Nimeshangazwa na kitendo cha ITV kutotangaza michezo ya Simba SC hata kwa tukio kubwa kama la kutwaa ubingwa wa Vodacom Premier League. Nimeambiwa eti wamewanunia viongozi wa Simba kwa sababu waliwakatalia kurusha 'live' moja ya mechi zao. Kwa maoni yangu huo sio uamuzi sahihi. Ni 'very unprofessional', inabidi ITV wajirudi kabla ya kupoteza umaarufu. Watambue kwamba Simba ni klabu kubwa na ina wapenzi wengi ndani na nje ya nchi. Great Thinkers wengine mnalionaje hili?