Elections 2010 Kulikoni itv dhidi ya cuf??

KAUMZA

JF-Expert Member
Aug 31, 2010
699
237
Wana jukwaa nimekuwa nikifuatilia sana siasa za uchaguzi wa Tanzania Bara tangu zama na zama. Kitu ambacho nimekigundua hasa katika kampeni za mwaka huu ni kuwa mikutano ya ya kampeni ya Chama cha Wananchi, CUF na mgombea wao Prof LIPUMBA haipewi nafasi kabisa katika Television hiyo. Wanaopewa nafasi ni CCM(JK) na CHADEMA(WS). Kwa sasa ukitaka kujua habari za CUF inabidi uangalie TBC ambapo kwa maoni yangu hakuna upendeleo kabisa katikazama hizi za siasa. ANAEWEZA KULITOLEA MAELEZO YA KINA, TAFADHALI ANIONDOLEE DUKUDUKU HILI.
 
KWANi CUF maana yake ni nini?

civic united front: mwenyekiti Prof Ibrahim Limpumba, katibu mkuu Maalim sheikh ustaadhi Seif Ahamad, political base ya chama hiki cha siasa ni jamii ya watanzania wenye itikadi ya dini ya kiislam
 
Mrdash1, kwani ilibidi utaje dini?. Kama CUF ni chama cha udini basi na Chadema pia maana anaekiongoza alikuwa askofu au sio?. wacha mambo hayo.
 
Mrdash1, kwani ilibidi utaje dini?. Kama CUF ni chama cha udini basi na Chadema pia maana anaekiongoza alikuwa askofu au sio?. wacha mambo hayo.

Pole kwa kukwazika. Tangu 2000 mpaka leo ITV imekuwa mstari wa mbele kuichunia CUF, mwaka 2005 walipokuwa na nguvu sana hawakupata coverage yoyote kutoka kwenye vyombo maslahi hivi.. sì magazeti wala TV. Kosa lao kubwa mgombea wao ni muislamu tu. Na kwa kuwa the mision nikupata cha mbadala kitakacho libeba kanisa baada ya CCM na JK kuzushiwa kama kuna udini. Ama kuhusu unafiki na udini wa mengi dhidi ya uislamu ni mkubwa mno na umeanza zamani tu. Mimi nilivyosikia kuna mdahalo nikajiandaa kumuona Dr wa Thiology na fullbright profesa... kumbe ni mchezo wa upande mmoja! wangempa Mnyamwezi nusu saa tu wakaona. Lakini wapi!? Mengi alishaapa kutompa coverage Prof. Huyu jamaa ovyo kabisa mwaka jana aliamuru radio one isitangaze habari za timu ya Simba completely. Huyu ndio Mengi bana! mzee wa maslahi.
 
Unapo zungumzia cuf unazungumzia ccm 'B'.Kwahiyo ccm wanapewa coverage kwa niaba yao.
 
CUF = CCM na hivyo coverage ya ccm ni combination yenu. kura za maoni zimeonyesha CUF itampa jk asilimia 48 ya wanachama wake so usikonde
 
Unapo zungumzia cuf unazungumzia ccm 'B'.Kwahiyo ccm wanapewa coverage kwa niaba yao.

Hayo ni ya kwako na CUF ila nadhani CUF ni chama pekee kilichopata dharubu ya vyombo vya dola. Mpaka mgombea wake wa Uraisi, prof wa ukweli kuvunjwa mkono na wafuasi wake kadhaa kuuwawa, viongozi wao kufungwa kule zenji etc. Tatizo hapa ni udini wa Mangi tu.
 
Kwa kifupi wao wanatoa zaidi lile linalogusa sana jamii,
Kwa mwaka huu Dr. Slaa kagusa sana watanzania. Lakini kwa Prof. ni kama kawa. unajua ITV hawafanyi vitu kwa mazoea ila ni kutokana na priority. Lakini mimi nafuatilia si kwamba hapewi kabisa ila anapewa kama mikutano yake. Lakini la jana ni exceptional.
 
Prof. Lipumba hana nyimbo CD yako ilishagoma kuplay kama ya TFF long time hata mwaka huu anagombea ili apate vijiasilimia fulani vywa kupatia ruzuku maana fungu la uhakika la ruzuku linatikana na % ya kura ya Presidential Candidate...
 
Back
Top Bottom