Kula kiafya kula vizuri na njia inayofaa

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,293
33,078
Good-Diet.jpg




Vitu vitamuvitamu kama keki, kuku wa kukaangwa, vibanzi ni vitamu lakini je vinafaa? Mwili wako hauwezi kuwa katika hali nzuri ya kiafya kwa kuvitegemea hivi vyakula pekee. Kula vyakula vilivyo na rutubishi vya kusaidia moyo wako, na sehemu ya tumbo (isiwe kubwa) utaishi maisha marefu na ya afya nzuri.

Ulijua eti kuna baadhi ya vyakula vinavyoweza kuusaidia mwili wako kupambana na uvamizi wa magonjwa. Ndio. Ni nani asiyetaka hivyo?

Kulingana na taasisi ya lishe bora ya huko Marekani, vyakula virutubishi ni matunda, mboga, nyama isiyo na mafuta, sehemu ya titi ya kuku, mikate ya wishwa, maziwa yasiyo na mafuta, mayai na njugu.

Hivi vyakula havijajazwa mafuta ya kununuliwa na vina virutubishi vyote vinavyohitajika na mwili wa binanadamu. Usitafute vyakula vya kuiva harakaharaka vinavyofanya maisha yetu rahisi kwa sababu tunavipika haraka haraka na kwa urahisi.

Vina mafuta mengi na hunonesha tu mwili lakinii havina virutubishi vya kutosha. Vyakula vilivyowekwa kwenye jokofu, vilivyohifadhiwa ndani ya makaratasi na mikebe, vinaweza kuwa na madini nyingi ya sodium.

Kula vizuri kunahusu kufanya uamuzi unaofaa kila mara. Lengo lako liwe tu kula lishe bora lenye virutubishi vyote visivyo na mafuta mengi na ambavyo si vya kunonesha.

Pia ni muhimu uchunge kiasi cha chakula unachokila. Usiweke tu mlima wa chakula kwenye sahani yako!
 
Mbinu ya kupikia lishe bora


Ikiwa umekuwa na fikira za kubadilisha mtindo mbaya wa kula, basi jifunze kuhusu lishe bora nyumbani ambayo ndiyo sehemu ya kuzingatia kwanza. Hata kama wewe si mpishi hodari, huna budi kujua mbinu bora za kutayarisha vyakula ili kupata virutubishi mwilini. Kwa sababu ukila chakula kilichopikwa na mtu mwingine kama vile hotelini, kwa kweli huwezi kujua kilicho kwenye sahani.

Kupika lishe bora siyo tu muhimu kwa kulinda umbo lako, mbali ni muhimu kwa watu wenye matatizo ya kiafya kama vile, wale wenye ugonjwa wa kisukari, shinikizo la damu na ‘cardiovascular disease" na lazima watumie vyakula vyenye ‘cholesterol' kidogo na sodiamu kidogo ili kuwa na afya bora

Basi epukana na mbinu ya kukaanga. Zingatia mbinu zifuatazo za kupika lishe bora ili kuwa na afya nzuri
Kuoka au mbinu ya kuoka chakula.

Vyakula vya baharini, batamzinga, kuku, nofu isiyokuwa na mafuta yote hupendeza sana yakipikwa kwenye joko. Tia kwenye bunguu ya kuoka mkate kisha uweke jokoni kwa muda uliopendekezwa kupika, kisha utakuwa umemaliza. Kama ni lazima, tumia mafuta kidogo kupaka kwenye sehemu ya chini ya bunguu (sahani)

Kuchoma
Unapotaka kuchoma chakula au kutumia mbinu hii, weka chakula kwenye waya ya kuchomea nyama iliyo juu ya kaa la joto. Kwa vyakula vidogo kama vile mboga iliyokatwa tumia ‘long handled grill basket', itakayozuia vipande vya mboga kuanguka. Ikiwa unabanika ndani ya chumba weka chakula kwenye ‘rack' chini ya kaa la moto. Mbinu zote mbili huacha mafuta kudondoka kutoka kwa chakula.

Kukaanga
Ikiwa ni lazima ukaange chakula, mbinu bora ni kuchukua kikaangiio kikubwa kilicho na mafuta kidogo kisha utie vipande vidogo vya nyama nofu au kuku na mboga unayopenda. Koroga ili iive vizuri na iwe chakula bora au lishe bora.

Kupika au kulainisha chakula kwa mvuke
Mbinu hii hutumia mvuke kutoka kwa maji yaliyochemka
Jaza mtungi kwa inchi moja ya maji, kisha uingize kung'uto, wacha maji ichemke kisha utie mboga halafu ufunike mtungi kwa kifuniko. Pika hadi mboga ilainike.
Mbinu ya kupika chakula kwa kukaanga kwa mafuta kidogo
Mbinu ya kupika chakula kwa kukaanga kwa mafuta kidogo ni sawa na mbinu ya kukaanga, ambayo huivisha chakula kwa haraka. Mbinu hii inahitaji kutia mafuta kidogo kwenye kikaango chini ya joto wastani. Ongeza kuku, nyama ama mboga kwenye kikaango kwa kuzingatia kuwa kuna nafasi ya kutosha kwenye kikaango inayotosha kupika chakula.

Tumia aina nyigine ya mafuta badala ya mafuta iliyoloa. Kama maelezo ya upishi yahitaji maziwa, baadhi ya matunda. Tumia mafuta kama vile mafuta ya zeituni. Badala ya mafuta ya kawaida. Badala ya krimu kali tumia jibini au chizi iliyotengenezwa kutoka kwa maziwa machunda. Jaribu na mimea ya msimu kuongeza ladha badala ya chumvi.
 
Ununuzi wa afya na busara

healthy_food..JPG





Kwa kuwa unajua sasa kuhusu lishe bora, usiingie tu ndani ya duka la kuuzia chakula na kuokota aina yoyote ya vyakula. La. Usipatie mwili wako chakula ambacho hauhitaj. Usitafute tu vyakula vya kukaanga haraka haraka na kuvila. Jaribu kuzingatia yafuatayo unaponunua chakula.

Panga mapema. Panga chakula cha kukutosha kwa wiki nzima. Andika orodha ya vitu utakavyohitaji kupikia. Utakuwa na muongozo wa kukufanya uzingatie lishe bora.

Nunua chakula chako kwenye duka la kuuzia chakul nje ya jingo kwani huwa hakijakaa kwa muda mrefu. Nunua mboga, matunda, vyakula vya baharini, nyama isiyo na mafuta, kuku, maziwa, mayai na mkate mahali ambapo ni pazuri (usinunue chakula ambacho huenda kimewekwa kwenye friji na kimeishi kwa muda mrefu).

Nunua vyakula ambavyo vina rutuba zote "whole meal" epuka vyakula ambavyo vimewekwa kemikali. Ongeza sukari na chumvi ukiwa nyumbani.


Vyakula vilivyohifadhiwa kwenye mikebe au jokofu huonekana vizuri na rahisi kuandaa usivigugue. Tafuta vile ambavyo havijahifadhiwa na havijakaa kwa mda mrefu.

Nunua tu wakati ambapo inakubidi. Lengo lako ni kupatia familia yako na wewe, lishe bora weka haya akilini kila mara unapoenda kununua chakula.
 
Virutubishi vinayotumiwa na mwili na vinavyohifadhiwa kama mafuta.


Mwili wako ni tarakilishi vizuri sana ulimwenguni. Unajua kujifanyia hesabu kuhusu chakula cha kutumiwa na cha kuhifadhiwa mwilini kama mafuta. Huwezi kuupatia chakula kisichofaa bila mwili wenyewe kutambua jambo lolote mbaya unalolifanay, liwe matokeo yake mazuri au mabaya. Iwapo utakumbuka kuwa

Mwili wako huchoma au huhifadhi kalori ya vyakula unavyokula. Unaweza ukakabiliwa na kuongeza au kupunguza uzito wako.

Je, kalori ni nini? Ni kilio cha joto au kipimo cha joto litolewalo na chakula
Kwa kila kalori unayokula, lazima uwe na mbinu utakayotumia kuiondoa. Ukila kalori nyingi, huenda ukasababisha ongezeko la mafuta kwenye mapaja, makalio na sehemu nyinginezo za mwili. Ukila kadri mwili wako unavyoweza kuicho, basi utabaki na kiwango cha uzito ulio nao. Lakini ukichoma kalori nyingi unayokula kila siku kupitia mazoezi ya kila siku na lishe bora utakuw katika harakati ya kupunguza uzito wako.
Kuhifadhi uzito ulio nao, hutegema kalori ya vyakula na nguvu unazotumia katika mazoezi ya kila siku.

Je, utajuaje ni kiwango kipi cha kalori unahitaji ili kuhifadhi uzito wako? Tumia mbinu hii: Je, unahitaji kalori ngapi?
Mbinu au mtindo wa zamani

Pia waweza kupima ili kujua kiwango cha kalori unayohitaji kila siku kwa kutumia fomula zifuatazo zinazojumuisha shughuli zako za kila siku.

Kwa watu wanaokaa tu bila kufanya mazoezi: uzito wako x 14 = kipimo cha kalori unayohitaji kila siku

Kwa watu wanaofanya mazoezi kiasi kidogo: Uzito wako x 17 – kalori unayohitaji kila siku

Kwa watu wanaofanya mazoezi sana: Uzito x 20 = Kipimo cha kalori unayohitaji kila siku

Kufanya mazoezi kwa kiwango cha wastani yamaanisha kuwa kupata mazoezii ya viungo vya kuongeza hewa angalau mara tatu au nne kwa Juma. Kufanya mazoezi sana yamaanisha mazoezi ya viungo angalau mara tano au saba kwa Juma. Kutofanya mazoezi yamanisha kuwa, unatumia muda wako mwingi kukaa tu badala ya kufanya mazoezi au kujishughulisha.

Umejifunza namna ya kukabiliana na kalori unayokula, utafanya nini ili kuchoma kalori leo? Anza kukabiliana na tatizo hili.
 
Naam, mkuu nashukuru sana kwa hili darasa..

ubarikiwe sana.
 
ahsante mkuu ila misosi hiyo kijijini adimu lazima uwe na vyako ndiyo utakula hivo sasa imekaaje mkuu,
Conquest-kula vizuri nafasi/uwezo:smile-big:
 
ahsante mkuu ila misosi hiyo kijijini adimu lazima uwe na vyako ndiyo utakula hivo sasa imekaaje mkuu,
Conquest-kula vizuri nafasi/uwezo:smile-big:
Mkuu wewe unakaa kijiji gani? kila kijiji kina Wakulima na vyakula vyote vinavyopatikana mijini huwa vinatoka sana vijijini je wewe kijiji chako huwa hakilimi Mazao ya chakula?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom