Kujenga kwa mshahara inawezekana??

ABEDNEGO

Senior Member
Aug 20, 2009
109
30
Jambo hili limenifikirisha na kunitatiza kwa muda mrefu sana jinsi gani watanzania wanavyoweza kujenga majumba ya kifahari ili hali ni watumishi wa serikali!!! Mimi ni mtumishi wa serikali wa muda mrefu sasa na napata kiwango cha juu vya mshahara wa serikali.Nikisema vya juu nina maana ya kuwa sawa na ngazi za makatibu wakuu.Tangu miaka hiyo ya 90 sijamaliza nyumba yangu ya kawaida tu.Wenzangu miaka miwili wanaporomosha majumba YA KUTISHA sijaona.Je ni kweli mshahara wa serikali unaweza kujenga nyumba tena ya kifahari??Najua kuna ufisadi lakini ndo watumishi wote wawe mafisadi ndo wajenge?Vijana wanaomaliza vyuo ndani ya miaka miwili wanajenga na kununua magari siri yake ni nini hasa?Kwani nimechukua hata mkopo wa Benki kulipa kwa mshahara nikajikuta nazidi matatizo ndani ya nyumba.Nisaidieeni tafadhali
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom