Kujinufaisha kupitia bank technical holes.

Developer

JF-Expert Member
Jan 8, 2011
446
503
Wakuu mi nna ka account kangu kwenye benki ya makabwela, NMB. Nakumbuka miezi ka minne hivi iliyopita nilikuwa nna sh alfu 40 , na nilikuwa nimepoteza kadi so nikaenda ndani kwenye counter nikadraw pesa yote(40) halafu ndani ka ya dakika tano baada ya kupewa pesa nikafikiri hawa watakuwa hawaja update database zao. Nikachukua simu yangu ya mkononi nikabofya kupitia NMB Mobile nikafanikiwa kununua vocha za sh 40. Nikajua watanipigia au ntakuta na negative elfu 40 waki upadate system au tu watakata nikiweka pesa. La tofauti na matarajio yangu kuna pesa niliwekewa baada kama ya mwezi na hawajakata chochote mpaka sasa? Swali langu je hii ina madhara gani kisheria za kibiashara incase naongeza ongeza kakiwango na kuzitoa kila mara kwa kamchezo haka? Ukizingatia hatuna mkataba wa kukopeshwa pesa kutoka kwenye hizi akaunti za kawaida?
 
lazima utakatwa tuu
toka mwaka jana mwezi wa nane mpaka leo hawakata, so huoni naweza kula bata kimtindo mpaka waje washtuke, labda uniambie madhara yake kisheria za kibiashara
 
toka mwaka jana mwezi wa nane mpaka leo hawakata, so huoni naweza kula bata kimtindo mpaka waje washtuke, labda uniambie madhara yake kisheria za kibiashara

mkuu... bank transactions zinafanyiwa auditing and re auditing ... ...auditors wa ndani na nje ..... tena na makampuni yanayokodishwa na makubwa hata miaka mitatu watakata tuu
 
toka mwaka jana mwezi wa nane mpaka leo hawakata, so huoni naweza kula bata kimtindo mpaka waje washtuke, labda uniambie madhara yake kisheria za kibiashara
kuna jamaa yangu alijikuta anakatwa laki sita alikuwa na kamchezo hako....... siku walipoupdata wakalmba hiyo deni... nusure awe chizi.. chukua kilicho halali yako.
 
NMB wateja wengi ,na systems zao haziko makini sana,inategemea sana human interactions otherwise ,report alerts zingekwisha kukamata muda mrefu.ila kumbuka benki na wewe mna mkataba wa kufanya kazi in a good will/faith,
hivyo bora urekebishe hili swala lako else siku ya kuitwa kuijeleza itakuwa aibu ukizingatia ni elfu 40 tu.
 
Hapo ujue itakuja kula kwako. Mie niliwahi kuingiziwa mshahara wa mwezi mmoja mara mbili, na nikawa sijui, ila baada ya miezi 7 nikashangaa nilipokwenda kucheck kama mshahara umeingia nikakuta umeingia na kutoka na akiba iliyokuwepo. Kwenda benki kuuliza kulikoni, waka-print statement ya mwaka mzima, ndo nikadundua kuwa kuna mwezi mmoja niliingiziwa mshahara double. Kwa hiyo ikawa maumivu, sikuwa na jinsi, bali kukubaliana na hali halisi. Kosa lilikuwa lao, ila mimi sikujua.
 
huo ni wizi. omba waamue kutoenda polisi. utakatwa tena kwa interest.
 
Toka kadi ilivyopotea ulikaa muda gani ndo ukaenda bank?, cause kwa uelewa wangu kama kadi ikipotea na HUDUMA, ya NMB mobile huwezi kuaccess endapo utakuwa umeriport kuwa kadi yako, imepotea, hii ni kutokana ATM ina connection na NMB MOBILE, usije ukawa unatuingiza chaka kaka, au unataka utumie ujanja huo, cause mi nachojua endapo kama ulifanikiwa kutokana na system misbehave , baada ya siku kadhaa akaunti yako ingeoverdraw, na kama ingeoverdraw, ela yoyote ingewekwa kwenye akaunti yako, ingeclear hiyo OVERDRAW(NEGATIVE BALANCE)
 
Back
Top Bottom