Kuhusu kozi ya kusomea chuo kikuu, Nimesomea PCM

nimahussein

Senior Member
Sep 17, 2013
181
26
Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 29 nilimaliza kidato cha nne mwaka 2002 na kufanikiwa kupata division1 ya 14 na nikafanya Advance level mwaka 2006 PCM na kupata division 2 ya 12 (Phy E, chem C na Advance math E) baada ya kumaliza form6 nilipata tamaa ya kusafiri kwenda kutafuta maisha ughaibuni lakini mambo yangu hayakwenda kama nilivyotaka niliishia kubeba box na sikufanikiwa kupata permit ya kuishi.

Now nimerudi hapa nyumbani Tanzania na nimeona kitu ambacho kinanitoa kwa upande wangu ni elimu.

Nahitaji mawazo yenu nisomee course gani ambayo ipo katika market hapa kwetu? Mimi katika mawazo yangu ambazo hata nje zina soko ni Geomatics, civil engineering, renewable energy, oil and gas, quantity surveying na electrical engineering.

Naomba mawazo yenu maana umri nao unaanza kunitupa mkono nisije nikafail tena..
Shukran sana.
 
Nakushauri uanze kusoma diploma Civil Engineering kati ya vyuo vifuatavyo Arusha tech,Mbeya University,DIT upate uzoefu kabla first degree.Ukifaulu vizuri unaweza kujiunga na chuo chochote either nchini au abroad.
 
Nikiwa na hio diploma ya civil naweza kufanya kazi hapa tanzania au ndio mpaka umalize degree
 
Nakushauri uanze kusoma diploma Civil Engineering kati ya vyuo vifuatavyo Arusha tech,Mbeya University,DIT upate uzoefu kabla first degree.Ukifaulu vizuri unaweza kujiunga na chuo chochote either nchini au abroad.
Nikiwa na hio diploma ya civil naweza kufanya kazi hapa tanzania au ndio mpaka umalize degree
 
Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 29 nilimaliza kidato cha nne mwaka 2002 na kufanikiwa kupata division1 ya 14 na nikafanya Advance level mwaka 2006 PCM na kupata division 2 ya 12 (Phy E, chem C na Advance math E) baada ya kumaliza form6 nilipata tamaa ya kusafiri kwenda kutafuta maisha ughaibuni lakini mambo yangu hayakwenda kama nilivyotaka niliishia kubeba box na sikufanikiwa kupata permit ya kuishi.

Now nimerudi hapa nyumbani Tanzania na nimeona kitu ambacho kinanitoa kwa upande wangu ni elimu.

Nahitaji mawazo yenu nisomee course gani ambayo ipo katika market hapa kwetu? Mimi katika mawazo yangu ambazo hata nje zina soko ni Geomatics, civil engineering, renewable energy, oil and gas, quantity surveying na electrical engineering.

Naomba mawazo yenu maana umri nao unaanza kunitupa mkono nisije nikafail tena..
Shukran sana.
If you don't mind try also telecommunication engineering kwa sasa inalipa sana nyumbani na nje. Mimi nafanyakazi nje ya nchi kwa muda mrefu na nimeona vijana wa kitanzania wakifanyakazi hizo na makampuni ya simu huko Uganda, South Sudan, Senegal. Ni field inayolipa sana hata UN.
 
If you don't mind try also telecommunication engineering kwa sasa inalipa sana nyumbani na nje. Mimi nafanyakazi nje ya nchi kwa muda mrefu na nimeona vijana wa kitanzania wakifanyakazi hizo na makampuni ya simu huko Uganda, South Sudan, Senegal. Ni field inayolipa sana hata UN.
Thanx mkuu,nitaiweka katika shortlist na hio
 
Nakushauri uanze kusoma diploma Civil Engineering kati ya vyuo vifuatavyo Arusha tech,Mbeya University,DIT upate uzoefu kabla first degree.Ukifaulu vizuri unaweza kujiunga na chuo chochote either nchini au abroad.
kwanini nisiombe degree ya civil engineering moja kwa moja mkuu..
 
Ngoja nikumegee kidogo, kijana kama wewe wa kutoka kijijini kwetu amepitia shida nyingi sana na hata kupata kufungwa kwakuhusika na kula pesa za kijiji yeye akiwa kama mtendaji wa kijiji na baada ya kutoka jela mke wake kumkimbia na kuchukuliwa na mwanaume mwingine na kumwachia watoto wa wawili na life kuwa tough sana. Kijikwaa si kuanguka ndivyo ninavyoamini, background ya huyo kijana naifahamu sana sina haja ya kuielezea ila ninaimani ni kijana mweye akili nzuri kwani alipata one o-level na two A-level (PCM). Nilipatwa na uchungu na nikaamua kumsaidia, lakini nilimshawishi arudi shule tena na alikubali. Nlimshauri achukue electronic and telecommunication enginering katika kile chuo cha Wahindi kule Mbezi ya Morogoro road, anachukua Diploma hakuweza kuchukuliwa kwenye degree kwakuwa ni miaka mingi sana alimaza A-level. Namlipia 100% fees, kula, kulala (nimempangishia nyumba) malipo yake kwangu ni kufaulu kwake tu. Mimi ninamdogo wangu pia anafani hiyo na kwa sasa ni technical director wa SMART Phone HQ Kampala, kuna Watanzania watatu wanafanyakazi hiyo na MTN Juba. Kuna watu wengi wanafanyakazi kama Tel enginers na UN kwakuwa mawasiliano siku hizi yanaumuhimu wa pekee. Ni kozi tough lakini nahisi inalipa, fanya maamuzi ya busara ila kama qualification zako ni poa anza na degree na si diploma. Kila la kheri bwana mdogo na Mungu akufanyie wepesi, maamuzi uliyoyafanya hutayajutia kwakuwa miaka mitatu hadi minne si kitu uta make difference. All the best.
 
kaka wewe kwanza kwa hayo matokeo ya form six uliyoyataja division two ya point kumi na mbili huwezi kuipata..wewe muongo..kwa hio mie sishauriani ni waongo
 
Soma engineering yeyote kati ya hizi..(mechanical,electrical au civil) trust me hutojutia!! Sikushauri kusoma telecom kwa kweli kwa kipindi hiki,kibongo bongo ajira zimekuwa chache coz vijana wengi wameivamia... all the best!!
 
Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 29 nilimaliza kidato cha nne mwaka 2002 na kufanikiwa kupata division1 ya 14 na nikafanya Advance level mwaka 2006 PCM na kupata division 2 ya 12 (Phy E, chem C na Advance math E) baada ya kumaliza form6 nilipata tamaa ya kusafiri kwenda kutafuta maisha ughaibuni lakini mambo yangu hayakwenda kama nilivyotaka niliishia kubeba box na sikufanikiwa kupata permit ya kuishi.

Now nimerudi hapa nyumbani Tanzania na nimeona kitu ambacho kinanitoa kwa upande wangu ni elimu.

Nahitaji mawazo yenu nisomee course gani ambayo ipo katika market hapa kwetu? Mimi katika mawazo yangu ambazo hata nje zina soko ni Geomatics, civil engineering, renewable energy, oil and gas, quantity surveying na electrical engineering.

Naomba mawazo yenu maana umri nao unaanza kunitupa mkono nisije nikafail tena..
Shukran sana.

EEC(PCM)=div2:12
mbona nikipiga hesabu sipati div 2:12
 
kaka wewe kwanza kwa hayo matokeo ya form six uliyoyataja division two ya point kumi na mbili huwezi kuipata..wewe muongo..kwa hio mie sishauriani ni waongo
Sawa ila kabla ya kuniita muongo ungetumia busara ya kuniuliza,nidanganye ili iweje?kifupi nimekosea advanc math D,ila sihitataji ushauri wako nimeshashauriwa na walio na busara
 
Soma engineering yeyote kati ya hizi..(mechanical,electrical au civil) trust me hutojutia!! Sikushauri kusoma telecom kwa kweli kwa kipindi hiki,kibongo bongo ajira zimekuwa chache coz vijana wengi wameivamia... all the best!!
Basi nitaangalia hio civil engineering ila ndio hvy qualification maana nasikia siku hizi wanafaulu sana tofauti na enzi zetu
 
Back
Top Bottom