"kujifanya uko juu kunacost sana mazee dah...!"

david mkwizu

Member
Jul 31, 2011
29
9
jamaa mmoja alikua anakaa kwenye kamji kadogo hivi..! sasa akafanikiwa kwenda kwenye school of law 'kusomea sheria'... baada ya kumaliza masomo yake akadhani ni vizuri arudi mjini kwao ili afanye kazi pale kwasababu hapakua na wanasheria wa kutosha..! alipofika akafungua ofisi ya mambo ya sheria "advocacy"...!

alipoanza mambo hayakua mazuri sana kwa sababu ya biashara kua ngumu na akaamua kuwa atafanya kila awezavyo ili awaoneshe watu wa mji ule kua anaweza..

siku moja wakati yuko ofisini kwake akaona mtu anatembea kuja mlangoni kwake "ofisini kwake" akasema ntafanya kila njia ili huyu mtu anikubali kua mimi niko juu kwenye mambo ya uwakili....
basi kabla yule mtu hajaingia mlangoni jamaa huku ndani akanyanyua simu akaanza kuongea huku akimkaribisha huyu mtu aketi (kwa ishara tu lakini)........" nimewaambia bila milioni mia tano hiyo kesi mimi siimalizi.. kwani si inabidi nije huko malaysia na jopo la vijana wangu" aliendelea kuongea jamaa kwenye simu.. "hata hivyo baada ya kusikiliza maamuzi yaliyofanywa na huyo jamaa wa woshington mimi itanibidi niende kwanza nikakae nae so niatakua na siku kama mbili hivi hapo D.C then ndio nitakuja huko... sijui tumeelewana.. haya ninakutakia siku njema kwenye utendaji wako bwana.....!"

akarudisha simu chini na kumwambia huyu mgeni aliyekua amekaa kwa utulivu kwenye kiti..." karibu bwana samahani nilikua busy kidogo samahani kwa usumbufu..! nikusaidie tafadhali...!

yule mgeni akamwambia mimi ni mfanyakazi wa kampuni ya simu hapa mjini nimekuja kukuunganishia line ya simu yako ambayo ilifungwa tangu mwezi uliopita

jamaa akajikuta anatokwa na jasho la kwapa...!
 
DUH! I don't mean to ruin it but,ain't he supposed to hook it up from the outside?..What was he doing inside?
 
Daaah!jamaa alileta umaarufu wa kuj**ba wakati anahar**ha tehe tehe
 
Hizi ni tabia za watu kuna mwingine unamwona sehemu let say bar then unapigia simu anakupa fix live kuwa yupo mkoa mwingine kikazi...unachofanya unamtuma mhudumu amjalie anachokunywa ...utamwona kasura kanavyokuwa kadogo kama ka arsene wenger akichwapwa na mashetani!!...Ila hii ya huu mwanasheria ni typical kayanga..kashozi type!!
 
Hizi ni tabia za watu kuna mwingine unamwona sehemu let say bar then unapigia simu anakupa fix live kuwa yupo mkoa mwingine kikazi...unachofanya unamtuma mhudumu amjalie anachokunywa ...utamwona kasura kanavyokuwa kadogo kama ka arsene wenger akichwapwa na mashetani!!...Ila hii ya huu mwanasheria ni typical kayanga..kashozi type!!
 
nilishaisoma namba hiyo hiyo ni strori ya kweli iliyomtokea jamaa wa kihayyya! samahanini watani teh teh@!
 
Back
Top Bottom