Kulikoni BAKWATA?

Nyumbu-

JF-Expert Member
May 26, 2009
987
349
Just thinking loudly..........hawa vigogo huku na mwenendo wa magamba. A new Mtandao?

Mufti Simba asambaratisha kamati kwa kushindwa kazi

Wednesday, 03 August 2011 23:00
Hussein Issa
SHEIKH Mkuu wa Tanzania, Mufti Shaaban Issa bin Simba, ameivunja kamati iliyoteuliwa kwa kuunda Jumuiya ya Wanawake wa Kiislamu nchini na kuteua nyingine.

Kamati hiyo mpya iliyoteuliwa ina wajumbe tisa itakuwa chini ya Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata), itaundwa kwa kuhusisha jumuiya mbalimbali za wanawake wa Kiislamu nchini.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Sheikh Simba alisema kamati iliyovunjwa ilishindwa kuwajibika ipasavyo baada ya kupewa jukumu hilo kwa miaka mitatu iliyopita.

“Nimeamua kuivunja kamati niliyoiteua ya kuunda Jumuiya ya Wanawake wa Kiislamu nchini, ambao wanatakiwa kuwa chini ya Bakwata kwa sababu hawakuwa makini,” alisema.
Alisema kutokana na kamati ya awali kushindwa kazi ameamua kuchagua nyingine itakayoongozwa na Shamim Khan na katibu wake atakuwa Mkuu wa Chuo cha Waislam Morogoro (MUM), Mwantumu Malale.
Wajumbe wengine ni Ramia Msemo, Hawa Shafii, Fatma Msindi, Tatu Katuga, Jamila Ahmed, Zawadi Ali na Zaria Saidi.
Mufti Simba alisema kazi ya kamati hiyo ni kutembea mikoa yote na kufanya uhamasishaji wa kuanzisha jumuiya hiyo kufuatana na kanuni za katiba, ambayo inaridhiwa na Baraza la Ulamaa. Ulamaa ni chombo cha juu cha Bakwata.
Licha ya kamati hiyo kupewa jukumu hilo, inatakiwa kuwakilisha taarifa za kila mwezi kwa Mufti kupitia katibu mkuu kuhusu utekelezaji wa majukumu hayo, suala ambalo awali halifanyika.
Naye mwenyekiti wa kamati hiyo, Shamim Khan, alisema watafanya kazi waliyopewa kwa uwezo wao wote na hawatamwangusha Mufti Simba
“Nitashirikiana na wenzangu wote ambao niko nao hapa kufanikisha kuundwa kwa jumuiya hii, kwa kuwangunisha makundi ya wanawake yaliyopo chini ya Bakwata,” alisema
 
asee huo ndo uongoz ,hatahivo kachelewa miaka 3 unavumilia upuuz mimi ningemfire miezi 2 tuu, imeandikwa 'aifanyaye kazi ya mola kwa ulegelege amekwisha laaniwa'
 
Kiukweli Bakwata kuna uozo mkubwa, hata kule Arusha waumini wakigombania mali na Mufti kuitisha kikao cha maulamaa wa bakwata kusuluhishana sijui kimefikia wapi (kimatokeo).
 
Back
Top Bottom