KUFURU: Gharama za matibabu ya viongozi wastaafu ni BILLIONI 9

Mkurabitambo

JF-Expert Member
Feb 3, 2010
230
57
Bunge linaloendelea na kikao chake mjini Dodoma, juzi liliambiwa kwamba Serikali imetenga Sh9 bilioni kwa ajili ya kugharamia matibabu ya viongozi wakuu wastaafu. Akihitimisha mjadala wa hotuba yake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais anayeshughulikia Menejimenti na Utumishi wa Umma, Celina Kombani alisema fedha hizo ni kwa ajili ya wastaafu wanaopaswa kutunzwa na Serikali.

Bila kuelezea suala hilo kwa undani, Waziri Kombani alisema tu kwamba kiwango hicho kimepungua mwaka huu kutoka Sh10 bilioni zilizotengwa mwaka jana hadi Sh9 bilioni mwaka huu kutokana na idadi ya viongozi wastaafu wanaopaswa kuhudumiwa na Serikali kupungua. Wastaafu wanaoangukia katika fungu hilo ni marais Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa.

Mawaziri wakuu wastaafu ni Joseph Warioba, Samuel Malecela, Cleopa Msuya, Salim Ahmed Salim na Edward Lowasa. Waziri Kombani hakuwataja viongozi wastaafu waliopungua, lakini sote tunafahamu fika kwamba Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere na Mzee Rashid Mfaume Kawawa tayari wametangulia mbele ya haki.

Bila shaka takwimu hizo zitakuwa zimewashangaza wengi kutokana na wingi wa fedha zinazotengwa kila mwaka kugharamia tu matibabu ya viongozi, bila kutilia maanani fedha nyingine nyingi zinazotengwa kama mafao ya viongozi hao wastaafu. Kwa akili ya kawaida, fedha hizo ni nyingi mno kulinganisha na idadi ya viongozi waliokusudiwa na takwimu hizo zinaacha maswali mengi kuliko majibu.

Tunasema hivyo kwa sababu hatuoni jinsi kiasi hicho kikubwa cha fedha kinaweza kugharamia matibabu ya idadi ndogo sana ya viongozi wetu wastaafu, kwani siyo siri pia kwamba wastaafu wetu wengi wamekuwa wakipatwa na maradhi ya kawaida ambayo siyo tu hayahitaji fedha nyingi kuyatibu, bali pia yangeweza kupata tiba hapa nchini. Ndiyo maana tunasema vifungu vikubwa vya fedha zinazotengwa kila mwaka kwa shughuli hiyo siyo tu vinatia shaka, bali pia vinaacha ukungu na kiza kinene vikiwa vimetanda.

Sisi hatusemi kwamba viongozi wetu hao wastaafu hawastahili kupata matibabu kwa kodi zetu. Tunachosema hapa ni kwamba gharama za matibabu yao hazipaswi kuwa siri au kuacha shaka hata kama wastaafu hao walitutumikia vizuri wakati wa utawala wao. Ni sahihi kabisa kwamba walipakodi wangetaka kujua kodi zao zinavyotumika kuwagharimia viongozi wao.

Bado tunasisitiza kwamba Sh9 billioni kwa matibabu ya viongozi hao wastaafu siyo tu ni nyingi mno, bali pia ni kufuru na za kufikirika. Takwimu hizo hazijumliki hata kidogo. Ni matibabu yapi yenye gharama hata robo ya kiasi hicho kilichotengwa, hata ukiweka usafiri, malazi na gharama nyingine? Ni kichekesho kwamba fedha hizo zimepitishwa na Bunge.



Source : Mwananchi
 
Dah kaka umeesomeka lkn kuna pahala unatuchanganya heading yako watuambia ni Bil.9 alafu ndani unakuja kusema Tril. 9 sasa tushike lipi?
Na ktk hao wastaafu umesahau kumuweka Mama Maria Nyerere naye yupo kwenye kundi hilo kwa heshma yake kama Mama wa Taifa hili ana hilo rungu na ndio maana hadi leo Utumishi wana mhudumia yule Mama kwa kila kitu ambacho alipaswa Hayati Mwl JKN akipate anakipata yule Mama"
 
Jamani kwa nchi zetu masikini muda wa rais kuwa madarakani ungeongezwa kutoka miaka 10 hadi 20.vinginevyo tutakua na utitiri wa viongozi wastaafu vijana wa kuwahudumia
 
Mimi namfahamu mwanajeshi mmoja alikuwa na cheo hivi...yaani yeye mpaka na mke wake huwa wanapelekwa India kwa matibabu...! chezea viongozi wenye akili ndogo weye...
 
Hiyo ndiyo bongo ,NDIO MAANA VIONGOZI WETU WAMEGOMA KUTATUA MGOMO WA MADAKTARI.WANABAJETI ZA KODI ZA KUTIBIWA NJE KUANZIA MAFUA HADI KUPASULIWA.MANAENDA NJE WANAJUA HAPA HAKUNA VIFAA,MSANII SAJUKI ALIKUWA ANASUBIRIA MAUPI,DR.ULIMBOKA KAKIMBIZWA SAUZ,DR,MWAKYEMBE INDIA NA WENGINEO.MADAKITARI BINGWA TUNAO TATIZO VIFAA ,VINGEKUWA MAGARI,RISASI,MWENGE,BUNDUKI AU UCHAGUZI PESA ISINGEKUWA TATIZO.FIKIRIA MAGARI YA KIFAHARI YA SERIKALI NUSU YAKE TU VINGEKUWA VIFAA,MPAKA HOSPITALI ZA KATA ZINGEFANYA UPASUAJI.
 
Kwa hiyo hizo bil. 10 za mwaka jana ziliisha zote au, zikibaki inakuwaje, eeh, hizi ni hela za kutibu watu au mitambo, viongozi gani wa kubwa na wangapi mwaka jana, ulisikia wanaumwa seriously, au wakifa ghafla huwa zinatumika kwa mazishi pia, hivi kweli hawa watu hawajiwezi katika kujigharamia matibabu yao madogo madogo ya hospitali, hata watoto wao wanaweza kuwasaidia kwenye ugonjwa mdogo mdogo, hizo fedha zikasaidia wale wasiojiweza kwelikweli, Ocean Road na kwingineko
Bunge linaloendelea na kikao chake mjini Dodoma, juzi liliambiwa kwamba Serikali imetenga Sh9 bilioni kwa ajili ya kugharamia matibabu ya viongozi wakuu wastaafu. Akihitimisha mjadala wa hotuba yake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais anayeshughulikia Menejimenti na Utumishi wa Umma, Celina Kombani alisema fedha hizo ni kwa ajili ya wastaafu wanaopaswa kutunzwa na Serikali.

Bila kuelezea suala hilo kwa undani, Waziri Kombani alisema tu kwamba kiwango hicho kimepungua mwaka huu kutoka Sh10 bilioni zilizotengwa mwaka jana hadi Sh9 bilioni mwaka huu kutokana na idadi ya viongozi wastaafu wanaopaswa kuhudumiwa na Serikali kupungua. Wastaafu wanaoangukia katika fungu hilo ni marais Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa.

Mawaziri wakuu wastaafu ni Joseph Warioba, Samuel Malecela, Cleopa Msuya, Salim Ahmed Salim na Edward Lowasa. Waziri Kombani hakuwataja viongozi wastaafu waliopungua, lakini sote tunafahamu fika kwamba Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere na Mzee Rashid Mfaume Kawawa tayari wametangulia mbele ya haki.

Bila shaka takwimu hizo zitakuwa zimewashangaza wengi kutokana na wingi wa fedha zinazotengwa kila mwaka kugharamia tu matibabu ya viongozi, bila kutilia maanani fedha nyingine nyingi zinazotengwa kama mafao ya viongozi hao wastaafu. Kwa akili ya kawaida, fedha hizo ni nyingi mno kulinganisha na idadi ya viongozi waliokusudiwa na takwimu hizo zinaacha maswali mengi kuliko majibu.

Tunasema hivyo kwa sababu hatuoni jinsi kiasi hicho kikubwa cha fedha kinaweza kugharamia matibabu ya idadi ndogo sana ya viongozi wetu wastaafu, kwani siyo siri pia kwamba wastaafu wetu wengi wamekuwa wakipatwa na maradhi ya kawaida ambayo siyo tu hayahitaji fedha nyingi kuyatibu, bali pia yangeweza kupata tiba hapa nchini. Ndiyo maana tunasema vifungu vikubwa vya fedha zinazotengwa kila mwaka kwa shughuli hiyo siyo tu vinatia shaka, bali pia vinaacha ukungu na kiza kinene vikiwa vimetanda.

Sisi hatusemi kwamba viongozi wetu hao wastaafu hawastahili kupata matibabu kwa kodi zetu. Tunachosema hapa ni kwamba gharama za matibabu yao hazipaswi kuwa siri au kuacha shaka hata kama wastaafu hao walitutumikia vizuri wakati wa utawala wao. Ni sahihi kabisa kwamba walipakodi wangetaka kujua kodi zao zinavyotumika kuwagharimia viongozi wao.

Bado tunasisitiza kwamba Sh9 billioni kwa matibabu ya viongozi hao wastaafu siyo tu ni nyingi mno, bali pia ni kufuru na za kufikirika. Takwimu hizo hazijumliki hata kidogo. Ni matibabu yapi yenye gharama hata robo ya kiasi hicho kilichotengwa, hata ukiweka usafiri, malazi na gharama nyingine? Ni kichekesho kwamba fedha hizo zimepitishwa na Bunge.



Source : Mwananchi
 
Swali la kujiuliza, bajeti iliyowekwa KWA ajili ya watanzania MILIONI 40, dhidi ya VIONGOZI wastaafu 8, eh Mungu uliye mwingi wa rehma legeza mioyo ya wote, Maono yaelekezwe KWA watanzania wAlio wengi, Ameeeeeeeeeeeeeeeeen!!!!!!!!!!!!!!!
 
Kwa hiyo hizo bil. 10 za mwaka jana ziliisha zote au, zikibaki inakuwaje, eeh, hizi ni hela za kutibu watu au mitambo, viongozi gani wa kubwa na wangapi mwaka jana, ulisikia wanaumwa seriously, au wakifa ghafla huwa zinatumika kwa mazishi pia, hivi kweli hawa watu hawajiwezi katika kujigharamia matibabu yao madogo madogo ya hospitali, hata watoto wao wanaweza kuwasaidia kwenye ugonjwa mdogo mdogo, hizo fedha zikasaidia wale wasiojiweza kwelikweli, Ocean Road na kwingineko

Swali zuri Doreen22 maana kuugua ni tofauti na kuchimba visima yaani kama umepanga kujimba visima 2000 kwa kiasi flani lazima uchimbe na ela iliyotengwa inaweza kuisha au kuzidi lakini kwenye kuugua inategemea maana si wote wanaweza kuugua na tunategemea ela inaweza kubaki japokuwa kwa nchi yetu kwa kuwa budget imepangwa utaona mtu anajilazimisha kuitumia ela (au swali la kuuliza lingine hizo ela wanapewa kama allowance au nini maana kitendo cha kupunguza toka 10 bilion to 9 bilion inaonyesha kama wanapewa directly as allowance, kama ni hivyo nadhani itabidi tuwakatie BIMA YA AFYA
 
Back
Top Bottom