Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Kula huku kula gani, kula bila ya kunawa?
Kula huku kula gani, kula bila kupumua?
Kula huku kula gani, kula bila kuchagua?
Kula huku kula gani, vya watoto navyo mwala?
Kula huku kula gani, mikono yote miwili?
kula huku kula gani, mbona nyinyi si makuli?
Kula huku kula gani, mwala hadi pilipili?
KUla huku kula gani, vya watoto navyo mwala?
Kula huku kula gani, kula huku mwacheua,
Kula huku kula gani, na meno mmekenua,
Kula huku kula gani, huku mnajisheua,
Kula huku kula gani, vya watoto navyo mwala?
Kula huku kula gani, mwala huku mwavimbiwa,
Kula huku kula gani, na harufu mnatowa,
Kula huku kula gani, na jasho hilo mwalowa,
Kula huku kula gani, vya watoto navyo mwala?
Kula huku kula gani, mwagawiana sinia,
Kula huku kula gani, zamu mnajipangia,
Kula huku kula gani, mwala tena mwarudia,
Kula huku kula gani, vya watoto navyo mwala?
Kula huku kula gani, mnakula hadi mbegu,
Kula huku kula gani, mwayala hata magugu,
Kula huku kula gani, huku mwatuita ndugu,
Kula huku kula gani, vya watoto navyo mwala?
Kula mmeshakwishakula, sasa muda wa kulipa,
Vya wanetu mmekula, kulipa na mtalipa,
Mlidhani tumelala, wajanja mkatukopa,
Vya kwenu hatutavila, na kura hatutawapa!
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
Kula huku kula gani, kula bila kupumua?
Kula huku kula gani, kula bila kuchagua?
Kula huku kula gani, vya watoto navyo mwala?
Kula huku kula gani, mikono yote miwili?
kula huku kula gani, mbona nyinyi si makuli?
Kula huku kula gani, mwala hadi pilipili?
KUla huku kula gani, vya watoto navyo mwala?
Kula huku kula gani, kula huku mwacheua,
Kula huku kula gani, na meno mmekenua,
Kula huku kula gani, huku mnajisheua,
Kula huku kula gani, vya watoto navyo mwala?
Kula huku kula gani, mwala huku mwavimbiwa,
Kula huku kula gani, na harufu mnatowa,
Kula huku kula gani, na jasho hilo mwalowa,
Kula huku kula gani, vya watoto navyo mwala?
Kula huku kula gani, mwagawiana sinia,
Kula huku kula gani, zamu mnajipangia,
Kula huku kula gani, mwala tena mwarudia,
Kula huku kula gani, vya watoto navyo mwala?
Kula huku kula gani, mnakula hadi mbegu,
Kula huku kula gani, mwayala hata magugu,
Kula huku kula gani, huku mwatuita ndugu,
Kula huku kula gani, vya watoto navyo mwala?
Kula mmeshakwishakula, sasa muda wa kulipa,
Vya wanetu mmekula, kulipa na mtalipa,
Mlidhani tumelala, wajanja mkatukopa,
Vya kwenu hatutavila, na kura hatutawapa!
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)