Kuku anaingia mwenyewe kwenye tenga...

Invisible

Robot
Feb 11, 2006
9,075
7,878
Kakukuruka vyema,

Kaachiwa na kuonyeshwa tundu la kutokea, badala yake kajidanganya kwa kutamani mbegu chache zilizobakia kwenye tenga. Anarudi, anarushiwa mchele wa kutosha nje ya tenga hataki kutoka kisa mahindi kiduchu. Kwa kiburi kabisa anajaribu kuwadonoa hata wale ambao wangemsaidia, anawatishia... anang'ang'ania kukaa kwenye tenga!

Kwakuwa ni 'kuku wa kizungu' tumwache tusifunike tenga na 'kumshughulikia'?
 
Mwache, msimpige mawe. Kaingia mwenyewe ni vema akachinjwa kabisa na viranga wake waangamizwe.

Hii si mbegu nzuri kuwepo bandani. Anadonoa wengine na kwa jinsi alivyo atawauwa nao......
 
Invisible hapa jf nadhan tupo huru sana jaribu kumuweka waz huyo kuku tumjue kuliko kutuacha solemba,ila kama ni kuku wa kisasa as if RA hv
 
Kakukuruka vyema,

Kaachiwa na kuonyeshwa tundu la kutokea, badala yake kajidanganya kwa kutamani mbegu chache zilizobakia kwenye tenga. Anarudi, anarushiwa mchele wa kutosha nje ya tenga hataki kutoka kisa mahindi kiduchu. Kwa kiburi kabisa anajaribu kuwadonoa hata wale ambao wangemsaidia, anawatishia... anang'ang'ania kukaa kwenye tenga!

Kwakuwa ni 'kuku wa kizungu' tumwache tusifunike tenga na 'kumshughulikia'?

thirsty.jpg
 
Mimi naona tukupe mji ili utupe jibu.
Na mji ni Bagamoyo au igunga,chagua moja
 
mna uhakika ni kuku? isijekuwa kanga!

Na huenda akawa ni mbuni.
Alikuwa anataka kutaga, akaona tenga limezagaazagaa kichakani, akapata pango la kutagia.
Mmemfukuza akakimbia. Kabla hafika mbali ndo anakumbuka kuwa ameacha mayai yake kwenye tenga. Kumbukeni, mayai ni watoto watarajiwa hao!
 
Na huenda akawa ni mbuni.
Alikuwa anataka kutaga, akaona tenga limezagaazagaa kichakani, akapata pango la kutagia.
Mmemfukuza akakimbia. Kabla hafika mbali ndo anakumbuka kuwa ameacha mayai yake kwenye tenga. Kumbukeni, mayai ni watoto watarajiwa hao!
Tumia akili wewe, tenga ni dogo kuliko mbuni. Aliyemuona anasema ni kuku sasa huyo mbuni utakuwa umemleta wewe?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom