Kakukuruka vyema,
Kaachiwa na kuonyeshwa tundu la kutokea, badala yake kajidanganya kwa kutamani mbegu chache zilizobakia kwenye tenga. Anarudi, anarushiwa mchele wa kutosha nje ya tenga hataki kutoka kisa mahindi kiduchu. Kwa kiburi kabisa anajaribu kuwadonoa hata wale ambao wangemsaidia, anawatishia... anang'ang'ania kukaa kwenye tenga!
Kwakuwa ni 'kuku wa kizungu' tumwache tusifunike tenga na 'kumshughulikia'?
Jamani Kuku anayezungumziwa hapa ni wananchi wa Igunga ambao kwa hiari yao walijikuta katika utawala(Tenga) wa CCM kwa miaka nenda rudi.Wamefunguliwa mlango wa tenga na kelele za ufisadi za Chadema zilizomtoa fisadi Rostam(Rostam ndiye mlango wa tenga) wamewekwa huru toka mikono ya CCM, cha ajabu wanaigunga hawataki kutoka kwa sababu tu ya woga wao ilhali nje(chadema) kuna manufaa endelevu ya kitaifa, huku wana igunga wakithubutu hata kuwa kuwadhihaki waliowafungulia mlango wa kutoka(Chadema)
Nawasilisha