Kuharibika kwa ndoa na ulezi wa mtoto

O-man

JF-Expert Member
Nov 17, 2011
323
65
Yupo kijana ameniletea hii changamoto. Mke anadai talaka baada ya ndoa (ya Kiislamu) isiyozidi miaka miwili. Hiyo kwake si hoja kwa sababu mke ameamua hata baada ya vikao vitatu vya usuluhishi. Baba anataka mto wake wa kiume wa miezi 8. Mke anasema asubiri mpaka atimize miaka 18 na katika muda huo awe anapeleka matunzo ya sh. 150,000 kwa mwezi. Hii imekaaje wakuu?
 
unfortunately mtoto mdogo kama huyo anakaa na mama yake... huyo baba akibakia nae siku akienda bar au kwa kimada yake atamuachia nani mtoto...
 
Sawa mkuu. Wazazi wa huyu kijana, ambao wote wapo, wamekubali kumlea huyo mtoto.
 
Kwani sheria inasemaje?nijuavyo mie kuanzia miaka 7 ndio mtoto anaweza kuchukuliwa na baba kama ndoa imevunjika,kwa umri huo lazima alelewe na mama
 
Back
Top Bottom