MAMMAMIA
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 3,811
- 1,603
Siku alipokuwa akitangaza majina ya wajumbe wa tume ya katiba, Kikwete alisema kuwa "Wananchi wajadili katiba, wasijadili Muungano" na akasisitiza kuwa watakaojadili Muungano watachukuliwa hatua kali.
Naye Waziri Mkuu juzi katika hotuba yake alipokuwa akizungumzia suala la mchakato wa katiba mpya, alilisitiza hilo, kuwa ni suala la katiba na sio Muungano.
Wasiwasi wangu, ikiwa nimeelewa dhamira ya maneno yao, tutawezaje kujadili katiba bila ya kujadili Katiba Mpya (ya Muungano) bila ya kujadili Muungano?. Ukiipitia katiba yetu kuanzia jina lake "KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA" hadi vipengele vyote vilivyomo ndani, vinahusu masuala ya Muungano, serikali, utendaji wake...iweje leo tuanaamiwa tujadili katiba tusijadili Muungano?
Naomba michango na msaada wenu.
Naye Waziri Mkuu juzi katika hotuba yake alipokuwa akizungumzia suala la mchakato wa katiba mpya, alilisitiza hilo, kuwa ni suala la katiba na sio Muungano.
Wasiwasi wangu, ikiwa nimeelewa dhamira ya maneno yao, tutawezaje kujadili katiba bila ya kujadili Katiba Mpya (ya Muungano) bila ya kujadili Muungano?. Ukiipitia katiba yetu kuanzia jina lake "KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA" hadi vipengele vyote vilivyomo ndani, vinahusu masuala ya Muungano, serikali, utendaji wake...iweje leo tuanaamiwa tujadili katiba tusijadili Muungano?
Naomba michango na msaada wenu.