Mbinu za kukata vitunguu pasipo kutokwa na machozi

tya02

JF-Expert Member
Nov 26, 2014
850
1,061
Habari zenu,

Wengi wetu tukimenya vitunguu maji na kuvikatakata mara nyingi tunatoa machozi.

Sasa chukua kikombe au bakuli tia chumvi na maji halafu weka pembeni huku ukikatakata vitunguu vyako; kamwe hautotoa chozi wala hutowashwa.

Jaribu leo.

Njia mbadala 1:

Pia anaweza kukiloweka kitunguu kwenye maji ya moto kwa dk 3 kabla ya kukikata Au kukiweka kwenye freezer kwa dk 10 kabla ya kukikata. Zote hizo zinasaidia

Njia mbadala 2:

Kata kipande kidogo cha kitunguu halafu kiweke kichwani. Kisha endelea kukata kitunguu kama kawaida wala machozi hayatakutoka.

Njia mbadala 3:

Mimi huwa ninavimenya vyenyewe kwanza kabla ya vitu vingine kama nyanya na karoti, then naviacha kwenye yale maji yakuoshea, so hadi nikimaliza kumenya na kukata vitu vingine ndo navitoa kwenye maji na kuvikata.

Naona hii ni simplest way coz u don need any extra things lyk chumvi, sijui bakuli la maji pemben au kuweka kipande kichwani, but also najua kuna umuhimu wa hiyo kemikali yake kwenye mwili ila mambo ya kububujikwa machoz kila mara nehiii.

Njia mbadala 4:

njia nyingine rahisi ni kukata kitunguu huku ukiwa unatafuna kitu chochote iwe big g au carrot mradi uwe unatafuna hakitakuathiri na ni njia nyepesi
 
Du bora mwanangu anapenda kachumbali lkn akinza kukata huwa si machozi bali ni kulia nitampa habari njema.
 
Du bora mwanangu anapenda kachumbali lkn akinza kukata huwa si machozi bali ni kulia nitampa habari njema.
Pia anweza kukiloweka kitunguu kwenye maji ya moto kwa dk 3 kabla ya kukikata Au kukiweka kwenye freezer kwa dk 1o kabla ya kukikata..Zote hizo zinasaidia
 
Mie nakerwa na ile harufu ya kitunguu kwenye mikono baada ya kukata. Hata ninawe kwa sabuni bado nitaisikia. Wakati mwingine km ni usiku basi kesho yake asubuhi bado nitaisikia.
 
Habari zenu,

Wengi wetu tukimenya vitunguu maji na kuvikatakata mara nyingi tunatoa machozi.

Sasa chukua kikombe au bakuli tia chumvi na maji halafu weka pembeni huku ukikatakata vitunguu vyako kamwe hautotoa chozi wala hutowashwa.

Jaribu leo.

Mimi huwa ninavimenya vyenyewe kwanza kabla ya vitu vingine kama nyanya na karoti, then naviacha kwenye yale maji yakuoshea, so hadi nikimaliza kumenya na kukata vitu vingine ndo navitoa kwenye maji na kuvikata.

Naona hii ni simplest way coz u don need any extra things lyk chumvi, sijui bakuli la maji pemben au kuweka kipande kichwani, but also najua kuna umuhimu wa hiyo kemikali yake kwenye mwili ila mambo ya kububujikwa machoz kila mara nehiii.
 
njia nyingine rahisi ni kukata kitunguu huku ukiwa unatafuna kitu chochote iwe big g au carrot mradi uwe unatafuna hakitakuathiri na ni njia nyepesi
 
Njia nzuri ya kukata vitunguu bila kutokwa machozi ni kuvaa helmet yenye kufunika kwa mbele au kuvaa miwani (goggles)
images.jpeg
images-1.jpeg


"ᴬ ᵐᵃⁿ ʷʰᵒ ˢᵗᵃⁿᵈˢ ᶠᵒʳ ⁿᵒᵗʰⁱⁿᵍ ʷⁱˡˡ ᶠᵃˡˡ ᶠᵒʳ ᵃⁿʸᵗʰⁱⁿᵍ"
 
Back
Top Bottom