Jpinduzi
Senior Member
- Feb 26, 2011
- 136
- 68
Watu wengi wamekuwa wakijiuliza je, baada ya kupata mimba bado mtu anaweza kuendelea kufanya mapenzi? Ni salama? Halafu huwa inakuwaje? Wataalamu wanasema mtu anaweza kuendelea kula uroda pamoja na kuwa ana mimba.
Mapenzi, kujamiiana, na kuwa karibu zaidi kimoyo yote ni mambo muhimu kwa furaha ya ujauzito.Baadhi ya wanawake wanajisikia vizuri kujamiiana wakiwa wajawazito. Baada ya wiki ya 12, wakati ambapo hali ya kichefuchefu na uchovu kwa kawaida hupungua, hisia nzuri hujitokeza. Damu hutiririka kwa wingi maeneo ya kiunoni, na kiwango cha homoni za kujisikia vizuri huongezeka hadi karibu na mwisho wa ujauzito.
Hii yote inachangia kukuza hamu ya kujamiiana. Ni salama kujamiiana? Kama ujauzito wako ni mzuri kiafya na unajisikia vizuri, hakika hakuna sababu ya kutokujamiiana. Baadhi ya wanawake madhara ya ujauzito yanawafanya wasijisikie kufanya mapenzi. Hii inaweza kuwapata hata wanaume. Kichefuchefu na uchovu vinaweza kukufanya usiwe na mawazo ya kujamiiana.
Baadhi ya wanaume hukataa kufanya mapenzi kwa kuogopa kumdhuru mtoto. Usikilize mwili wako. Usijilazimishe kufanya kitu ambacho hakikupi raha. Ni muhimu pia kukumbuka kwamba tumbo kubwa linaweza kuwa kipingamizi kati yenu. Hapa inabidi kubadilisha mtindo / miondoko. Wapenzi wanaweza kuwa karibu bila kujamiiana. Kupigana mabusu na kukumbatiana kunawafanya kujisikia kama vile mmeshafanya mapenzi. Kitu cha muhimu ni kuelewa mwenzako anajisikiaje. Zungumza na sikiliza mahitaji ya mwenzio.
Mapenzi, kujamiiana, na kuwa karibu zaidi kimoyo yote ni mambo muhimu kwa furaha ya ujauzito.Baadhi ya wanawake wanajisikia vizuri kujamiiana wakiwa wajawazito. Baada ya wiki ya 12, wakati ambapo hali ya kichefuchefu na uchovu kwa kawaida hupungua, hisia nzuri hujitokeza. Damu hutiririka kwa wingi maeneo ya kiunoni, na kiwango cha homoni za kujisikia vizuri huongezeka hadi karibu na mwisho wa ujauzito.
Hii yote inachangia kukuza hamu ya kujamiiana. Ni salama kujamiiana? Kama ujauzito wako ni mzuri kiafya na unajisikia vizuri, hakika hakuna sababu ya kutokujamiiana. Baadhi ya wanawake madhara ya ujauzito yanawafanya wasijisikie kufanya mapenzi. Hii inaweza kuwapata hata wanaume. Kichefuchefu na uchovu vinaweza kukufanya usiwe na mawazo ya kujamiiana.
Baadhi ya wanaume hukataa kufanya mapenzi kwa kuogopa kumdhuru mtoto. Usikilize mwili wako. Usijilazimishe kufanya kitu ambacho hakikupi raha. Ni muhimu pia kukumbuka kwamba tumbo kubwa linaweza kuwa kipingamizi kati yenu. Hapa inabidi kubadilisha mtindo / miondoko. Wapenzi wanaweza kuwa karibu bila kujamiiana. Kupigana mabusu na kukumbatiana kunawafanya kujisikia kama vile mmeshafanya mapenzi. Kitu cha muhimu ni kuelewa mwenzako anajisikiaje. Zungumza na sikiliza mahitaji ya mwenzio.