Mtu66
Senior Member
- Jun 26, 2007
- 165
- 3
Askofu Mokiwa: Kuleni hela za wagombea, kura msiwape
Monday, 04 October 2010 07:56 0
Askofu Mkuu wa kanisa la Anglican Tanzania,Valentino Mokiwa,akizungumza Dar es salaam jana,wakati wa uzinduzi wa huduma ya Bina ya afya ya imani,kwa watu wenye kipato cha chini,Bima iliyoanzishwa na mtandao wa afya wa kanisa hilo.
Michael Jamson
ASKOFU mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Valentino Mokiwa amewakumbusha na kuwataka waumini wa kanisa hilo kupokea na kula pesa zote zinazotolewa na wagombea wa nafasi mbalimbali katika kampeni zinazoendelea nchi nzima akisema "fedha za namna hiyo si dhambi, haramu wala rushwa".
Lakini Askofu Mokiwa akawakumbusha waumini kuwa fedha hizo zisiwafanye wawapigie kura wagombea wa namna hiyo kwa kuwa wanaotoa rushwa hiyo ni "wajinga na kula fedha ya mjinga bila ya kumtekelezea azma yake si kosa".Kiongozi huyo wa kidini alisema hayo wakati wa kuzindua mpango wa "Bima ya Afya ya Imani kwa Watu Wenye Kipato cha Chini".
"Mnawajua wagombea wenye sifa na uwezo wa kuongoza, lakini hao wanaokuja kwa kuahidi vitu vingi na kutoa pesa hawafai hata kidogo kuchaguliwa, alisema.
"Pokeeni; kuleni lakini katu msimchague kwa maana kiongozi anayetanguliza hela hatufai; mtu wa namna hiyo mimi ninamuita mjinga na kula hela ya mjinga si haramu; si dhambi na wala si rushwa, ila tu usimtekelezee lile alilotaka kwa kutokumchagua," alisema.
Kwa mujibui wa mpango wa bima hiyo, iliyozinduliwa jijini Dar es Salaam jana eneo la Buguruni Malapa, mwanafamilia anatakiwa kulipia Sh60,000 kwa mwaka kama gharama za vipimo na matibabu ili atibiwa magonjwa matatu ambayo ni maralia, kifua na huduma za wanawake wajawazito.
Alisema magonjwa aliyoyataja ndiyo yanayowasumbua watu wa kipato cha chini mara kwa mmara kutokana na hali na mazingira wanamoishi.
Alisema katika maeneo mengi kumeibuka maduka ya dawa ambayo yako kibiashara zaidi kiasi cha kudiriki kuuza dawa bila hata kuona cheti kutoka kwa daktari.
Alisema nao wananchi kutokana na kukwepa gharama za kumuona daktari, kupima na kununua dawa zinazozidi Sh10,000, huamua kwenda kwenye maduka hayo wanapojisikia dhaifu na kununua dawa.
Naye mwakilishi wa Mtandao wa Afya wa Anglikani, Japhet Makau alisema kwa bara la Afrika, Tanzania ni nchi ya kwanza kunufaika na huduma hiyo na kwamba itakuwa mkombozi mkubwa kwa watu wa kipato cha kawaida maana kanisa limelenga kuwaondolea adha zilizokuwa zikiwakabiri kwa muda mrefu.
Kuleni hela za wagombea, T-shirt vaaaeni....Malori pandeni na chakula kuleni ....kura msiwape kwa sababu ni WAJINGA
Monday, 04 October 2010 07:56 0
Michael Jamson
ASKOFU mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Valentino Mokiwa amewakumbusha na kuwataka waumini wa kanisa hilo kupokea na kula pesa zote zinazotolewa na wagombea wa nafasi mbalimbali katika kampeni zinazoendelea nchi nzima akisema "fedha za namna hiyo si dhambi, haramu wala rushwa".
Lakini Askofu Mokiwa akawakumbusha waumini kuwa fedha hizo zisiwafanye wawapigie kura wagombea wa namna hiyo kwa kuwa wanaotoa rushwa hiyo ni "wajinga na kula fedha ya mjinga bila ya kumtekelezea azma yake si kosa".Kiongozi huyo wa kidini alisema hayo wakati wa kuzindua mpango wa "Bima ya Afya ya Imani kwa Watu Wenye Kipato cha Chini".
"Mnawajua wagombea wenye sifa na uwezo wa kuongoza, lakini hao wanaokuja kwa kuahidi vitu vingi na kutoa pesa hawafai hata kidogo kuchaguliwa, alisema.
"Pokeeni; kuleni lakini katu msimchague kwa maana kiongozi anayetanguliza hela hatufai; mtu wa namna hiyo mimi ninamuita mjinga na kula hela ya mjinga si haramu; si dhambi na wala si rushwa, ila tu usimtekelezee lile alilotaka kwa kutokumchagua," alisema.
Kwa mujibui wa mpango wa bima hiyo, iliyozinduliwa jijini Dar es Salaam jana eneo la Buguruni Malapa, mwanafamilia anatakiwa kulipia Sh60,000 kwa mwaka kama gharama za vipimo na matibabu ili atibiwa magonjwa matatu ambayo ni maralia, kifua na huduma za wanawake wajawazito.
Alisema magonjwa aliyoyataja ndiyo yanayowasumbua watu wa kipato cha chini mara kwa mmara kutokana na hali na mazingira wanamoishi.
Alisema katika maeneo mengi kumeibuka maduka ya dawa ambayo yako kibiashara zaidi kiasi cha kudiriki kuuza dawa bila hata kuona cheti kutoka kwa daktari.
Alisema nao wananchi kutokana na kukwepa gharama za kumuona daktari, kupima na kununua dawa zinazozidi Sh10,000, huamua kwenda kwenye maduka hayo wanapojisikia dhaifu na kununua dawa.
Naye mwakilishi wa Mtandao wa Afya wa Anglikani, Japhet Makau alisema kwa bara la Afrika, Tanzania ni nchi ya kwanza kunufaika na huduma hiyo na kwamba itakuwa mkombozi mkubwa kwa watu wa kipato cha kawaida maana kanisa limelenga kuwaondolea adha zilizokuwa zikiwakabiri kwa muda mrefu.
Kuleni hela za wagombea, T-shirt vaaaeni....Malori pandeni na chakula kuleni ....kura msiwape kwa sababu ni WAJINGA