lukindo
JF-Expert Member
- Mar 20, 2010
- 8,466
- 9,028
Habari wana jf
Nimekuwepo Dar es Salaam na na-experience mgao wa umeme wa mara kwa mara. Hii imekuwa mitaani (residential places) lakini na mjini pia (katikati ya mji na Kariakoo) kuna ukatikaji usio rasmi. Hivi ninavyoandika umeme huku katikati ya mji hakuna na ilikuwa hivi kwa zaidi ya majuma mawili yaliyopita.
Sijamuona dada yetu Badra Masoud au Waziri Ngereja wakiongelea tatizo hili kwa siku hizi! Kama sikosei waziri na Tanesco waliwahi hapo nyuma kidogo kusema mgao ulikuwa umeisha (kama sio kupungua).
Kulikoni, mwenye taarifa na kinachoendelea naomba atujuze ili tuweze kupanga ratiba hizi za 'mateso'.
Inasikitisha!!!.
Nimekuwepo Dar es Salaam na na-experience mgao wa umeme wa mara kwa mara. Hii imekuwa mitaani (residential places) lakini na mjini pia (katikati ya mji na Kariakoo) kuna ukatikaji usio rasmi. Hivi ninavyoandika umeme huku katikati ya mji hakuna na ilikuwa hivi kwa zaidi ya majuma mawili yaliyopita.
Sijamuona dada yetu Badra Masoud au Waziri Ngereja wakiongelea tatizo hili kwa siku hizi! Kama sikosei waziri na Tanesco waliwahi hapo nyuma kidogo kusema mgao ulikuwa umeisha (kama sio kupungua).
Kulikoni, mwenye taarifa na kinachoendelea naomba atujuze ili tuweze kupanga ratiba hizi za 'mateso'.
Inasikitisha!!!.