Kujamiiana wakati wa ujauzito

Jpinduzi

Senior Member
Feb 26, 2011
136
68
Watu wengi wamekuwa wakijiuliza je, baada ya kupata mimba bado mtu anaweza kuendelea kufanya mapenzi? Ni salama? Halafu huwa inakuwaje? Wataalamu wanasema mtu anaweza kuendelea kula uroda pamoja na kuwa ana mimba.
Mapenzi, kujamiiana, na kuwa karibu zaidi kimoyo yote ni mambo muhimu kwa furaha ya ujauzito.Baadhi ya wanawake wanajisikia vizuri kujamiiana wakiwa wajawazito. Baada ya wiki ya 12, wakati ambapo hali ya kichefuchefu na uchovu kwa kawaida hupungua, hisia nzuri hujitokeza. Damu hutiririka kwa wingi maeneo ya kiunoni, na kiwango cha homoni za kujisikia vizuri huongezeka hadi karibu na mwisho wa ujauzito.

Hii yote inachangia kukuza hamu ya kujamiiana. Ni salama kujamiiana? Kama ujauzito wako ni mzuri kiafya na unajisikia vizuri, hakika hakuna sababu ya kutokujamiiana. Baadhi ya wanawake madhara ya ujauzito yanawafanya wasijisikie kufanya mapenzi. Hii inaweza kuwapata hata wanaume. Kichefuchefu na uchovu vinaweza kukufanya usiwe na mawazo ya kujamiiana.

Baadhi ya wanaume hukataa kufanya mapenzi kwa kuogopa kumdhuru mtoto. Usikilize mwili wako. Usijilazimishe kufanya kitu ambacho hakikupi raha. Ni muhimu pia kukumbuka kwamba tumbo kubwa linaweza kuwa kipingamizi kati yenu. Hapa inabidi kubadilisha mtindo / miondoko. Wapenzi wanaweza kuwa karibu bila kujamiiana. Kupigana mabusu na kukumbatiana kunawafanya kujisikia kama vile mmeshafanya mapenzi. Kitu cha muhimu ni kuelewa mwenzako anajisikiaje. Zungumza na sikiliza mahitaji ya mwenzio.
 
Kujamiiana wakati wa ujauzito kuna madhara kwa mtoto aliye tumboni................ najua wapenda ngono watanibishia, lakini huo ndio ukweli wenyewe.
Ikumbukwe kwamba mtoto aliye tumboni hutumia pumzi ya mama, hivyo basi wakati tendo la ndoa linapofanyika na mama anapotaka kufika kileleni kunakuwa namabadiiko makubwa ya pumzi na hiyo humsababisha mtoto kuhangaika kule tumboni. inaelezwa kwamba wakati mwingine husababisha kifo cha mtoti tumboni...............

Wanawake wanalazimika kufanya tendo hilo wakati wa ujauzito kwa sababu ya kulinda ndoa zao, wanawajua waume zao wakikosa tendo kwa muda mrefu, watadesa nje......................
 
Hicho ni kisa asili tu, hakina ukweli wowote................. Ondoa tamaa yako hapa...........

Na wakunga wanasisitiza umkune mke wako mpaka abakishe wiki 2 kujifungua njia inakuwa wazi
 
Kujamiiana wakati wa ujauzito kuna madhara kwa mtoto aliye tumboni................ najua wapenda ngono watanibishia, lakini huo ndio ukweli wenyewe.Ikumbukwe kwamba mtoto aliye tumboni hutumia pumzi ya mama, hivyo basi wakati tendo la ndoa linapofanyika na mama anapotaka kufika kileleni kunakuwa namabadiiko makubwa ya pumzi na hiyo humsababisha mtoto kuhangaika kule tumboni. inaelezwa kwamba wakati mwingine husababisha kifo cha mtoti tumboni...............Wanawake wanalazimika kufanya tendo hilo wakati wa ujauzito kwa sababu ya kulinda ndoa zao, wanawajua waume zao wakikosa tendo kwa muda mrefu, watadesa nje......................
eeehh!! kumbe....!! acha nimwambie anipumzishe!!!!
 
eeehh!! kumbe....!! acha nimwambie anipumzishe!!!!

unaweza ukajikuta mapumziko yanakuwa ya muda mrefu na kupelekea kupoteza mpenzi/mume kabisa. we endelea kumpa tu la muhimu hapo ni kwamba missionary style should be foregone for sometime
 
Kujamiiana wakati wa ujauzito kuna madhara kwa mtoto aliye tumboni................ najua wapenda ngono watanibishia, lakini huo ndio ukweli wenyewe.
Ikumbukwe kwamba mtoto aliye tumboni hutumia pumzi ya mama, hivyo basi wakati tendo la ndoa linapofanyika na mama anapotaka kufika kileleni kunakuwa namabadiiko makubwa ya pumzi na hiyo humsababisha mtoto kuhangaika kule tumboni. inaelezwa kwamba wakati mwingine husababisha kifo cha mtoti tumboni...............

Wanawake wanalazimika kufanya tendo hilo wakati wa ujauzito kwa sababu ya kulinda ndoa zao, wanawajua waume zao wakikosa tendo kwa muda mrefu, watadesa nje......................

shukran mkuu kwa darasa...
 
Kujamiiana wakati wa ujauzito kuna madhara kwa mtoto aliye tumboni................ najua wapenda ngono watanibishia, lakini huo ndio ukweli wenyewe.
Ikumbukwe kwamba mtoto aliye tumboni hutumia pumzi ya mama, hivyo basi wakati tendo la ndoa linapofanyika na mama anapotaka kufika kileleni kunakuwa namabadiiko makubwa ya pumzi na hiyo humsababisha mtoto kuhangaika kule tumboni. inaelezwa kwamba wakati mwingine husababisha kifo cha mtoti tumboni...............

Wanawake wanalazimika kufanya tendo hilo wakati wa ujauzito kwa sababu ya kulinda ndoa zao, wanawajua waume zao wakikosa tendo kwa muda mrefu, watadesa nje......................

Mtambuzi I beg to differ na kwa hisani yako naomba uruhusu mods waipeleke kule kwa daktari tukaichambue hii kitu
 
Kujamiiana wakati wa ujauzito kuna madhara kwa mtoto aliye tumboni................ najua wapenda ngono watanibishia, lakini huo ndio ukweli wenyewe.
Ikumbukwe kwamba mtoto aliye tumboni hutumia pumzi ya mama, hivyo basi wakati tendo la ndoa linapofanyika na mama anapotaka kufika kileleni kunakuwa namabadiiko makubwa ya pumzi na hiyo humsababisha mtoto kuhangaika kule tumboni. inaelezwa kwamba wakati mwingine husababisha kifo cha mtoti tumboni...............

Wanawake wanalazimika kufanya tendo hilo wakati wa ujauzito kwa sababu ya kulinda ndoa zao, wanawajua waume zao wakikosa tendo kwa muda mrefu, watadesa nje......................

Mkuu Mchambuzi hapo kwenye nyekundu si kweli kwa mimba zote. Kama daktari ambaye anafuatilia mimba ya mjamzito hajaona dalili zote za hatari kwenye ujauzito basi hata siku moja hatatoa ushauri wa kuacha kujamiiana kwa kuwa ni hatari kwa mama mjazito au kiumbe mtarajiwa. Tena mara nyingi kama ujauzito hauna matatizo hushauri kujamiina hata mpaka dakika za mwisho mwisho maana huongeza njia na kusaidia mama mjamzito kujifungua kirahisi hasa kama ni yule anayetegemewa kujifungua kwa njia ya kawaida na siyo kwa visu, ila kama kuna mushkeli wowote katika ujauzito ambao unaweza kuhatarisha uhai wa mama na mtoto basi daktari huweza kuzuia tendo hilo kufanyika kabisa kwa kipindi chote cha ujauzito.
 
Mkuu Mchambuzi hapo kwenye nyekundu si kweli kwa mimba zote. Kama daktari ambaye anafuatilia mimba ya mjamzito hajaona dalili zote za hatari kwenye ujauzito basi hata siku moja hatatoa ushauri wa kuacha kujamiiana kwa kuwa ni hatari kwa mama mjazito au kiumbe mtarajiwa. Tena mara nyingi kama ujauzito hauna matatizo hushauri kujamiina hata mpaka dakika za mwisho mwisho maana huongeza njia na kusaidia mama mjamzito kujifungua kirahisi hasa kama ni yule anayetegemewa kujifungua kwa njia ya kawaida na siyo kwa visu, ila kama kuna mushkeli wowote katika ujauzito ambao unaweza kuhatarisha uhai wa mama na mtoto basi daktari huweza kuzuia tendo hilo kufanyika kabisa kwa kipindi chote cha ujauzito.

Labda nilichokosea ni kutoweka neno baadhi, lakini nilikuwa napinga swala la kwamba hakuna madhara kabisa............... kwa kuwa hakuna takwimu sahiihi zinazothibitisha vifo vya aina hiyo, labda ndio sababu wengi wanaona ni jambo lisilo na madhara, lakini yapo madhara kama nilivyoeleza. Hilo la kupanua njia, siamini kama daktari anaweza kutoa ushauri wa namna hiyo, kwamba ili kupanua njia ya uzazi ni lazima kujamiiana.......... Mimi nadhani Daktari analazimika kukubali baada yakuulizwa swali hilo na wanandoa kutokana na tamaa zetu za ngono.......... wewe unafikiri angejibu nini? Daktari amezaliwa na kulelewa katika jamii hii hii inayoamini kwamba jambo hilo halina madhara, kwa kuwa ameona wanandoa wako salama kushiriki, hana budi kukubali, labada tu pale ambapo ataona vinginevyo..........................
 
Labda nilichokosea ni kutoweka neno baadhi, lakini nilikuwa napinga swala la kwamba hakuna madhara kabisa............... kwa kuwa hakuna takwimu sahiihi zinazothibitisha vifo vya aina hiyo, labda ndio sababu wengi wanaona ni jambo lisilo na madhara, lakini yapo madhara kama nilivyoeleza. Hilo la kupanua njia, siamini kama daktari anaweza kutoa ushauri wa namna hiyo, kwamba ili kupanua njia ya uzazi ni lazima kujamiiana.......... Mimi nadhani Daktari analazimika kukubali baada yakuulizwa swali hilo na wanandoa kutokana na tamaa zetu za ngono.......... wewe unafikiri angejibu nini? Daktari amezaliwa na kulelewa katika jamii hii hii inayoamini kwamba jambo hilo halina madhara, kwa kuwa ameona wanandoa wako salama kushiriki, hana budi kukubali, labada tu pale ambapo ataona vinginevyo..........................

Ahsante sana Mkuu hapo kwenye blue, kwenye nyekundu Dr yeyote yule mwenye kufuata professional ethics za udaktari wake hatapindisha maneno kama anaona kuruhusu kujamiiana kunaweza kuhatarisha usalama kwa mjamzito na kiumbe mtarajiwa, kama daktari anawaruhusu ili kuwafurahisha tu na baadaye kukawa na tatizo kubwa ambalo chanzo chake kinaweza kuthibitishwa kwamba ni kujamiiana na ambapo dr alitakiwa asiwaruhusu basi Dr anaweza kabisa kufunguliwa mashtaka na pia hata kupoteza haki yake ya kufanya kazi kama daktari.
 
Back
Top Bottom