" wa Zanzibar na hivyo makamu wa rais. Watu wa usalama kama kina Mashiba wakatuambia "vijana huyu Mwinyi ndiye atakuwa rais baada ya Nyerere". Tukaona kama utani vile.

Baadaye marehemu Maneti (pamoja na wengine wengi) akaimba "Ali Mwinyi, Ali Mwinyi, Ndiyo, Ndiyo, Ndiyo". The rest is much documented in Tanzanian history.

Hivi ndivyo Jumbe alivyoanguka na Mwinyi kupanda.

Makamu mwingine wa rais aliyekuwa anaandaliwa kwa urais alikuwa daktari wa mifugo Omar Ali Juma, yeye anguko lake la umauti lilitokana na kuchanganya Viagra na kahawa- a deadly combination-, kitu ambacho kama mtaalamu wa mambo ya baiolojia angetakiwa kukijua. Mkapa hakupenda Kikwete awe rais na alikuwa anamuandaa Dr. Omar kuchukua urais, kwa mujibu wa watu wa familia ya Mkapa waliokuwa wanaishi naye Ikulu na Sea View. Ila Viagra ambayo Makamu wa rais aliiongezea kahawa - a deadly combination- ikakatili ndoto hizi na kufanya nyota ya Kikwete iendelee kung'ara.

I don't know which is worse, a Kikwete presidency or a Juma presidency.
 
Aboud Jumbe Mwinyi alikuwa Rais wa pili wa Zanzibar toka mwaka 1972 hadi mwaka 1982 alipotimuliwa na CCM baada ya kuchafuka kwa hali ya hewa.Nasikia siku hizi anaishi mji mwema kigamboni Dar es Salaam akisubiri siku zake ziishe hapa dunia.
 
Lemme shooting off the hip, according to credible sources.

Jumbe alitaka kuvunja muungano, wakati huo Seif Sharif Hamad Waziri kiongozi Zanzibar. Hamad aliposikia habari hizi akamtonya Nyerere, wakamtumia katibu muhtasi wa Jumbe kuiba makaratasi ambayo Jumbe angeyatumia kuuvunja muungano, yakiwamo yale ya kuupitia muungano kwa review kila miaka 10. Na hati nyingine za muungano ambazo Wazanzibari mpaka leo wanazidai. Inasemekana hizi hati zilipochukuliwa na Nyerere hazikurudishwa Zanzibar mpaka Nyerere alipofariki. Wengine wanasema hii ni siri kali kati ya Nyerere na Hamad, na pengine katibu muhtasi huyu ambaye anaonekana amenyamazishwa (na labda hakujua hata umuhimu wa makaratasi haya) sijui kama yuko hai bado .

Ndiyo maana mpaka Nyerere anafariki, na hata baada ya Seif Sharif Hamad kuingia upinzani. Nyerere na Hamad walikuwa wanateta, na kuna mengine Nyerere kaenda nayo kaburini na Hamad mpaka leo hataki kusema alipokuwa anateta na Nyerere walikuwa wanaongea nini. Wametoka mbali.

Nyerere alipopata vielelezo vyote akamlazimisha Jumbe ajiuzulu, kukatangazwa "mchafuko wa hali ya hewa ya kisiasa" Zanzibar. Nyerere akamchagua Spika wa baraza la wawakilishi Zanzibar, balozi Ali Hassan Mwinyi (no relation), kuwa "rais wa muda" wa Zanzibar na hivyo makamu wa rais. Watu wa usalama kama kina Mashiba wakatuambia "vijana huyu Mwinyi ndiye atakuwa rais baada ya Nyerere". Tukaona kama utani vile.

Baadaye marehemu Maneti (pamoja na wengine wengi) akaimba "Ali Mwinyi, Ali Mwinyi, Ndiyo, Ndiyo, Ndiyo". The rest is much documented in Tanzanian history.

Hivi ndivyo Jumbe alivyoanguka na Mwinyi kupanda.

Makamu mwingine wa rais aliyekuwa anaandaliwa kwa urais alikuwa daktari wa mifugo Omar Ali Juma, yeye anguko lake la umauti lilitokana na kuchanganya Viagra na kahawa- a deadly combination-, kitu ambacho kama mtaalamu wa mambo ya baiolojia angetakiwa kukijua. Mkapa hakupenda Kikwete awe rais na alikuwa anamuandaa Dr. Omar kuchukua urais, kwa mujibu wa watu wa familia ya Mkapa waliokuwa wanaishi naye Ikulu na Sea View. Ila Viagra ambayo Makamu wa rais aliiongezea kahawa - a deadly combination- ikakatili ndoto hizi na kufanya nyota ya Kikwete iendelee kung'ara.

I don't know which is worse, a Kikwete presidency or a Juma presidency.



mna uongo mwingi sana kuliko ukweli
 
Tupe basi ukweli unaoujua wewe. PS nimependa masimulizi ya Kiranga.


tushawahi kuzungmzia kuhusu Aboud Jumbe Legacy enzi zile za 2008 na nnakumbuka ww ulikuwepo jamvini labda tumuombe mod airejeshe ile thread nnadhani unakumbuka


tulimzunumza kwa marefu na mapana mazuri yake na mabaya yake
 
mna uongo mwingi sana kuliko ukweli

Ingekuwa vizuri ukatueleza ukweli unaoujua wewe na uongo uliouona hapa, maana hii ndiyo maana ya forum, kubadilishana ujuzi, lakini kama unasema tu huu ni uongo, bila ya kusema kwa nini huu ni uongo, na ukweli ni upi, huelimishi wala kusaidia.

Sanasana unaweza kusababisha unaowaita waongo kukusema weye ndiye muongo, na mazungumzo kugeuka kuwa malumbano yaso tija.

Tuambie uongo u wapi, na ukweli u wapi.
 
tushawahi kuzungmzia kuhusu Aboud Jumbe Legacy enzi zile za 2008 na nnakumbuka ww ulikuwepo jamvini labda tumuombe mod airejeshe ile thread nnadhani unakumbuka


tulimzunumza kwa marefu na mapana mazuri yake na mabaya yake

Mod akikwambia database ili collapse na rekodi zote zimepotea, tunahitaji kuchangia upya, utasemaje ?
 
..huyu Jumbe alikuwa anapinga Muungano, halafu leo hii hataki kurudi kwao Zanzibar. miaka yote ameendelea kujibanza Mjimwema, Kigamboni.

..anyway, inasemekana alitafuta Mwanasheria toka Ghana, akiitwa Kwah Swanzy, kumsaidia kuandaa kesi ya kikatiba dhidi ya serikali ya Muungano.

..inasemekana nyaraka za suala hilo zilichomolewa toka ktk ofisi ya Raisi wa Zanzibar, na kupelekwa kwa Juliasi.

..baada ya hapo sisi wananchi tulishtukizwa tu na habari toka makao makuu ya chama dodoma, kwenye kikao cha NEC, kwamba Mzee Jumbe amejiuzulu na nafasi yake imechukuliwa na Ali Hassan Mwinyi.

..inasemekana humo mwenye kikao cha NEC, vinara wa kutoka Zenj katika kumshambulia Alhaji Aboud Jumbe, alikuwa ni huyu Maalim Seif Sharrif Hamad.

..baada ya sakata hiyo, Maalim Seif Sharrif Hamad, aliteuliwa kuwa Waziri Kiongozi, akichukua nafasi ya Brig.Ramadhani Haji Faki.

..wanasiasa mbalimbali wa Zenj, mfano Col.Seif Bakari, waliingia ktk mkumbo mmoja na Aboud Jumbe, na kuwekwa kizuizini Bara.

..mambo yalitulia kidogo, lakini yakaja kuchafuka zaidi wakati Ali Hassan Mwinyi alipoteuliwa kumrithi Mwalimu Nyerere, na Sheikh Idiris Abdul Wakil kuteuliwa kugombea nafasi ya Uraisi wa Zanzibar.

NB:

..Sheikh Idiris Abdul Wakil alikuwa akiishi Ilala-Bungoni kabla ya kuteuliwa kuwa Raisi wa Zenj.

..ndiyo maana nasema hawa wa-Zenj dawa yao ni kuwatimua wote toka Bara warudi kwao wakaongee vizuri kuhusu kuvunja muungano.
 
..huyu Jumbe alikuwa anapinga Muungano, halafu leo hii hataki kurudi kwao Zanzibar. miaka yote ameendelea kujibanza Mjimwema, Kigamboni.

Mimi nilijua huyu mzee huenda ametangulia kwenye hukumu ya haki! Maana hasikiki kabisa kama mmojawapo wa viongozi waandamizi
 
..huyu Jumbe alikuwa anapinga Muungano, halafu leo hii hataki kurudi kwao Zanzibar. miaka yote ameendelea kujibanza Mjimwema, Kigamboni.

..anyway, inasemekana alitafuta Mwanasheria toka Ghana, akiitwa Kwah Swanzy, kumsaidia kuandaa kesi ya kikatiba dhidi ya serikali ya Muungano.

..inasemekana nyaraka za suala hilo zilichomolewa toka ktk ofisi ya Raisi wa Zanzibar, na kupelekwa kwa Juliasi.

..baada ya hapo sisi wananchi tulishtukizwa tu na habari toka makao makuu ya chama dodoma, kwenye kikao cha NEC, kwamba Mzee Jumbe amejiuzulu na nafasi yake imechukuliwa na Ali Hassan Mwinyi.

..inasemekana humo mwenye kikao cha NEC, vinara wa kutoka Zenj katika kumshambulia Alhaji Aboud Jumbe, alikuwa ni huyu Maalim Seif Sharrif Hamad.

..baada ya sakata hiyo, Maalim Seif Sharrif Hamad, aliteuliwa kuwa Waziri Kiongozi, akichukua nafasi ya Brig.Ramadhani Haji Faki.

..wanasiasa mbalimbali wa Zenj, mfano Col.Seif Bakari, waliingia ktk mkumbo mmoja na Aboud Jumbe, na kuwekwa kizuizini Bara.

..mambo yalitulia kidogo, lakini yakaja kuchafuka zaidi wakati Ali Hassan Mwinyi alipoteuliwa kumrithi Mwalimu Nyerere, na Sheikh Idiris Abdul Wakil kuteuliwa kugombea nafasi ya Uraisi wa Zanzibar.

NB:

..Sheikh Idiris Abdul Wakil alikuwa akiishi Ilala-Bungoni kabla ya kuteuliwa kuwa Raisi wa Zenj.

..ndiyo maana nasema hawa wa-Zenj dawa yao ni kuwatimua wote toka Bara warudi kwao wakaongee vizuri kuhusu kuvunja muungano.


nadhani hapa tunaweza kupata alau machache na kuna nyengine ambazo tulikuwa tukimzungumzia nyerere ukienda unaweza pata

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/3034-legacy-ya-mzee-aboud-jumbe-zanzibar.html


uongo wa mwanzo kusema Maalim Seif alikuwa Waziri kiongozi wakati waziri kiongozi alikuwa Ramadhan Haji Faki

kidogo kidogo tunajifunza
 
nadhani hapa tunaweza kupata alau machache na kuna nyengine ambazo tulikuwa tukimzungumzia nyerere ukienda unaweza pata

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/3034-legacy-ya-mzee-aboud-jumbe-zanzibar.html


uongo wa mwanzo kusema Maalim Seif alikuwa Waziri kiongozi wakati waziri kiongozi alikuwa Ramadhan Haji Faki

kidogo kidogo tunajifunza

I stand corrected, Hamad hakuwa Waziri Kiongozi wakati wa machafuko ya hali ya hewa Zanzibar. Rather, alizawadiwa Uwaziri Kiongozi kwa kazi nzuri ya kumfichua Jumbe.

Seif Sharif Hamad - Wikipedia, the free encyclopedia
 
..huyu Jumbe alikuwa anapinga Muungano, halafu leo hii hataki kurudi kwao Zanzibar. miaka yote ameendelea kujibanza Mjimwema, Kigamboni.

..anyway, inasemekana alitafuta Mwanasheria toka Ghana, akiitwa Kwah Swanzy, kumsaidia kuandaa kesi ya kikatiba dhidi ya serikali ya Muungano.

..inasemekana nyaraka za suala hilo zilichomolewa toka ktk ofisi ya Raisi wa Zanzibar, na kupelekwa kwa Juliasi.

..baada ya hapo sisi wananchi tulishtukizwa tu na habari toka makao makuu ya chama dodoma, kwenye kikao cha NEC, kwamba Mzee Jumbe amejiuzulu na nafasi yake imechukuliwa na Ali Hassan Mwinyi.

..inasemekana humo mwenye kikao cha NEC, vinara wa kutoka Zenj katika kumshambulia Alhaji Aboud Jumbe, alikuwa ni huyu Maalim Seif Sharrif Hamad.

..baada ya sakata hiyo, Maalim Seif Sharrif Hamad, aliteuliwa kuwa Waziri Kiongozi, akichukua nafasi ya Brig.Ramadhani Haji Faki.

..wanasiasa mbalimbali wa Zenj, mfano Col.Seif Bakari, waliingia ktk mkumbo mmoja na Aboud Jumbe, na kuwekwa kizuizini Bara.

..mambo yalitulia kidogo, lakini yakaja kuchafuka zaidi wakati Ali Hassan Mwinyi alipoteuliwa kumrithi Mwalimu Nyerere, na Sheikh Idiris Abdul Wakil kuteuliwa kugombea nafasi ya Uraisi wa Zanzibar.

NB:

..Sheikh Idiris Abdul Wakil alikuwa akiishi Ilala-Bungoni kabla ya kuteuliwa kuwa Raisi wa Zenj.

..ndiyo maana nasema hawa wa-Zenj dawa yao ni kuwatimua wote toka Bara warudi kwao wakaongee vizuri kuhusu kuvunja muungano.
Nilikuwa sijui kama nyerere alikuwa dikteta kiasi hiki. yaani alikuwa analotaka ndo linalokuwa. Hii ni aibu kwa mtawala ambaye kila kukicha anasifiwa. Alietaka awe rais ndo aliekuwa. Hakupenda kupingwa wala mtu kuwa na mawazo mbadala. Hii ni hatari kwani akiwa hata na maoni ambayo hayana tija kama ya muungano hamna wakumshauri. we do not need a leaders of such kind. KULIKUWA NA UBAYA GANI WA KUACHIA HOJA KAMA ILIKUWAPO KWA MFANO HII YA MUUNGANO KUJADILIWA NA KUWA NA RADHI YA JAMII ZOTE HUSIKA? AU KWENYE HUO MUUNGANO KUNA SIRI GANI? KWA NINI HAKUTAKA KUJADILIWA? MATOKEO YAKE NAONA WATU WANAMKEJELI TU MZEE JUMBE. SISHANGAI HUENDA HUYU MZEE ALIKUWA SAHIHI. This is a century shame!
 
I stand corrected, Hamad hakuwa Waziri Kiongozi wakati wa machafuko ya hali ya hewa Zanzibar. Rather, alizawadiwa Uwaziri Kiongozi kwa kazi nzuri ya kumfichua Jumbe.

Seif Sharif Hamad - Wikipedia, the free encyclopedia

Ni kweli Hamadi hakuwa Waziri Kiongozi alikuwa Faki,Hamadi alipewa baada ya mapinduzi baridi yaliyofanyika Dodoma.Baada ya hapo bara tulipeleka makomando jeshi la JWTZ kwa kile kilijulikana kama kuchafuka kwa hali ya hewa ya kisiasa Visiwani Zanzibar.Tulipowashusha makomandoo,bandarini Zanzibar asubuhi kama saa 1 wananchi wa hapo walionekana kuwa na majonzi.
 
Nilikuwa sijui kama nyerere alikuwa dikteta kiasi hiki. yaani alikuwa analotaka ndo linalokuwa. Hii ni aibu kwa mtawala ambaye kila kukicha anasifiwa. Alietaka awe rais ndo aliekuwa. Hakupenda kupingwa wala mtu kuwa na mawazo mbadala. Hii ni hatari kwani akiwa hata na maoni ambayo hayana tija kama ya muungano hamna wakumshauri. we do not need a leaders of such kind. KULIKUWA NA UBAYA GANI WA KUACHIA HOJA KAMA ILIKUWAPO KWA MFANO HII YA MUUNGANO KUJADILIWA NA KUWA NA RADHI YA JAMII ZOTE HUSIKA? AU KWENYE HUO MUUNGANO KUNA SIRI GANI? KWA NINI HAKUTAKA KUJADILIWA? MATOKEO YAKE NAONA WATU WANAMKEJELI TU MZEE JUMBE. SISHANGAI HUENDA HUYU MZEE ALIKUWA SAHIHI. This is a century shame!
Hivi, Karume alipoamua kupindua utawala wa Sultani alitoa fursa gani kwa Wazanzibari kujadilia na kutoa radhi yao?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom