Kuhusu Joseph Mungai

Mungai aja juu

2008-11-24 16:48:04
Na Emmanuel Lengwa, Jijini


Mbunge wa CCM wa jimbo la Mufindi Kaskazini, Mheshimiwa Joseph James Mungai, ambaye Ijumaa wiki iliyopita alilipukiwa na mkazi mmoja wa Jijini, akimtuhumu kwamba ni fisadi, ameeleza kusikitishwa kwake na kauli hiyo, na akasema madai hayo siyo ya kweli.

Tuhuma hizo zilielekezwa kwake na Bw. Renatus Mkinga wakati akichangia mada kwenye kipindi cha Kipimajoto, kinachorushwa `live` na kituo cha luninga cha ITV.

Katika madai yake, Bw. Mkinga alidai kuwa Mhe. Mungai akiwa Wizara ya Elimu na Utamaduni, ulitokea wizi wa fedha zaidi ya shilingi bilioni tatu , mali ya wizara hiyo.

Akadai kuwa punde tu wizi huo ulipotokea, mfanyakazi mmoja wa Wizara hiyo ambaye Bw. Mkinga hakumtaja jina, aligundua na kutoa taarifa ili hatua zaidi zichukuliwe.

Bw. Mkinga alizidi kudai kuwa badala ya Waziri Mungai kufuatilia taarifa hizo, alikanusha kuwa hakuna wizi uliotokea na kuchukua hatua ya kumtimua kazi mfanyakazi huyo aliyebaini upotevu wa fedha.

Hata hivyo Mhe. Mungai leo amenusha madai hayo.
``Kamwe sijawahi kutuhumiwa kwa jambo lolote…hilo lililosemwa silijui wala halijawahi kunitokea,`` amesema Mheshimiwa Mungai.

Amesema wakati akiwa Waziri wa Elimu na Utamaduni, aliiongoza wizara hiyo kwa uadilifu na uzalendo mkubwa kwa maslahi ya taifa na hakuwahi kufanya hujuma ya aina yeyote.

Kipindi hicho ya Kipimajoto kinachorushwa na ITV kila Ijumaa, wiki iliyopita kilikuwa kikijadili mada ya ``Nini kifanyike kupata suluhu ya migomo ya wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu
 
Kama atakimbia ni kazi bure kwani Serikali ina mkono mrefu na mali zote alizoiba zitakamatwa tu.Viongozi wetu walijisahau na kuanza kujifanyia watakavyo sasa wavune walichopanda.Mimi nathani JK ameamua hakuna atakayepona kwa uhujumu alioufanya kwa taifa letu.
 
Mungai anaingia hapa mjini Dar leo usiku kwa KLM. Amekatisha safari yake USA kwa takribani wiki mbili. Bimdogo na watoto hawakupata visa, hivyo hawakuweza kuondoka, mipango ikafa. Taarifa ni kuwa siyo suala la Elimu au Mambo Ya Ndani vinavyomtatiza na kumpa kihoro. Inagusa masuala ya Kilimo, ruzuku za mbolea, uuzwaji wa mashamba Kilosa, Iringa vijijini, Mufindi yanayomgusa Chenge, Lowasa, Maj Gen Luhanga na mzungu mmoja anaitwa Asprem. Malipo yanapitia CRDB na Stanbic. Details zaidi zinatafutwa.
 
Joseph James Mungai Mbunge tarehe 3/1/2009 alifanya kufuru Mjini Iringa baada ya kumtumia wakala wake kunadi jengo lilliopo manispaa ya Iringa kwa shs 315m.Jengo likithaminiwa halizidi shs 200m .
Jengo hilo lilikuwa na milikiwa na Ndg Zaid baraka alikuwa akidaiwa na Mamlaka ya Kodi TRA ,lilipo eneo la Gangilonga kiwanja na 21 zone 2,wakala huyo wa Mungai aliwaacha watazamaji na wafanyabisahara hoi,baada ya kulinadi jengo hilo kwa bei ya juu !wakala huyo wa Mungai aliyejulikana Kama Ndg Vitus Mushi aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM manispaa ya iringa
Baada ya hapo alitakiwa kulipa asilimia 25% jambo ambalo alilifanya na kupewa risiti iliyoandikwa
Receiced from JOSEPH JAMES MUNGAI shs 78.750.000/-ikiwa asilmia 25% ya alichokinadi .
Huyo ndiye Joseph James Mungai!!
 
Joseph James Mungai Mbunge tarehe 3/1/2009 alifanya kufuru Mjini Iringa baada ya kumtumia wakala wake kunadi jengo lilliopo manispaa ya Iringa kwa shs 315m.Jengo likithaminiwa halizidi shs 200m .
Jengo hilo lilikuwa na milikiwa na Ndg Zaid baraka alikuwa akidaiwa na Mamlaka ya Kodi TRA ,lilipo eneo la Gangilonga kiwanja na 21 zone 2,wakala huyo wa Mungai aliwaacha watazamaji na wafanyabisahara hoi,baada ya kulinadi jengo hilo kwa bei ya juu !wakala huyo wa Mungai aliyejulikana Kama Ndg Vitus Mushi aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM manispaa ya iringa
Baada ya hapo alitakiwa kulipa asilimia 25% jambo ambalo alilifanya na kupewa risiti iliyoandikwa
Receiced from JOSEPH JAMES MUNGAI shs 78.750.000/-ikiwa asilmia 25% ya alichokinadi .
Huyo ndiye Joseph James Mungai!!

Mkuu heshima mbele. Hebu tufafanulie zaidi . Hivi Mungai kanunua au kanadi? Mimi naona kunadi ni kuuza kitu kwa mnada. Ukitoa ofa kwenye mnada nako kunaitwa kunadi? Haijakaa sawa nafikiri. Wataalam wa lugha njooni huku.
 
Joseph James Mungai Mbunge tarehe 3/1/2009 alifanya kufuru Mjini Iringa baada ya kumtumia wakala wake kunadi jengo lilliopo manispaa ya Iringa kwa shs 315m.Jengo likithaminiwa halizidi shs 200m .
Jengo hilo lilikuwa na milikiwa na Ndg Zaid baraka alikuwa akidaiwa na Mamlaka ya Kodi TRA ,lilipo eneo la Gangilonga kiwanja na 21 zone 2,wakala huyo wa Mungai aliwaacha watazamaji na wafanyabisahara hoi,baada ya kulinadi jengo hilo kwa bei ya juu !wakala huyo wa Mungai aliyejulikana Kama Ndg Vitus Mushi aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM manispaa ya iringa
Baada ya hapo alitakiwa kulipa asilimia 25% jambo ambalo alilifanya na kupewa risiti iliyoandikwa
Receiced from JOSEPH JAMES MUNGAI shs 78.750.000/-ikiwa asilmia 25% ya alichokinadi .
Huyo ndiye Joseph James Mungai!!

mbona post yako hii haieleweki?
 
Mungai anaingia hapa mjini Dar leo usiku kwa KLM. Amekatisha safari yake USA kwa takribani wiki mbili. Bimdogo na watoto hawakupata visa, hivyo hawakuweza kuondoka, mipango ikafa. Taarifa ni kuwa siyo suala la Elimu au Mambo Ya Ndani vinavyomtatiza na kumpa kihoro. Inagusa masuala ya Kilimo, ruzuku za mbolea, uuzwaji wa mashamba Kilosa, Iringa vijijini, Mufindi yanayomgusa Chenge, Lowasa, Maj Gen Luhanga na mzungu mmoja anaitwa Asprem. Malipo yanapitia CRDB na Stanbic. Details zaidi zinatafutwa.
Je thread hii ina uhusiano na ile ya ununuzi wa ghorofa?
 
Hii posting imechanganywa maneno halafu ikajichanganya kabisa.

Let me guess,

'Mungai amenunua Jengo kwenye mnada wa hadhara kwa Shs. Mil.315'

Kama hivyo ndivyo, hebu eleza kwa kinadaga ubaga kama ni tatizo kwako au vipi?
 
Hii posting imechanganywa maneno halafu ikajichanganya kabisa.

Let me guess,

'Mungai amenunua Jengo kwenye mnada wa hadhara kwa Shs. Mil.315'

Kama hivyo ndivyo, hebu eleza kwa kinadaga ubaga kama ni tatizo kwako au vipi?

bado kuna michanganyo. Thamani ya jengo ni sh mil 200, Mungai anejikaanga kwa mil 315! Wendawazimu gani umemfanya anunue jengo la bei rahisi kwa bei ghali namna hiyo?
 
Mungai kafanya kufuru, kanunua jengo kwenye mnada kwa bei maradufu tena akiwa marekani, tatizo ni lipi? Mungai ni mwekezaji wa siku nyingi, mkurugenzi na mmiliki wa tatepa, kampuni ya chai ,tajiri sana
 
bado kuna michanganyo. Thamani ya jengo ni sh mil 200, Mungai anejikaanga kwa mil 315! Wendawazimu gani umemfanya anunue jengo la bei rahisi kwa bei ghali namna hiyo?

Mpita Njia,
Ukisoma vizuri hiyo thamani anayoitaja mtoa taarifa haina nguvu yeyote kwani ni mawazo yake ambayo hatuwezi kuya-quantify kwani siyo facts.

Hata kama hilo jengo lingekuwa thaminiwa kwa Shs. Mil 200 haizuii nguvu ya mnada kulinadi kwa zaidi ya thamani ya makaratasi, kumbuka soko nalo lina nguvu zake.

Hebu tujiulize, zile nyumba za mbavu za mbwa hapo Kariakoo zinauzwa sawasawa na zile za Sinza?
 
Niliposoma mara ya kwanza, nilifikiri Mungai kauza jengo baada ya kukimbilia USA. Imebidi nisome mara kibao ili kuelewa nini kinaongelewa hapa.

Kuna kosa gani kama amenunua kwa bei kubwa? Labda yeye analitaka sana hilo jengo. Pia kuna uhusiano gani na yeye kuwa USA kwenye hili?
 
Hii posting imechanganywa maneno halafu ikajichanganya kabisa.

Let me guess,

'Mungai amenunua Jengo kwenye mnada wa hadhara kwa Shs. Mil.315'

Kama hivyo ndivyo, hebu eleza kwa kinadaga ubaga kama ni tatizo kwako au vipi?

Ndugu Pundamilia, kama ulivyo guess kuwa Mungai ndio kanunua. Lakini bado kuna maswali, manake mleta hoja anasema Mungai alimtumia wakala wake kunadi jengo kwa 315m ambalo likithaminiwa halizidi 200m. Ina maana hapa Mungai ndio kauza na si kununua, na hii yaweza kuthibitishwa alipomlipa huyo wakala wa kunadi 25%. Lakini bado na huyu Ndg Zaid baraka aliyeandikwa alikuwa akidaiwa na Mamlaka ya Kodi TRA, anaingiaje tena hapa???.

Nadhani Sir Leem aje tena aweke wazi hoja yake, inachanganya mno!!
 
Mpita Njia,
Ukisoma vizuri hiyo thamani anayoitaja mtoa taarifa haina nguvu yeyote kwani ni mawazo yake ambayo hatuwezi kuya-quantify kwani siyo facts.

Hata kama hilo jengo lingekuwa thaminiwa kwa Shs. Mil 200 haizuii nguvu ya mnada kulinadi kwa zaidi ya thamani ya makaratasi, kumbuka soko nalo lina nguvu zake.

Hebu tujiulize, zile nyumba za mbavu za mbwa hapo Kariakoo zinauzwa sawasawa na zile za Sinza?

Ewaaaaa, nadhani sasa mtoa mada atakuwa ameshaanza kuelewa maana watuw alianza kwa kumshangaa badala ya kutoa ufafanuzi kama huu
 
Joseph James Mungai Mbunge tarehe 3/1/2009 alifanya kufuru Mjini Iringa baada ya kumtumia wakala wake kunadi jengo lilliopo manispaa ya Iringa kwa shs 315m.Jengo likithaminiwa halizidi shs 200m .
Jengo hilo lilikuwa na milikiwa na Ndg Zaid baraka alikuwa akidaiwa na Mamlaka ya Kodi TRA ,lilipo eneo la Gangilonga kiwanja na 21 zone 2,wakala huyo wa Mungai aliwaacha watazamaji na wafanyabisahara hoi,baada ya kulinadi jengo hilo kwa bei ya juu !wakala huyo wa Mungai aliyejulikana Kama Ndg Vitus Mushi aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM manispaa ya iringa
Baada ya hapo alitakiwa kulipa asilimia 25% jambo ambalo alilifanya na kupewa risiti iliyoandikwa
Receiced from JOSEPH JAMES MUNGAI shs 78.750.000/-ikiwa asilmia 25% ya alichokinadi .
Huyo ndiye Joseph James Mungai!!

Mkuu
Sasa nakubali Kiswahili nacho Watanzania kinatupa shida. Kunadi vs kununua, wakala vs mdaiwa. Sir Leem, unaweza kutueleza kwa lugha nyingine tukaelewa hata kama tutahitaji mkalimani?
 
Ndugu Pundamilia, kama ulivyo guess kuwa Mungai ndio kanunua. Lakini bado kuna maswali, manake mleta hoja anasema Mungai alimtumia wakala wake kunadi jengo kwa 315m ambalo likithaminiwa halizidi 200m. Ina maana hapa Mungai ndio kauza na si kununua, na hii yaweza kuthibitishwa alipomlipa huyo wakala wa kunadi 25%. Lakini bado na huyu Ndg Zaid baraka aliyeandikwa alikuwa akidaiwa na Mamlaka ya Kodi TRA, anaingiaje tena hapa???.

Nadhani Sir Leem aje tena aweke wazi hoja yake, inachanganya mno!!

Mfumwa,
Kabla ya mtoa taarifa hajarudi kuweka sawa posting yake, mimi nimeeelewa kama hivi;

1)Zaid Mbaraka ndiye alikuwa mmiliki wa Jengo lililopigwa mnada

2)Zaid Mbaraka huenda alikuwa anadaiwa na TRA

3)Mungai ndiye aliyeshinda bid ya juu kabisa katika mnada huo

4)Kwenye mnada huo transactions za ununuzi zilifaywa na Mushi (wakala) kwa niaba ya Mungai (mmiliki mpya).

Nadhani nimetjitahidi kumsoma mtoa hoja.

Uwakala sitatizo kabisa, kwani watu huaminiana hata kumtuma rafiki yake kwenda Unguja kumwolea, halafu akaletewa mke tayari ndoa imeshafungwa ati!!!
 
Back
Top Bottom